< Ezra 6 >

1 Kisha Mfalme Dario alitoa amri, nao wakafanya uchunguzi katika kumbukumbu zilizohifadhiwa katika hazina huko Babeli.
Tedy král Darius rozkázal, aby hledali v bibliotéce, mezi poklady složenými v Babyloně.
2 Karatasi moja ndefu ya maandishi ilipatikana huko Ekbatana katika jimbo la Umedi. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa humo: Kumbukumbu:
I nalezena jest v Achmeta na hradě, kterýž jest v Médské krajině, jedna kniha, a takto zapsána byla v ní pamět:
3 Katika mwaka wa kwanza wa kutawala Mfalme Koreshi, mfalme alitoa amri kuhusu Hekalu la Mungu katika Yerusalemu: Hekalu na lijengwe tena mahali palepale Wayahudi walipokuwa wakitoa dhabihu, kwenye msingi ule ule. Iwe na kimo cha mikono sitini, upana wa mikono sitini,
Léta prvního Cýra krále Cýrus král rozkázal: Dům Boží, kterýž byl v Jeruzalémě, ať jest v městě staven na místě, kdež se obětují oběti, a grunty jeho ať vzhůru ženou, zvýší loktů šedesáti, a zšíří loktů šedesáti,
4 kuta zijengwe kwa safu tatu za mawe makubwa kisha ifuate safu moja ya mbao. Gharama zitalipwa kutoka hazina ya mfalme.
Třmi řady z kamení velikého, a řad z dříví nového, náklad pak z domu královského bude dáván.
5 Pia, vyombo vya dhahabu na vya fedha vya nyumba ya Mungu, ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka kwenye Hekalu huko Yerusalemu akavileta Babeli, yapasa virudishwe mahali pake ndani ya Hekalu huko Yerusalemu, yapasa viwekwe ndani ya nyumba ya Mungu.
Nadto nádobí domu Božího zlaté i stříbrné, kteréž Nabuchodonozor byl pobral z chrámu, jenž byl v Jeruzalémě, a byl je přenesl do Babylona, ať zase navrátí, aby se dostalo do chrámu Jeruzalémského na místo své, a složeno bylo v domě Božím.
6 Sasa basi, Tatenai, mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai pamoja na ninyi, maafisa wenzao wa jimbo hilo kaeni mbali na mahali hapo.
Protož nyní, ty Tattenai, vývodo za řekou, Setarbozenai s tovaryši svými, i Afarsechaiští, kteříž jste za řekou, ustupte odtud.
7 Msiingilie kazi ya Hekalu hili la Mungu. Mwacheni mtawala wa Wayahudi na viongozi Wayahudi wajenge upya nyumba hii ya Mungu mahali pake.
Nechte jich při díle toho domu Božího. Vůdce Židovský a starší jejich nechať ten dům Boží stavějí na místě jeho.
8 Zaidi ya hayo, hapa natoa amri kuhusu mtakalofanya kwa ajili ya wazee wa Wayahudi katika ujenzi wa nyumba hii ya Mungu: Gharama za watu hawa zitalipwa kikamilifu kutoka hazina ya mfalme, kutoka kwenye mapato ya Ngʼambo ya Mto Frati, ili ujenzi usisimame.
Ode mne také poručeno jest o tom, co byste měli činiti s staršími Židovskými při stavení toho domu Božího, totiž, aby z zboží královského, z důchodů, jenž jsou za řekou, bez meškání náklad dáván byl mužům těm, aby dílo nemělo překážky.
9 Chochote kinachohitajika kama mafahali wachanga, kondoo dume, wana-kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano, chumvi, divai na mafuta kama vitakavyohitajika na makuhani huko Yerusalemu, lazima wapewe kila siku pasipo kukosa,
A to, čehož by bylo potřebí, buď volků aneb skopců i beránků k zápalným obětem Boha nebeského, obilé, soli, vína i oleje, jakž by rozkázali kněží Jeruzalémští, nechť se jim dává na každý den, a to beze všeho podvodu,
10 ili waweze kutoa dhabihu inayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe hali njema.
Aby měli z čeho obětovati vůni příjemnou Bohu nebeskému, a aby se modlili za život krále i za syny jeho.
11 Zaidi ya hayo, ninaamuru kwamba mtu yeyote atakayebadilisha amri hii, boriti itangʼolewa kutoka nyumba yake, ichongwe upande mmoja na atumbuliwe nayo. Kwa ajili ya kosa hili nyumba yake ifanywe lundo la taka.
Nadto ode mne jest rozkázáno: Kdož by koli zrušil přikázaní toto, aby vybořeno bylo z domu jeho dřevo, a zdviženo bylo, na němž by oběšen byl, a dům jeho ať jest hnojištěm pro takovou věc.
12 Naye Mungu, aliyeliweka Jina lake huko, amwangushe mfalme yeyote au watu watakaoinua mikono kubadili amri hii au kuharibu Hekalu hili lililoko Yerusalemu. Mimi Dario nimetoa amri hii. Nayo itekelezwe kwa bidii na kwa makini.
Bůh pak, jehož jméno tam přebývá, zkaziž všelikého krále i lid, kterýž by vztáhl ruku svou k změnění toho, a zkáze toho domu Božího, jenž jest v Jeruzalémě. Já Darius přikazuji sám, bez meškání ať se stane.
13 Kwa sababu ya amri aliyotoa Mfalme Dario, Tatenai mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao wakaitekeleza kwa bidii na kwa makini.
Tedy Tattenai, vývoda za řekou, a Setarbozenai s tovaryši svými vedlé toho, jakž rozkázal Darius král, tak učinili bez meškání.
14 Hivyo wazee wa Wayahudi waliendelea kujenga na kustawi kutokana na mahubiri ya manabii Hagai na Zekaria, mwana wa Ido. Wakakamilisha ujenzi wa Hekalu kulingana na agizo la Mungu wa Israeli na amri ya Koreshi, Dario na Artashasta wafalme wa Uajemi.
I stavěli starší Židovští, a šťastně se jim vedlo vedlé proroctví Aggea proroka, a Zachariáše syna Iddova. Stavěli tedy a dokonali z rozkázaní Boha Izraelského, a z rozkázaní Cýra a Daria, a Artaxerxa krále Perského.
15 Hekalu lilikamilika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa Adari, ndio mwezi wa tatu, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.
A dokonán jest ten dům k třetímu dni měsíce Adar, a ten byl rok šestý kralování Daria krále.
16 Kisha watu wa Israeli: makuhani, Walawi na wengine wote waliohamishwa, wakaadhimisha kule kuwekwa wakfu nyumba ya Mungu kwa shangwe.
Tedy synové Izraelští, kněží a Levítové, i jiní, kteříž byli přišli z převedení, posvětili toho domu Božího s radostí.
17 Kwa ajili ya kuwekwa wakfu nyumba hii ya Mungu walitoa mafahali mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, sadaka kwa ajili ya dhambi ya Israeli yote walitoa mbuzi dume kumi na wawili, mmoja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.
A obětovali při posvěcení toho Božího domu sto telat, skopců dvě stě, beránků čtyři sta, a kozlů k oběti za hřích za všecken Izrael dvanáct, vedlé počtu pokolení Izraelského.
18 Wakawaweka makuhani katika nafasi zao na Walawi wakawekwa katika makundi yao ya huduma kwa Mungu huko Yerusalemu, kulingana na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose.
I postavili kněží v třídách jejich, a Levíty v pořádcích jejich při službě Boží v Jeruzalémě, jakož psáno jest v knize Mojžíšově.
19 Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, waliorudi kutoka uhamishoni wakaadhimisha Pasaka.
Slavili také ti, kteříž se vrátili z přestěhování, velikunoc čtrnáctého dne měsíce prvního.
20 Makuhani na Walawi walikuwa wamekwisha kujitakasa nao wamekuwa safi kwa kufuata kawaida za ibada. Walawi wakachinja kondoo wa Pasaka kwa ajili ya wana wa waliorudi kutoka utumwani uhamishoni, kwa ajili ya ndugu zao makuhani na wao wenyewe.
Nebo očistili se byli kněží a Levítové jednomyslně. Všickni čistí byli, a obětovali beránka velikonočního za všecky, jenž zajati byli, i za bratří své kněží, i sami za sebe.
21 Hivyo Waisraeli waliokuwa wamerudi kutoka utumwani uhamishoni wakaila Pasaka, pamoja na wale waliokuwa wamejitenga na matendo ya unajisi wa Mataifa ya jirani ili kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli.
A jedli synové Izraelští, kteříž se byli navrátili z přestěhování, i každý, kdož odděliv se od poškvrnění pohanů země, připojil se k nim, aby hledal Hospodina Boha Izraelského.
22 Kwa muda wa siku saba waliiadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa furaha, kwa sababu Bwana alikuwa amewajaza furaha kwa kubadilisha nia ya mfalme wa Ashuru kwamba awasaidie ujenzi wa nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.
Drželi také slavnost přesnic za sedm dní s veselím, proto že je rozveselil Hospodin, a obrátil srdce krále Assyrského k nim, aby jich posilnil v díle domu Božího, Boha Izraelského.

< Ezra 6 >