< Ezra 6 >

1 Kisha Mfalme Dario alitoa amri, nao wakafanya uchunguzi katika kumbukumbu zilizohifadhiwa katika hazina huko Babeli.
Alors, le roi Darius fit un édit pour que l'on cherchât dans les bibliothèques où est le trésor de Babylone.
2 Karatasi moja ndefu ya maandishi ilipatikana huko Ekbatana katika jimbo la Umedi. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa humo: Kumbukumbu:
Et l'on trouva en cette ville, dans le palais, un chapitre où ce mémorial était écrit.
3 Katika mwaka wa kwanza wa kutawala Mfalme Koreshi, mfalme alitoa amri kuhusu Hekalu la Mungu katika Yerusalemu: Hekalu na lijengwe tena mahali palepale Wayahudi walipokuwa wakitoa dhabihu, kwenye msingi ule ule. Iwe na kimo cha mikono sitini, upana wa mikono sitini,
En la première année de la domination du roi Cyrus, le roi Cyrus a fait cet édit, touchant le saint temple de Dieu à Jérusalem: Que le temple soit rebâti, ainsi que le lieu où l'on sacrifiait des victimes. Et il en a déterminé la hauteur et la largeur: soixante coudées des deux parts.
4 kuta zijengwe kwa safu tatu za mawe makubwa kisha ifuate safu moja ya mbao. Gharama zitalipwa kutoka hazina ya mfalme.
Et il a ajouté: Qu'il y ait trois étages en pierres dures et un en bois, et que la dépense soit supportée par le trésor royal.
5 Pia, vyombo vya dhahabu na vya fedha vya nyumba ya Mungu, ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka kwenye Hekalu huko Yerusalemu akavileta Babeli, yapasa virudishwe mahali pake ndani ya Hekalu huko Yerusalemu, yapasa viwekwe ndani ya nyumba ya Mungu.
Que l'on rende les vases d'or et d'argent du temple de Dieu, apportés de Jérusalem par Nabuchodonosor, et mis à Babylone; qu'ils retournent au temple de Jérusalem, à la place où ils étaient, dans le temple de Dieu.
6 Sasa basi, Tatenai, mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai pamoja na ninyi, maafisa wenzao wa jimbo hilo kaeni mbali na mahali hapo.
Maintenant, vous, gouverneurs au delà du fleuve, vous, Satharbuzanaï et Apharsachéens, mes serviteurs au delà du fleuve, donnez-leur ces choses, et tenez-vous loin d'eux.
7 Msiingilie kazi ya Hekalu hili la Mungu. Mwacheni mtawala wa Wayahudi na viongozi Wayahudi wajenge upya nyumba hii ya Mungu mahali pake.
Laissez faire les travaux du temple de Dieu: que les chefs des Juifs, que leurs anciens bâtissent le temple au lieu où il était.
8 Zaidi ya hayo, hapa natoa amri kuhusu mtakalofanya kwa ajili ya wazee wa Wayahudi katika ujenzi wa nyumba hii ya Mungu: Gharama za watu hawa zitalipwa kikamilifu kutoka hazina ya mfalme, kutoka kwenye mapato ya Ngʼambo ya Mto Frati, ili ujenzi usisimame.
Un édit est aussi rendu par moi pour que vous ne vous mêliez en rien de ce que feront les anciens des Juifs, pendant qu'ils bâtiront le temple de ce Dieu, et que, dans le but de ne point arrêter les travaux, on donne avec zèle à ces hommes, sur les impôts du roi, levés au delà de l'Euphrate, ce qu'il faudra pour la dépense.
9 Chochote kinachohitajika kama mafahali wachanga, kondoo dume, wana-kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano, chumvi, divai na mafuta kama vitakavyohitajika na makuhani huko Yerusalemu, lazima wapewe kila siku pasipo kukosa,
Et, ce qui viendrait à leur manquer, qu'on le leur donne jour par jour, à mesure qu'ils le demanderont, soit des bœufs, des béliers, des agneaux, pour les holocaustes du Dieu du ciel, soit du froment, du sel, du vin et de l'huile, selon le besoin des prêtres qui se trouvent à Jérusalem,
10 ili waweze kutoa dhabihu inayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe hali njema.
Afin qu'ils fassent aisément leurs offrandes d'odeur de suavité au Dieu du ciel, et qu'ils prient pour la vie du roi et de ses fils.
11 Zaidi ya hayo, ninaamuru kwamba mtu yeyote atakayebadilisha amri hii, boriti itangʼolewa kutoka nyumba yake, ichongwe upande mmoja na atumbuliwe nayo. Kwa ajili ya kosa hili nyumba yake ifanywe lundo la taka.
Et j'ai fait un édit portant que quiconque s'écartera de mes ordres sera attaché à une poutre enlevée de sa maison, et mis à mort sur ce bois, et que sa maison sera confisquée.
12 Naye Mungu, aliyeliweka Jina lake huko, amwangushe mfalme yeyote au watu watakaoinua mikono kubadili amri hii au kuharibu Hekalu hili lililoko Yerusalemu. Mimi Dario nimetoa amri hii. Nayo itekelezwe kwa bidii na kwa makini.
Puisse le Dieu, dont le nom résidera en ce temple, renverser tout roi ou peuple qui étendra la main pour endommager ou détruire le temple de Dieu à Jérusalem. Moi, Darius, j'ai fait cet édit; qu'on soit attentif à s'y conformer.
13 Kwa sababu ya amri aliyotoa Mfalme Dario, Tatenai mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao wakaitekeleza kwa bidii na kwa makini.
Alors, Tanthanaï, gouverneur en deçà de l'Euphrate; Satharbuzanaï, et les autres serviteurs du roi à qui Darius avait écrit, lui obéirent avec zèle.
14 Hivyo wazee wa Wayahudi waliendelea kujenga na kustawi kutokana na mahubiri ya manabii Hagai na Zekaria, mwana wa Ido. Wakakamilisha ujenzi wa Hekalu kulingana na agizo la Mungu wa Israeli na amri ya Koreshi, Dario na Artashasta wafalme wa Uajemi.
Et les anciens des Juifs et les lévites bâtirent, selon la prophétie d'Aggée le prophète, et de Zacharie, fils d'Addo; et ils bâtirent, et ils achevèrent le temple suivant la volonté de Dieu, et grâce aux édits de Cyrus, de Darius et d'Arthasastha, rois des Perses.
15 Hekalu lilikamilika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa Adari, ndio mwezi wa tatu, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.
Et ils achevèrent le temple le troisième jour du mois d'adar, et la sixième année du règne de Darius.
16 Kisha watu wa Israeli: makuhani, Walawi na wengine wote waliohamishwa, wakaadhimisha kule kuwekwa wakfu nyumba ya Mungu kwa shangwe.
Et les fils d'Israël, et les prêtres, et les lévites, et le reste des fils de l'exil, firent, avec allégresse, la dédicace du temple de Dieu.
17 Kwa ajili ya kuwekwa wakfu nyumba hii ya Mungu walitoa mafahali mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, sadaka kwa ajili ya dhambi ya Israeli yote walitoa mbuzi dume kumi na wawili, mmoja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.
Pour la dédicace du temple de Dieu, ils offrirent cent bœufs, deux cents béliers, quatre cents agneaux; et l'offrande pour les péchés de tout Israël fut de douze boucs, nombre égal à celui des tribus d'Israël.
18 Wakawaweka makuhani katika nafasi zao na Walawi wakawekwa katika makundi yao ya huduma kwa Mungu huko Yerusalemu, kulingana na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose.
Ils rétablirent les prêtres selon leurs divisions, et les lévites selon leurs catégories, pour le service de Dieu à Jérusalem, comme il est écrit au livre de Moïse.
19 Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, waliorudi kutoka uhamishoni wakaadhimisha Pasaka.
Et les fils de l'exil firent la Pâque le quatorzième jour du second mois.
20 Makuhani na Walawi walikuwa wamekwisha kujitakasa nao wamekuwa safi kwa kufuata kawaida za ibada. Walawi wakachinja kondoo wa Pasaka kwa ajili ya wana wa waliorudi kutoka utumwani uhamishoni, kwa ajili ya ndugu zao makuhani na wao wenyewe.
Car les prêtres et les lévites s'étaient purifiés; ils avaient tous été reconnus purs. Et ils immolèrent la pâque pour tous les fils de l'exil, et pour leurs frères les prêtres et les lévites.
21 Hivyo Waisraeli waliokuwa wamerudi kutoka utumwani uhamishoni wakaila Pasaka, pamoja na wale waliokuwa wamejitenga na matendo ya unajisi wa Mataifa ya jirani ili kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli.
Et les fils d'Israël mangèrent la pâque, tant ceux qui étaient revenus de l'exil que ceux qui s'étaient préservés de l'impureté des peuples de la contrée, leurs voisins, et qui avaient cherché le Seigneur Dieu d'Israël.
22 Kwa muda wa siku saba waliiadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa furaha, kwa sababu Bwana alikuwa amewajaza furaha kwa kubadilisha nia ya mfalme wa Ashuru kwamba awasaidie ujenzi wa nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.
Et ils célébrèrent la fête des Azymes durant sept jours avec allégresse; car le Seigneur les réjouit, et il avait incliné le cœur du roi d'Assyrie en leur faveur pour fortifier leurs mains dans les travaux du temple du Dieu d'Israël.

< Ezra 6 >