< Ezra 5 >

1 Ndipo nabii Hagai na nabii Zekaria mzao wa Ido, wakawatolea unabii Wayahudi waliokuwa Yuda na Yerusalemu kwa jina la Mungu wa Israeli, aliyekuwa pamoja nao.
Potem prorocy Aggeusz i Zachariasz, syn Iddo, prorokowali Żydom w Judzie i w Jerozolimie w imię Boga Izraela, [mówiąc] do nich.
2 Ndipo Zerubabeli mwana wa Shealtieli na Yeshua mwana wa Yosadaki wakaanza kujenga tena nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Nao manabii wa Mungu walikuwa pamoja nao, wakiwasaidia.
Wtedy powstali Zorobabel, syn Szealtiela, i Jeszua, syn Jocadaka, i zaczęli budować dom Boży w Jerozolimie; a z nimi prorocy Boga, którzy im pomagali.
3 Wakati ule Tatenai mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao waliwaendea, wakawauliza, “Ni nani aliyewapa ruhusa ya kujenga tena Hekalu hili na kurudishia upya kama lilivyokuwa?”
W tym czasie przyszli do nich Tattenaj, namiestnik zarzecza, i Szetarboznaj oraz ich towarzysze i tak mówili do nich: Kto wam rozkazał budować ten dom i wznosić jego mury?
4 Pia waliwauliza, “Je, majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani?”
Odpowiedzieliśmy im, jakie są imiona tych mężczyzn, którzy pracują przy tej budowli.
5 Lakini jicho la Mungu wao lilikuwa likiwaangalia wazee wa Wayahudi, nao hawakuzuiliwa kujenga mpaka taarifa ikaandikwa kwa Dario na majibu yake kupokelewa.
Lecz oko ich Boga czuwało nad starszymi z Żydów, tak że nie mogli im przeszkadzać, dopóki sprawa ta nie dotarła do Dariusza – o niej donosili [mu] przez list.
6 Hii ni nakala ya barua ile Tatenai, mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao maafisa wa ngʼambo ya mto Frati waliyompelekea Mfalme Dario.
[To jest] odpis listu, który do króla Dariusza posłali Tattenaj, namiestnik zarzecza, Szetarboznaj i jego towarzysze Afarsachajczycy, którzy byli za rzeką.
7 Taarifa waliyompelekea ilisomeka kama ifuatavyo: Kwa Mfalme Dario: Salamu kwa moyo mkunjufu.
Posłali mu list, w którym było napisane tak: Królowi Dariuszowi wszelkiej pomyślności!
8 Inampasa Mfalme ajue kwamba tulikwenda katika eneo la Yuda, kwenye Hekalu la Mungu mkuu. Watu wanalijenga kwa mawe makubwa na kuweka mbao kwenye kuta. Kazi inafanyika kwa bidii na inaendelea kwa haraka chini ya uongozi wao.
Niech będzie królowi wiadomo, że przybyliśmy do prowincji Judy, do domu wielkiego Boga, który jest odbudowywany z wielkich kamieni, a [którego] ściany są wykładane drewnem. Ta praca posuwa się szybko i szczęści się w ich rękach.
9 Tuliwauliza viongozi, “Ni nani aliyewapa ruhusa kujenga upya Hekalu hili na kurejeza hali ya jengo kama lilivyokuwa?”
Pytaliśmy wtedy tych starszych, mówiąc do nich: Kto wam rozkazał budować ten dom i wznosić te mury?
10 Pia tuliwauliza majina yao, ili tukuandikie kukujulisha majina ya viongozi wao.
Pytaliśmy także o ich imiona, abyśmy mogli ci je oznajmić i zapisać imiona mężczyzn, którzy stoją na ich czele.
11 Hili ndilo jibu walilotupa: “Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunalijenga upya Hekalu ambalo lilijengwa miaka mingi iliyopita, lile ambalo mfalme mkuu wa Israeli alilijenga na kulikamilisha.
A tak nam odpowiedzieli: My jesteśmy sługami Boga nieba i ziemi i odbudowujemy dom, który został wzniesiony przed wieloma laty, a który zbudował i wystawił wielki król Izraela.
12 Lakini kwa sababu baba zetu walimkasirisha Mungu wa mbinguni, basi aliwatia mkononi mwa Nebukadneza, Mkaldayo, mfalme wa Babeli, ambaye aliliharibu Hekalu hili na kuwaondoa watu na kuwapeleka uhamishoni huko Babeli.
Lecz gdy nasi ojcowie pobudzili do gniewu Boga nieba, on wydał ich w ręce Nabuchodonozora, króla Babilonu, Chaldejczyka, który zburzył ten dom, a lud uprowadził do niewoli w Babilonie.
13 “Pamoja na hayo, katika mwaka wa kwanza wa kutawala Koreshi mfalme wa Babeli, Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujengwa upya nyumba hii ya Mungu.
Jednak w pierwszym roku Cyrusa, króla Babilonu, sam król Cyrus wydał dekret, aby odbudować ten dom Boży.
14 Yeye hata aliviondoa vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu, kutoka Hekalu la Babeli ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka ndani ya Hekalu huko Yerusalemu na kuvileta katika Hekalu la Babeli. “Vyombo hivyo Mfalme Koreshi alimkabidhi mtu aliyeitwa Sheshbaza, ambaye Koreshi alikuwa amemteua awe mtawala,
Ponadto złote i srebrne naczynia domu Bożego, które Nabuchodonozor zabrał ze świątyni w Jerozolimie i umieścił w świątyni w Babilonie, król Cyrus wyniósł ze świątyni w Babilonie i zostały przekazane niejakiemu Szeszbassarowi, którego ustanowił namiestnikiem.
15 naye akamwambia, ‘Chukua vyombo hivi uende ukaviweke ndani ya Hekalu huko Yerusalemu. Nawe uijenge upya nyumba ya Mungu mahali pake.’
I powiedział mu: Weź te naczynia, idź i złóż je w świątyni, która jest w Jerozolimie, a niech dom Boży zostanie odbudowany na swoim miejscu.
16 Hivyo huyu Sheshbaza alikuja na kuweka misingi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu. Tangu siku hiyo hadi sasa imekuwa ikiendelea kujengwa lakini bado haijamalizika.”
Wtedy ten Szeszbassar przyszedł i położył fundamenty domu Bożego w Jerozolimie, i od tego czasu aż do dzisiaj buduje się go, ale nie jest ukończony.
17 Sasa kama ikimpendeza mfalme, uchunguzi na ufanyike katika kumbukumbu za maandishi ya ufalme mjini Babeli, kuona kama kweli Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika Yerusalemu. Kisha tunaomba mfalme na atutumie uamuzi wake kuhusu jambo hili.
Jeśli więc król uzna to za dobrą rzecz, niech poszukają w skarbcach królewskich w Babilonie, czy [rzeczywiście] tak jest, że król Cyrus rozkazał, aby odbudować ten dom Boży w Jerozolimie, i niech król powiadomi nas o swej woli w tej sprawie.

< Ezra 5 >