< Ezra 7 >

1 Baada ya mambo haya, wakati wa utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,
Forsothe aftir these wordis Esdras, the sone of Saraie, sone of Azarie, sone of Helchie,
2 mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
sone of Sellum, sone of Sadoch, sone of Achitob,
3 mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,
sone of Amarie, sone of Azarie,
4 mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
sone of Maraioth, sone of Saraie, sone of Ozi,
5 mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Aroni.
sone of Bocci, sone of Abisue, sone of Phynees, sone of Eleazar, sone of Aaron, preest at the bigynnyng, was in the rewme of Artaxerses, king of Persis; thilke Esdras stiede fro Babiloyne,
6 Huyu Ezra alipanda kutoka Babeli. Alikuwa mwalimu mwenye ujuzi mzuri katika sheria ya Mose, ambayo Bwana, Mungu wa Israeli, alikuwa ametoa. Mfalme alikuwa amempa Ezra kila kitu alichoomba, kwa maana Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
and he was a swift writere in the lawe of Moises, which the Lord God of Israel yaf; and the kyng yaf to hym al his axyng, by the goode hoond of his Lord God on hym.
7 Pia baadhi ya Waisraeli, wakiwemo makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu na watumishi wa Hekalu, nao walikuja Yerusalemu mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
And there stieden of the sones of Israel, and of the sones of preestis, and of the sones of dekenes, and of the syngeris, and of the porteris, and of Nathyneis, `in to Jerusalem in the seuenthe yeer of Artaxerses, kyng.
8 Ezra aliwasili Yerusalemu mwezi wa tano wa mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
And thei camen in to Jerusalem in the fyuethe monethe; thilke is the seuenthe of the kyng.
9 Ezra alianza safari yake kutoka Babeli tangu siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akawasili Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa maana mkono wa neema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.
For in the firste dai of the firste monethe he bigan to stie fro Babiloyne, and in the firste dai of the fyuethe monethe he cam in to Jerusalem, bi the good hond of his God on hym. Forsothe
10 Kwa maana Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza na kushika sheria ya Bwana na kuwafundisha watu wa Israeli amri na sheria zake.
Esdras made redi his herte to enquere the lawe of the Lord, and to do, and teche in Israel the comaundement and doom.
11 Hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alikuwa amempa Ezra aliyekuwa kuhani na mwalimu, mtu aliyeelimika katika mambo yahusuyo maagizo na amri za Bwana kwa Israeli.
Sotheli this is the saumpler of the pistle of the comaundement, which the kyng Artaxerses yaf to Esdras, preest, writere lerud in the wordis and comaundementis of the Lord, and in hise cerymonyes in Israel.
12 Artashasta, mfalme wa wafalme, Kwa Ezra kuhani, mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Salamu.
Artaxerses, kyng of kyngis, desirith helthe to Esdras, the preest, moost wijs writere of the lawe of God of heuene.
13 Sasa naamuru kwamba mtu yeyote Mwisraeli katika ufalme wangu, pamoja na makuhani na Walawi, ambaye anataka kwenda Yerusalemu pamoja nawe aweza kwenda.
It is demyd of me, that whom euer it plesith in my rewme of the puple of Israel, and of hise preestis, and dekenes, to go in to Jerusalem, go he with thee.
14 Unatumwa na mfalme na washauri wake saba kuchunguza kuhusu Yuda na Yerusalemu kulingana na Sheria ya Mungu wako, iliyoko mkononi mwako.
For thou art sent fro the face of the kyng and of hise seuene counseleris, that thou visite Judee and Jerusalem in the lawe of thi God, which is in thin hond;
15 Zaidi ya hayo, uchukue pamoja nawe fedha na dhahabu ambazo mfalme na washauri wake wamempa Mungu wa Israeli kwa hiari, Mungu ambaye maskani yake yako Yerusalemu,
and that thou bere siluer and gold, which the kyng and hise counseleris han offrid bi fre wille to God of Israel, whos tabernacle is in Jerusalem.
16 pia fedha na dhahabu zote unazoweza kupata kutoka jimbo la Babeli, pamoja na sadaka za hiari watakazotoa watu na makuhani kwa ajili ya Hekalu la Mungu wao katika Yerusalemu.
And take thou freli al siluer and gold, which euer thou fyndist in al the prouynce of Babiloyne, and the puple wole offre, and of preestis that offriden bi fre wille to the hows of her God, which is in Jerusalem;
17 Hakikisha kwamba fedha hizi zimetumika kununua mafahali, kondoo dume na wana-kondoo pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, uvitoe dhabihu juu ya madhabahu ya Hekalu la Mungu wenu katika Yerusalemu.
and bie thou bisili of this monei calues, rammes, lambren, and sacrifices, and moiste sacrifices of tho; and offre thou tho on the auter of the temple of youre God, which temple is in Jerusalem.
18 Kisha wewe na Wayahudi ndugu zako mnaweza kufanya lolote linaloonekana jema sana kwa fedha na dhahabu zilizosalia, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
But also if ony thing plesith to thee, and to thi britheren, for to do of the residue siluer and gold, do ye bi the wille of youre God;
19 Uvitoe kwa Mungu wa Yerusalemu vyombo vyote ulivyokabidhiwa kwa ajili ya ibada katika Hekalu la Mungu wako.
also bitake thou in the siyt of God in Jerusalem the vessels, that ben youun in to the seruyce of the hows of thi God.
20 Kitu kingine chochote kinachohitajika kwa ajili ya Hekalu la Mungu wenu ambacho unatakiwa kukitoa, waweza kukitoa kutoka hazina ya mfalme.
But also thou schalt yyue of the tresouris of the kyng, and of the comyn arke, `ethir purse, and of me `othere thingis, that ben nedeful in the hows of thi God, as myche euere as is nedeful, that thou spende.
21 Mimi, Mfalme Artashasta, sasa naagiza watunza hazina wote wa Ngʼambo ya Mto Frati kutoa kwa bidii chochote kwa Ezra kuhani na mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni atakachohitaji kwenu,
Y Artaxerses, kyng, haue ordeyned, and demyd to alle the keperis of the comyn arke, that ben biyende the flood, that what euer thing Esdras, the preest, writere of the lawe of God of heuene, axith of you, ye yyue with out tariyng,
22 talanta 100 za fedha, ngano kori 100, divai bathi 100, mafuta ya zeituni bathi 100, na chumvi kiasi chochote.
`til to an hundrid talentis of siluer, and to an hundrid `mesuris clepid chorus of wheete, and til an hundrid mesuris clepid bathus of wyn, and `til to an hundrid `mesuris clepid bathus of oile, salt forsothe without mesure.
23 Chochote ambacho Mungu wa mbinguni ameagiza, kifanyike kwa ukamilifu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wa mbinguni. Kwa nini pawepo ghadhabu dhidi ya utawala wa mfalme na wanawe?
Al thing that perteyneth to the custom, `ethir religioun, of God of heuene, be youun diligentli in the hows of God of heuene, lest perauenture he be wrooth ayens the rewme of the kyng and of hise sones.
24 Pia ninyi fahamuni kuwa hamna mamlaka ya kuwatoza kodi, ushuru au ada makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, watumishi wa Hekalu au wafanyakazi wengine kwenye nyumba ya Mungu.
Also we make knowun to you of alle the preestis, and dekenes, syngeris, and porteris, and Nathyneis, and mynystris of the hows of this God, `that ye han not power to put on hem tol, and tribute, and costis for keperis of the lond.
25 Nawe Ezra, kufuatana na hekima ya Mungu wenu uliyo nayo, weka mahakimu na waamuzi wote wanaozifahamu sheria za Mungu wenu ili watoe haki kwa watu wote wa Ngʼambo ya Mto Frati. Nawe inakupasa umfundishe yeyote ambaye hazifahamu.
Forsothe thou, Esdras, bi the wisdom of thi God, which is in thin hond, ordeyne iugis and gouernouris, that thei deme to the puple, which is biyende the flood, that is, to hem that kunnen the lawe of thi God, and the lawe of the kyng; but also teche ye freli vnkunnynge men.
26 Yeyote ambaye hataitii sheria ya Mungu wenu pia sheria ya mfalme, hakika lazima aadhibiwe kwa kuuawa, kuhamishwa, kunyangʼanywa mali au kufungwa gerezani.
And ech man, that doth not the lawe of thi God, and the lawe of the kyng diligentli, doom schal be of hym, ethir in to the deeth, ethir in to exilyng, ethir in to condempnyng of his catel, ethir certis in to prisoun. And Esdras, the writere, seide, Blissid be the Lord God of oure fadris,
27 Sifa ziwe kwa Bwana, Mungu wa baba zetu, Mungu ambaye kwa njia hii ameweka ndani ya moyo wa mfalme kuipa heshima nyumba ya Bwana iliyoko Yerusalemu, kwa namna hii
that yaf this thing in the herte of the kyng, that he schulde glorifie the hows of the Lord,
28 ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Bwana Mungu wangu ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.
which is in Jerusalem, and bowide his mercy in to me bifor the kyng, and hise counseleris, and bifore alle the myyti princes of the kyng. And Y was coumfortid bi the hond of `my Lord God, that was in me, and Y gederide of the sones of Israel princes, that stieden with me.

< Ezra 7 >