< Ezra 6 >
1 Kisha Mfalme Dario alitoa amri, nao wakafanya uchunguzi katika kumbukumbu zilizohifadhiwa katika hazina huko Babeli.
Alors le roi Darius donna un ordre, et l'on fouilla la maison des archives, où les trésors étaient déposés à Babylone.
2 Karatasi moja ndefu ya maandishi ilipatikana huko Ekbatana katika jimbo la Umedi. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa humo: Kumbukumbu:
On trouva un rouleau à Achmetha, dans le palais qui est dans la province de Médie, et voici ce qui y était écrit pour mémoire:
3 Katika mwaka wa kwanza wa kutawala Mfalme Koreshi, mfalme alitoa amri kuhusu Hekalu la Mungu katika Yerusalemu: Hekalu na lijengwe tena mahali palepale Wayahudi walipokuwa wakitoa dhabihu, kwenye msingi ule ule. Iwe na kimo cha mikono sitini, upana wa mikono sitini,
La première année du roi Cyrus, le roi Cyrus donna un ordre: En ce qui concerne la maison de Dieu à Jérusalem, que la maison soit construite, le lieu où l'on offre des sacrifices, et que ses fondations soient solidement posées, avec sa hauteur de soixante coudées et sa largeur de soixante coudées;
4 kuta zijengwe kwa safu tatu za mawe makubwa kisha ifuate safu moja ya mbao. Gharama zitalipwa kutoka hazina ya mfalme.
avec trois rangées de grandes pierres et une rangée de bois neuf. Les dépenses seront payées sur la maison du roi.
5 Pia, vyombo vya dhahabu na vya fedha vya nyumba ya Mungu, ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka kwenye Hekalu huko Yerusalemu akavileta Babeli, yapasa virudishwe mahali pake ndani ya Hekalu huko Yerusalemu, yapasa viwekwe ndani ya nyumba ya Mungu.
Que les objets d'or et d'argent de la maison de Dieu, que Nabuchodonosor a enlevés du temple de Jérusalem et transportés à Babylone, soient restaurés et ramenés dans le temple de Jérusalem, à leur place. Tu les mettras dans la maison de Dieu.
6 Sasa basi, Tatenai, mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai pamoja na ninyi, maafisa wenzao wa jimbo hilo kaeni mbali na mahali hapo.
Maintenant, Tattenaï, gouverneur de l'autre côté du fleuve, Shetharbozenaï, et tes compagnons, les Apharsacites, qui sont de l'autre côté du fleuve, vous devez rester loin de là.
7 Msiingilie kazi ya Hekalu hili la Mungu. Mwacheni mtawala wa Wayahudi na viongozi Wayahudi wajenge upya nyumba hii ya Mungu mahali pake.
Laissez l'ouvrage de cette maison de Dieu; laissez le gouverneur des Juifs et les anciens des Juifs construire cette maison de Dieu à sa place.
8 Zaidi ya hayo, hapa natoa amri kuhusu mtakalofanya kwa ajili ya wazee wa Wayahudi katika ujenzi wa nyumba hii ya Mungu: Gharama za watu hawa zitalipwa kikamilifu kutoka hazina ya mfalme, kutoka kwenye mapato ya Ngʼambo ya Mto Frati, ili ujenzi usisimame.
J'établis un décret sur ce que vous devez faire pour ces anciens des Juifs, pour la construction de cette maison de Dieu: sur les biens du roi, sur le tribut de l'autre côté du fleuve, des dépenses doivent être faites en toute diligence pour ces hommes, afin qu'ils ne soient pas gênés.
9 Chochote kinachohitajika kama mafahali wachanga, kondoo dume, wana-kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano, chumvi, divai na mafuta kama vitakavyohitajika na makuhani huko Yerusalemu, lazima wapewe kila siku pasipo kukosa,
Ce dont ils ont besoin, jeunes taureaux, béliers et agneaux, pour les holocaustes au Dieu des cieux, ainsi que du blé, du sel, du vin et de l'huile, selon la parole des prêtres qui sont à Jérusalem, on le leur donnera chaque jour sans faute,
10 ili waweze kutoa dhabihu inayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe hali njema.
afin qu'ils puissent offrir des sacrifices d'une agréable odeur au Dieu des cieux, et prier pour la vie du roi et de ses fils.
11 Zaidi ya hayo, ninaamuru kwamba mtu yeyote atakayebadilisha amri hii, boriti itangʼolewa kutoka nyumba yake, ichongwe upande mmoja na atumbuliwe nayo. Kwa ajili ya kosa hili nyumba yake ifanywe lundo la taka.
J'ai aussi décrété que celui qui altérera ce message, qu'on arrache une poutre de sa maison, qu'on le soulève et qu'on l'attache dessus, et que sa maison devienne un tas de fumier à cause de cela.
12 Naye Mungu, aliyeliweka Jina lake huko, amwangushe mfalme yeyote au watu watakaoinua mikono kubadili amri hii au kuharibu Hekalu hili lililoko Yerusalemu. Mimi Dario nimetoa amri hii. Nayo itekelezwe kwa bidii na kwa makini.
Que le Dieu qui y a fait résider son nom renverse tous les rois et les peuples qui tendent la main pour altérer ceci, pour détruire cette maison de Dieu qui est à Jérusalem. Moi, Darius, j'ai pris un décret. Que cela soit fait avec toute la diligence voulue.
13 Kwa sababu ya amri aliyotoa Mfalme Dario, Tatenai mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao wakaitekeleza kwa bidii na kwa makini.
Alors Tattenai, gouverneur de l'autre côté du fleuve, Shetharbozenai et leurs compagnons firent tout cela avec diligence, car le roi Darius avait envoyé un décret.
14 Hivyo wazee wa Wayahudi waliendelea kujenga na kustawi kutokana na mahubiri ya manabii Hagai na Zekaria, mwana wa Ido. Wakakamilisha ujenzi wa Hekalu kulingana na agizo la Mungu wa Israeli na amri ya Koreshi, Dario na Artashasta wafalme wa Uajemi.
Les anciens des Juifs bâtirent et prospérèrent, grâce à la prophétie d'Aggée, le prophète, et de Zacharie, fils d'Iddo. Ils la bâtirent et l'achevèrent, selon le commandement du Dieu d'Israël et selon le décret de Cyrus, de Darius et d'Artaxerxès, roi de Perse.
15 Hekalu lilikamilika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa Adari, ndio mwezi wa tatu, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.
Cette maison fut achevée le troisième jour du mois d'Adar, la sixième année du règne du roi Darius.
16 Kisha watu wa Israeli: makuhani, Walawi na wengine wote waliohamishwa, wakaadhimisha kule kuwekwa wakfu nyumba ya Mungu kwa shangwe.
Les enfants d'Israël, les sacrificateurs, les Lévites et le reste des enfants de la captivité, célébrèrent avec joie la dédicace de cette maison de Dieu.
17 Kwa ajili ya kuwekwa wakfu nyumba hii ya Mungu walitoa mafahali mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, sadaka kwa ajili ya dhambi ya Israeli yote walitoa mbuzi dume kumi na wawili, mmoja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.
Ils offrirent à la dédicace de cette maison de Dieu cent taureaux, deux cents béliers, quatre cents agneaux, et en sacrifice pour le péché pour tout Israël, douze boucs, selon le nombre des tribus d'Israël.
18 Wakawaweka makuhani katika nafasi zao na Walawi wakawekwa katika makundi yao ya huduma kwa Mungu huko Yerusalemu, kulingana na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose.
Ils établirent les sacrificateurs selon leurs divisions et les Lévites selon leurs classes, pour le service de Dieu qui est à Jérusalem, comme il est écrit dans le livre de Moïse.
19 Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, waliorudi kutoka uhamishoni wakaadhimisha Pasaka.
Les enfants de la captivité célébrèrent la Pâque le quatorzième jour du premier mois.
20 Makuhani na Walawi walikuwa wamekwisha kujitakasa nao wamekuwa safi kwa kufuata kawaida za ibada. Walawi wakachinja kondoo wa Pasaka kwa ajili ya wana wa waliorudi kutoka utumwani uhamishoni, kwa ajili ya ndugu zao makuhani na wao wenyewe.
Comme les prêtres et les lévites s'étaient purifiés ensemble, ils étaient tous purs. Ils immolèrent la Pâque pour tous les enfants de la captivité, pour leurs frères les prêtres et pour eux-mêmes.
21 Hivyo Waisraeli waliokuwa wamerudi kutoka utumwani uhamishoni wakaila Pasaka, pamoja na wale waliokuwa wamejitenga na matendo ya unajisi wa Mataifa ya jirani ili kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli.
Les enfants d'Israël revenus de la captivité et tous ceux qui s'étaient séparés de la souillure des nations du pays pour chercher Yahvé, le Dieu d'Israël, mangèrent,
22 Kwa muda wa siku saba waliiadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa furaha, kwa sababu Bwana alikuwa amewajaza furaha kwa kubadilisha nia ya mfalme wa Ashuru kwamba awasaidie ujenzi wa nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.
et célébrèrent avec joie la fête des pains sans levain pendant sept jours, car Yahvé les avait rendus joyeux et avait tourné vers eux le cœur du roi d'Assyrie, pour fortifier leurs mains dans l'œuvre de Dieu, la maison d'Israël.