< Ezra 7 >
1 Baada ya mambo haya, wakati wa utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,
Now after these things, when Artaxerxes was king of Persia, Ezra, the son of Seraiah, the son of Azariah, the son of Hilkiah,
2 mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
The son of Shallum, the son of Zadok, the son of Ahitub,
3 mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,
The son of Amariah, the son of Azariah, the son of Meraioth,
4 mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
The son of Zerahiah, the son of Uzzi, the son of Bukki,
5 mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Aroni.
The son of Abishua, the son of Phinehas, the son of Eleazar, the son of Aaron the chief priest:
6 Huyu Ezra alipanda kutoka Babeli. Alikuwa mwalimu mwenye ujuzi mzuri katika sheria ya Mose, ambayo Bwana, Mungu wa Israeli, alikuwa ametoa. Mfalme alikuwa amempa Ezra kila kitu alichoomba, kwa maana Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
This Ezra went up from Babylon; and he was a scribe, expert in the law of Moses which the Lord, the God of Israel, had given: and the king, moved by the Lord his God, gave him whatever he made request for.
7 Pia baadhi ya Waisraeli, wakiwemo makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu na watumishi wa Hekalu, nao walikuja Yerusalemu mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
And some of the children of Israel went up, with some of the priests and the Levites and the music-makers and the door-keepers and the Nethinim, to Jerusalem, in the seventh year of Artaxerxes the king.
8 Ezra aliwasili Yerusalemu mwezi wa tano wa mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
And he came to Jerusalem in the fifth month, in the seventh year of the king's rule.
9 Ezra alianza safari yake kutoka Babeli tangu siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akawasili Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa maana mkono wa neema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.
For, starting his journey from Babylon on the first day of the first month, he came to Jerusalem on the first day of the fifth month, by the good help of his God.
10 Kwa maana Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza na kushika sheria ya Bwana na kuwafundisha watu wa Israeli amri na sheria zake.
For Ezra had given his mind to learning the law of the Lord and doing it, and to teaching his rules and decisions in Israel.
11 Hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alikuwa amempa Ezra aliyekuwa kuhani na mwalimu, mtu aliyeelimika katika mambo yahusuyo maagizo na amri za Bwana kwa Israeli.
Now this is a copy of the letter which King Artaxerxes gave to Ezra, the priest and the scribe, who put into writing the words of the orders of the Lord, and of his rules for Israel:
12 Artashasta, mfalme wa wafalme, Kwa Ezra kuhani, mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Salamu.
Artaxerxes, king of kings, to Ezra the priest, scribe of the law of the God of heaven, all peace;
13 Sasa naamuru kwamba mtu yeyote Mwisraeli katika ufalme wangu, pamoja na makuhani na Walawi, ambaye anataka kwenda Yerusalemu pamoja nawe aweza kwenda.
And now it is my order that all those of the people of Israel, and their priests and Levites in my kingdom, who are ready and have a desire to go to Jerusalem, are to go with you.
14 Unatumwa na mfalme na washauri wake saba kuchunguza kuhusu Yuda na Yerusalemu kulingana na Sheria ya Mungu wako, iliyoko mkononi mwako.
Because you are sent by the king and his seven wise men, to get knowledge about Judah and Jerusalem, as you are ordered by the law of your God which is in your hand;
15 Zaidi ya hayo, uchukue pamoja nawe fedha na dhahabu ambazo mfalme na washauri wake wamempa Mungu wa Israeli kwa hiari, Mungu ambaye maskani yake yako Yerusalemu,
And to take with you the silver and gold freely offered by the king and his wise men to the God of Israel, whose Temple is in Jerusalem,
16 pia fedha na dhahabu zote unazoweza kupata kutoka jimbo la Babeli, pamoja na sadaka za hiari watakazotoa watu na makuhani kwa ajili ya Hekalu la Mungu wao katika Yerusalemu.
As well as all the silver and gold which you get from the land of Babylon, together with the offering of the people and of the priests, freely given for the house of their God, which is in Jerusalem:
17 Hakikisha kwamba fedha hizi zimetumika kununua mafahali, kondoo dume na wana-kondoo pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, uvitoe dhabihu juu ya madhabahu ya Hekalu la Mungu wenu katika Yerusalemu.
So with this money get with care oxen, sheep, and lambs, with their meal offerings and their drink offerings, to be offered on the altar of the house of your God, which is in Jerusalem.
18 Kisha wewe na Wayahudi ndugu zako mnaweza kufanya lolote linaloonekana jema sana kwa fedha na dhahabu zilizosalia, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
And whatever seems right to you and to your brothers to do with the rest of the silver and gold, that do, as may be pleasing to your God.
19 Uvitoe kwa Mungu wa Yerusalemu vyombo vyote ulivyokabidhiwa kwa ajili ya ibada katika Hekalu la Mungu wako.
And the vessels which have been given to you for the uses of the house of your God, you are to give to the God of Jerusalem.
20 Kitu kingine chochote kinachohitajika kwa ajili ya Hekalu la Mungu wenu ambacho unatakiwa kukitoa, waweza kukitoa kutoka hazina ya mfalme.
And whatever more is needed for the house of your God, and which you may have to give, take it from the king's store-house.
21 Mimi, Mfalme Artashasta, sasa naagiza watunza hazina wote wa Ngʼambo ya Mto Frati kutoa kwa bidii chochote kwa Ezra kuhani na mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni atakachohitaji kwenu,
And I, even I, Artaxerxes the king, now give orders to all keepers of the king's money across the river, that whatever Ezra the priest, the scribe of the law of the God of heaven, may have need of from you, is to be done with all care,
22 talanta 100 za fedha, ngano kori 100, divai bathi 100, mafuta ya zeituni bathi 100, na chumvi kiasi chochote.
Up to a hundred talents of silver, a hundred measures of grain, a hundred measures of wine, and a hundred measures of oil, and salt without measure.
23 Chochote ambacho Mungu wa mbinguni ameagiza, kifanyike kwa ukamilifu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wa mbinguni. Kwa nini pawepo ghadhabu dhidi ya utawala wa mfalme na wanawe?
Whatever is ordered by the God of heaven, let it be done completely for the house of the God of heaven; so that there may not be wrath against the kingdom of the king and his sons.
24 Pia ninyi fahamuni kuwa hamna mamlaka ya kuwatoza kodi, ushuru au ada makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, watumishi wa Hekalu au wafanyakazi wengine kwenye nyumba ya Mungu.
In addition, we make it clear to you, that it will be against the law to put any tax or payment in goods or forced payment on any of the priests or Levites, the music-makers, door-keepers, Nethinim, or any servants of this house of God.
25 Nawe Ezra, kufuatana na hekima ya Mungu wenu uliyo nayo, weka mahakimu na waamuzi wote wanaozifahamu sheria za Mungu wenu ili watoe haki kwa watu wote wa Ngʼambo ya Mto Frati. Nawe inakupasa umfundishe yeyote ambaye hazifahamu.
And you, Ezra, by the wisdom of your God which is in you, are to put rulers and judges to have authority over all the people across the river who have knowledge of the laws of your God; and you are to give teaching to him who has no knowledge of them.
26 Yeyote ambaye hataitii sheria ya Mungu wenu pia sheria ya mfalme, hakika lazima aadhibiwe kwa kuuawa, kuhamishwa, kunyangʼanywa mali au kufungwa gerezani.
And if anyone does not keep the law of your God and the law of the king, take care that punishment is given to him, by death or by driving him from his country or by taking away his goods or by putting him in prison.
27 Sifa ziwe kwa Bwana, Mungu wa baba zetu, Mungu ambaye kwa njia hii ameweka ndani ya moyo wa mfalme kuipa heshima nyumba ya Bwana iliyoko Yerusalemu, kwa namna hii
Praise be to the Lord, the God of our fathers, who has put such a thing into the heart of the king, to make fair the house of the Lord which is in Jerusalem;
28 ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Bwana Mungu wangu ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.
And has given mercy to me before the king and his government and before all the king's great captains. And I was made strong by the hand of the Lord my God which was on me, and I got together out of Israel chief men to go up with me.