< Ezra 7 >

1 Baada ya mambo haya, wakati wa utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,
Po tych wydarzeniach, za panowania Artakserksesa, króla Persji, Ezdrasz, syn Serajasza, syna Azariasza, syna Chilkiasza;
2 mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
Syna Szalluma, syna Sadoka, syna Achituba;
3 mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,
Syna Amariasza, syna Azariasza, syna Merajota;
4 mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
Syna Zerachiasza, syna Uzziego, syna Bukkiego;
5 mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Aroni.
Syna Abiszui, syna Pinchasa, syna Eleazara, syna Aarona, najwyższego kapłana;
6 Huyu Ezra alipanda kutoka Babeli. Alikuwa mwalimu mwenye ujuzi mzuri katika sheria ya Mose, ambayo Bwana, Mungu wa Israeli, alikuwa ametoa. Mfalme alikuwa amempa Ezra kila kitu alichoomba, kwa maana Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
Tenże Ezdrasz wyruszył z Babilonu, a był człowiekiem uczonym w prawie Mojżesza, które dał PAN, Bóg Izraela. A król spełnił wszystkie jego prośby, gdyż ręka PANA, jego Boga, była nad nim.
7 Pia baadhi ya Waisraeli, wakiwemo makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu na watumishi wa Hekalu, nao walikuja Yerusalemu mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
Wyruszyli też [niektórzy] z synów Izraela oraz z kapłanów, Lewitów, śpiewaków, odźwiernych i z Netinitów do Jerozolimy w siódmym roku króla Artakserksesa.
8 Ezra aliwasili Yerusalemu mwezi wa tano wa mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
[Ezdrasz] przybył do Jerozolimy w piątym miesiącu – było to w siódmym roku króla.
9 Ezra alianza safari yake kutoka Babeli tangu siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akawasili Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa maana mkono wa neema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.
Wyruszył z Babilonu w pierwszym [dniu] pierwszego miesiąca, a do Jerozolimy przybył w pierwszym [dniu] piątego miesiąca, ponieważ była nad nim łaskawa ręka jego Boga.
10 Kwa maana Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza na kushika sheria ya Bwana na kuwafundisha watu wa Israeli amri na sheria zake.
Ezdrasz bowiem przygotował swoje serce, aby szukać prawa PANA i wykonywać je, a także by nauczać w Izraelu ustaw i sądów.
11 Hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alikuwa amempa Ezra aliyekuwa kuhani na mwalimu, mtu aliyeelimika katika mambo yahusuyo maagizo na amri za Bwana kwa Israeli.
A oto odpis listu, który król Artakserkses dał Ezdraszowi, kapłanowi i uczonemu, biegłemu w słowach przykazań PANA i w jego ustawach w Izraelu:
12 Artashasta, mfalme wa wafalme, Kwa Ezra kuhani, mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Salamu.
Artakserkses, król królów, Ezdraszowi, kapłanowi, uczonemu w prawie Boga niebios, [mężowi] doskonałemu, otóż;
13 Sasa naamuru kwamba mtu yeyote Mwisraeli katika ufalme wangu, pamoja na makuhani na Walawi, ambaye anataka kwenda Yerusalemu pamoja nawe aweza kwenda.
Wydaję dekret [o tym], że każdy z ludu Izraela, spośród jego kapłanów i Lewitów w moim państwie, kto dobrowolnie pragnie udać się do Jerozolimy, może iść z tobą.
14 Unatumwa na mfalme na washauri wake saba kuchunguza kuhusu Yuda na Yerusalemu kulingana na Sheria ya Mungu wako, iliyoko mkononi mwako.
Ty bowiem zostałeś wysłany przez króla i jego siedmiu doradców, abyś według prawa swego Boga, które masz w swoim ręku, zbadał sprawy w Judei i Jerozolimie;
15 Zaidi ya hayo, uchukue pamoja nawe fedha na dhahabu ambazo mfalme na washauri wake wamempa Mungu wa Israeli kwa hiari, Mungu ambaye maskani yake yako Yerusalemu,
I abyś zaniósł srebro i złoto, które król i jego doradcy dobrowolnie ofiarowali Bogu Izraela, którego przybytek [jest] w Jerozolimie;
16 pia fedha na dhahabu zote unazoweza kupata kutoka jimbo la Babeli, pamoja na sadaka za hiari watakazotoa watu na makuhani kwa ajili ya Hekalu la Mungu wao katika Yerusalemu.
Oraz całe srebro i złoto, które otrzymasz w całej prowincji Babilonu wraz z dobrowolnymi darami od ludu i kapłanów, które dobrowolnie ofiarują na dom swego Boga w Jerozolimie;
17 Hakikisha kwamba fedha hizi zimetumika kununua mafahali, kondoo dume na wana-kondoo pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, uvitoe dhabihu juu ya madhabahu ya Hekalu la Mungu wenu katika Yerusalemu.
Abyś za te pieniądze bezzwłocznie kupił cielce, barany, jagnięta wraz z przynależnymi do nich ofiarami z pokarmów i płynów i złożył je na ołtarzu domu waszego Boga w Jerozolimie;
18 Kisha wewe na Wayahudi ndugu zako mnaweza kufanya lolote linaloonekana jema sana kwa fedha na dhahabu zilizosalia, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
Z pozostałym srebrem i złotem uczyńcie zaś to, co ty i twoi bracia uznacie za słuszne, tak czyńcie, według woli waszego Boga.
19 Uvitoe kwa Mungu wa Yerusalemu vyombo vyote ulivyokabidhiwa kwa ajili ya ibada katika Hekalu la Mungu wako.
Naczynia też, które zostały ci dane do służby w domu twojego Boga, oddaj przed Bogiem w Jerozolimie;
20 Kitu kingine chochote kinachohitajika kwa ajili ya Hekalu la Mungu wenu ambacho unatakiwa kukitoa, waweza kukitoa kutoka hazina ya mfalme.
Także i inne potrzeby do domu twojego Boga, za które przyjdzie ci zapłacić, opłać ze skarbca królewskiego.
21 Mimi, Mfalme Artashasta, sasa naagiza watunza hazina wote wa Ngʼambo ya Mto Frati kutoa kwa bidii chochote kwa Ezra kuhani na mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni atakachohitaji kwenu,
A ja, król Artakserkses, wydaję wszystkim podskarbim zarzecza rozkaz o tym, że wszystko, czegokolwiek zażąda od was kapłan Ezdrasz, uczony w prawie Boga niebios, ma być bezzwłocznie wykonane;
22 talanta 100 za fedha, ngano kori 100, divai bathi 100, mafuta ya zeituni bathi 100, na chumvi kiasi chochote.
Aż do stu talentów srebra, stu kor pszenicy, stu bat wina, stu bat oliwy, a soli bez ograniczenia.
23 Chochote ambacho Mungu wa mbinguni ameagiza, kifanyike kwa ukamilifu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wa mbinguni. Kwa nini pawepo ghadhabu dhidi ya utawala wa mfalme na wanawe?
Wszystko, co nakazuje Bóg niebios, ma być wykonane starannie dla domu Boga niebios, bo dlaczego ma być wzbudzony jego gniew przeciwko państwu króla i jego synów?
24 Pia ninyi fahamuni kuwa hamna mamlaka ya kuwatoza kodi, ushuru au ada makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, watumishi wa Hekalu au wafanyakazi wengine kwenye nyumba ya Mungu.
Zawiadamiamy was również, że na żadnego z kapłanów, Lewitów, śpiewaków, odźwiernych, Netinitów oraz [pozostałych] sług tego domu Boga nie wolno nakładać podatku, danin ani cła.
25 Nawe Ezra, kufuatana na hekima ya Mungu wenu uliyo nayo, weka mahakimu na waamuzi wote wanaozifahamu sheria za Mungu wenu ili watoe haki kwa watu wote wa Ngʼambo ya Mto Frati. Nawe inakupasa umfundishe yeyote ambaye hazifahamu.
A ty, Ezdraszu, według mądrości swego Boga, która jest w tobie, ustanów urzędników i sędziów, którzy będą sądzić cały lud zarzecza, wszystkich, którzy znają prawo twego Boga; a tych, którzy go nie znają, macie uczyć.
26 Yeyote ambaye hataitii sheria ya Mungu wenu pia sheria ya mfalme, hakika lazima aadhibiwe kwa kuuawa, kuhamishwa, kunyangʼanywa mali au kufungwa gerezani.
Na każdego, kto nie wykona prawa twego Boga i prawa króla, niech bezzwłocznie będzie wydany wyrok – albo śmierci, albo wygnania, albo przepadku mienia, albo więzienia.
27 Sifa ziwe kwa Bwana, Mungu wa baba zetu, Mungu ambaye kwa njia hii ameweka ndani ya moyo wa mfalme kuipa heshima nyumba ya Bwana iliyoko Yerusalemu, kwa namna hii
[Ezdrasz powiedział]: Błogosławiony niech będzie PAN, Bóg naszych ojców, który włożył w serce króla [pragnienie], aby ozdobić dom PANA, który [jest] w Jerozolimie;
28 ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Bwana Mungu wangu ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.
A mnie okazał łaskę wobec króla i jego doradców oraz wszystkich możnych dostojników króla. A ja, będąc wzmocniony ręką PANA, swego Boga, [która była] nade mną, zgromadziłem naczelników z Izraela, aby wyruszyli ze mną.

< Ezra 7 >