< Ezra 6 >

1 Kisha Mfalme Dario alitoa amri, nao wakafanya uchunguzi katika kumbukumbu zilizohifadhiwa katika hazina huko Babeli.
Hahoi siangpahrang Darius ni kâ a poe teh Babilon râw kuemnae koe, cauk tânae dawk a tawng awh.
2 Karatasi moja ndefu ya maandishi ilipatikana huko Ekbatana katika jimbo la Umedi. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa humo: Kumbukumbu:
Hat toteh, Medes ram Akhametha kho e siangpahrang im vah cakalawng e a hmu awh. Hawvah kahawicalah tâ hanelah hettelah thut lah ao.
3 Katika mwaka wa kwanza wa kutawala Mfalme Koreshi, mfalme alitoa amri kuhusu Hekalu la Mungu katika Yerusalemu: Hekalu na lijengwe tena mahali palepale Wayahudi walipokuwa wakitoa dhabihu, kwenye msingi ule ule. Iwe na kimo cha mikono sitini, upana wa mikono sitini,
Jerusalem e Cathut e im teh siangpahrang Sairus ni a bawinae kum nah hettelah kâ a poe, thuengnae khoungroe im teh bout sak e lah awm seh, adu hai kacaklah ung naseh.
4 kuta zijengwe kwa safu tatu za mawe makubwa kisha ifuate safu moja ya mbao. Gharama zitalipwa kutoka hazina ya mfalme.
A rasang e dong 60, akaw e dong 60, talung kalenpounge coung thum touh lah pacoung hnukkhu, a katha e thing hoi boutbout pacoung sin naseh. Aphunaw hateh siangpahrang e hnopai hoi poe lah ao han.
5 Pia, vyombo vya dhahabu na vya fedha vya nyumba ya Mungu, ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka kwenye Hekalu huko Yerusalemu akavileta Babeli, yapasa virudishwe mahali pake ndani ya Hekalu huko Yerusalemu, yapasa viwekwe ndani ya nyumba ya Mungu.
Hahoi Cathut e im dawk e sui, ngun hoi hnopai Nebukhadnezar ni Jerusalem lah a ceikhai teh Babilon vah a kâenkhai e naw hah bout poe naseh, Jerusalem e bawkim amae hmuen koevah ceikhai vaiteh Cathut e im dawk bout hrueng naseh.
6 Sasa basi, Tatenai, mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai pamoja na ninyi, maafisa wenzao wa jimbo hilo kaeni mbali na mahali hapo.
Hatdawkvah, tui namran kaukkung Tattenai hoi Setharbozenai hoi tui namran lah kaawm e a hui Afasat taminaw hah hnai awh hanh.
7 Msiingilie kazi ya Hekalu hili la Mungu. Mwacheni mtawala wa Wayahudi na viongozi Wayahudi wajenge upya nyumba hii ya Mungu mahali pake.
Hete BAWIPA e bawkim sak e dawk runae poe awh hanh. Judah kahrawikungnaw hoi Judah kacuenaw ni Cathut e im teh amae hmuen koe bout sak naseh.
8 Zaidi ya hayo, hapa natoa amri kuhusu mtakalofanya kwa ajili ya wazee wa Wayahudi katika ujenzi wa nyumba hii ya Mungu: Gharama za watu hawa zitalipwa kikamilifu kutoka hazina ya mfalme, kutoka kwenye mapato ya Ngʼambo ya Mto Frati, ili ujenzi usisimame.
Hahoi sak e kabawp hanelah kâ na poe awh, thaw a hmacawn nahanelah, tui namran kanîloumlae tamuk teh, siangpahrang e hnopai thung hoi poe lah ao han.
9 Chochote kinachohitajika kama mafahali wachanga, kondoo dume, wana-kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano, chumvi, divai na mafuta kama vitakavyohitajika na makuhani huko Yerusalemu, lazima wapewe kila siku pasipo kukosa,
Panki e patetlah kalvan Cathut koe hmaisawi thueng nahanelah maitoca thoseh, tutan thoseh, tuca thoseh, cakang, misur, satui hai thoseh, Jerusalem kaawm e vaihmanaw ni a dei e patetlah hnintangkuem hnan laipalah, poe awh naseh.
10 ili waweze kutoa dhabihu inayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe hali njema.
Hat toteh, kalvan Cathut koe hmuitui thuengnae pout laipalah siangpahrang hoi a ca hringsaw thai nahanlah a ratoum thai awh han.
11 Zaidi ya hayo, ninaamuru kwamba mtu yeyote atakayebadilisha amri hii, boriti itangʼolewa kutoka nyumba yake, ichongwe upande mmoja na atumbuliwe nayo. Kwa ajili ya kosa hili nyumba yake ifanywe lundo la taka.
Hete lawk ka ek e tami teh, a im khom phawk pouh vaiteh bout ung e dawk ama hai bang vaiteh, a im teh vaipuen lah tho sak han telah, kâ ka poe.
12 Naye Mungu, aliyeliweka Jina lake huko, amwangushe mfalme yeyote au watu watakaoinua mikono kubadili amri hii au kuharibu Hekalu hili lililoko Yerusalemu. Mimi Dario nimetoa amri hii. Nayo itekelezwe kwa bidii na kwa makini.
Hahoi, hawvah a min kaawm sak e BAWIPA ni Jerusalem e Cathut im raphoe hanelah a kâcai. teh, kut ka dâw e siangpahrang hoi a ram pueng teh raphoe pouh e lah awm naseh telah, kai Darius ni kâ poe e patetlah roup tarawi naseh.
13 Kwa sababu ya amri aliyotoa Mfalme Dario, Tatenai mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao wakaitekeleza kwa bidii na kwa makini.
Hahoi teh, tui namran lah kaukkung Tattenai hoi Setharbozenai hoi a huinaw ni Darius e ca a hmu awh e patetlah a sak awh,
14 Hivyo wazee wa Wayahudi waliendelea kujenga na kustawi kutokana na mahubiri ya manabii Hagai na Zekaria, mwana wa Ido. Wakakamilisha ujenzi wa Hekalu kulingana na agizo la Mungu wa Israeli na amri ya Koreshi, Dario na Artashasta wafalme wa Uajemi.
Hahoi profet Haggai hoi Iddo capa Zekhariah ni a dei roi e lawk kecu dawk Judah kahrawikungnaw ni kahawicalah a sak awh. Isarel Cathut e kâpoelawk patetlah Persia siangpahrang Sairus hoi Darius hoi Artaxerxes tinaw ni kâ poe e patetlah a sak awh teh a cum awh.
15 Hekalu lilikamilika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa Adari, ndio mwezi wa tatu, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.
Hote im teh siangpahrang Darius a bawi kum 6nae, Adar thapa hni 3 nah a cum awh.
16 Kisha watu wa Israeli: makuhani, Walawi na wengine wote waliohamishwa, wakaadhimisha kule kuwekwa wakfu nyumba ya Mungu kwa shangwe.
Isarel catoun, vaihmanaw hoi Levih miphun, san dawk hoi ka tâcawt e ni Cathut e im teh pout laipalah lunghawicalah a sak awh.
17 Kwa ajili ya kuwekwa wakfu nyumba hii ya Mungu walitoa mafahali mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, sadaka kwa ajili ya dhambi ya Israeli yote walitoa mbuzi dume kumi na wawili, mmoja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.
Hete im saknae dawkvah maitotan 200, tuca 400 touh a poe awh. Hahoi Isarelnaw hanelah yon thuengnae dawk Isarel miphun yit touh hoiyah hmae 12 touh.
18 Wakawaweka makuhani katika nafasi zao na Walawi wakawekwa katika makundi yao ya huduma kwa Mungu huko Yerusalemu, kulingana na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose.
Mosi e cauk dawk thut e patetlah Jerusalem e Cathut im thaw tawk hanelah vaihmanaw hoi Levihnaw hah ahuhu lahoi ao sak awh.
19 Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, waliorudi kutoka uhamishoni wakaadhimisha Pasaka.
Hahoi, san dawk hoi kahloutnaw ni thapa pasuek, hnin 14 nah ceitakhai pawi a sak awh.
20 Makuhani na Walawi walikuwa wamekwisha kujitakasa nao wamekuwa safi kwa kufuata kawaida za ibada. Walawi wakachinja kondoo wa Pasaka kwa ajili ya wana wa waliorudi kutoka utumwani uhamishoni, kwa ajili ya ndugu zao makuhani na wao wenyewe.
Vaihmanaw hoi Levih miphunnaw amamouh kâthoung sak teh abuemlahoi a thoung awh. Hahoi ceitakhai pawi nah san dawk hoi kahloutnaw hoi a hmaunawngha vaihmanaw hanelah tu a thei awh.
21 Hivyo Waisraeli waliokuwa wamerudi kutoka utumwani uhamishoni wakaila Pasaka, pamoja na wale waliokuwa wamejitenga na matendo ya unajisi wa Mataifa ya jirani ili kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli.
Hahoi Isarel catoun san dawk hoi kahlout ni teh Isarel BAWIPA Cathut ka tawng ni teh alouke ramnaw e lawk ngai laipalah, a yonnae naw thoung sak e pueng hoi a canei awh.
22 Kwa muda wa siku saba waliiadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa furaha, kwa sababu Bwana alikuwa amewajaza furaha kwa kubadilisha nia ya mfalme wa Ashuru kwamba awasaidie ujenzi wa nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.
Lung kanawmcalah tawn phuen hoeh e pawi hah hnin sari touh thung a sak awh. Bangkongtetpawiteh, BAWIPA ni ahnimanaw teh a lunghawi sak. Isarel Cathut e im saknae dawk a kut tha ao sak nahanelah Assiria siangpahrang e lungthin hah ahnimouh koe lah a kamlang sak.

< Ezra 6 >