< Ezra 5 >

1 Ndipo nabii Hagai na nabii Zekaria mzao wa Ido, wakawatolea unabii Wayahudi waliokuwa Yuda na Yerusalemu kwa jina la Mungu wa Israeli, aliyekuwa pamoja nao.
Or Aggée, le prophète, et Zacharie, fils d’Addo, prophétisèrent, prophétisant aux Juifs qui étaient en Judée et à Jérusalem, au nom du Dieu d’Israël.
2 Ndipo Zerubabeli mwana wa Shealtieli na Yeshua mwana wa Yosadaki wakaanza kujenga tena nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Nao manabii wa Mungu walikuwa pamoja nao, wakiwasaidia.
Alors se levèrent Zorobabel, fils de Salathiel, et Josué, fils de Josédec, et ils commencèrent à bâtir le temple de Dieu à Jérusalem, et avec eux les prophètes de Dieu qui les aidaient.
3 Wakati ule Tatenai mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao waliwaendea, wakawauliza, “Ni nani aliyewapa ruhusa ya kujenga tena Hekalu hili na kurudishia upya kama lilivyokuwa?”
Or, en ce temps-là, vinrent vers eux Thathanaï, qui était chef au-delà du fleuve, et Stharbuzanaï, et leurs conseillers, et c’est ainsi qu’ils leur dirent: Qui vous a donné le conseil de bâtir cette maison et de restaurer ses murs?
4 Pia waliwauliza, “Je, majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani?”
À quoi nous répondîmes en leur disant quels étaient les noms des hommes auteurs de cette construction.
5 Lakini jicho la Mungu wao lilikuwa likiwaangalia wazee wa Wayahudi, nao hawakuzuiliwa kujenga mpaka taarifa ikaandikwa kwa Dario na majibu yake kupokelewa.
Or l’œil de leur Dieu fut sur les anciens des Juifs, et ils ne purent les empêcher. Et il leur plut que l’affaire fût renvoyée à Darius, et qu’alors ils répondraient à cette accusation.
6 Hii ni nakala ya barua ile Tatenai, mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao maafisa wa ngʼambo ya mto Frati waliyompelekea Mfalme Dario.
Copie de la lettre que Thathanaï, chef de la contrée au-delà du fleuve, et Stharbuzanaï et ses conseillers Arphasachéens, qui étaient au-delà du fleuve, envoyèrent à Darius, le roi.
7 Taarifa waliyompelekea ilisomeka kama ifuatavyo: Kwa Mfalme Dario: Salamu kwa moyo mkunjufu.
La parole qu’ils lui avaient envoyée était écrite ainsi: À Darius, le roi, toute paix.
8 Inampasa Mfalme ajue kwamba tulikwenda katika eneo la Yuda, kwenye Hekalu la Mungu mkuu. Watu wanalijenga kwa mawe makubwa na kuweka mbao kwenye kuta. Kazi inafanyika kwa bidii na inaendelea kwa haraka chini ya uongozi wao.
Qu’il soit connu du roi que nous sommes allés dans la province de Judée, dans la maison du grand Dieu que l’on bâtit de pierres non polies et dont on pose les bois sur les murailles. Or cet ouvrage s’élève avec diligence et s’accroît entre leurs mains.
9 Tuliwauliza viongozi, “Ni nani aliyewapa ruhusa kujenga upya Hekalu hili na kurejeza hali ya jengo kama lilivyokuwa?”
Nous avons donc interrogé les vieillards, et c’est ainsi que nous leur avons dit: Qui vous a donné le pouvoir de bâtir cette maison et de rétablir ces murs?
10 Pia tuliwauliza majina yao, ili tukuandikie kukujulisha majina ya viongozi wao.
Mais nous leur avons aussi demandé leurs noms, afin de vous les indiquer, et nous avons écrit les noms des hommes qui sont les princes parmi eux.
11 Hili ndilo jibu walilotupa: “Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunalijenga upya Hekalu ambalo lilijengwa miaka mingi iliyopita, lile ambalo mfalme mkuu wa Israeli alilijenga na kulikamilisha.
Or ils nous ont répondu ces paroles, disant: Nous sommes serviteurs du Dieu du ciel et de la terre; nous bâtissons le temple qui était construit beaucoup d’années avant celles-ci, et que le grand roi d’Israël avait bâti et construit.
12 Lakini kwa sababu baba zetu walimkasirisha Mungu wa mbinguni, basi aliwatia mkononi mwa Nebukadneza, Mkaldayo, mfalme wa Babeli, ambaye aliliharibu Hekalu hili na kuwaondoa watu na kuwapeleka uhamishoni huko Babeli.
Mais après que nos pères eurent provoqué au courroux le Dieu au ciel, il les livra entre les mains de Nabuchodonosor, roi de Babylone, Chaldéen; et il détruisit même cette maison, et transporta son peuple à Babylone.
13 “Pamoja na hayo, katika mwaka wa kwanza wa kutawala Koreshi mfalme wa Babeli, Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujengwa upya nyumba hii ya Mungu.
Or, à la première année de Cyrus, roi de Babylone, le roi Cyrus publia un édit afin que cette maison de Dieu fût bâtie.
14 Yeye hata aliviondoa vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu, kutoka Hekalu la Babeli ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka ndani ya Hekalu huko Yerusalemu na kuvileta katika Hekalu la Babeli. “Vyombo hivyo Mfalme Koreshi alimkabidhi mtu aliyeitwa Sheshbaza, ambaye Koreshi alikuwa amemteua awe mtawala,
Et même les vases d’or et d’argent du temple de Dieu, que Nabuchodonosor avait enlevés du temple qui était à Jérusalem, et qu’il avait apportés dans le temple de Babylone, le roi Cyrus les tira du temple de Babylone, et ils furent donnés à un nommé Sassabasar, qu’il établit même prince.
15 naye akamwambia, ‘Chukua vyombo hivi uende ukaviweke ndani ya Hekalu huko Yerusalemu. Nawe uijenge upya nyumba ya Mungu mahali pake.’
Et il lui dit: Prends ces vases, et va, et mets-les dans le temple qui est à Jérusalem, et que la maison de Dieu soit bâtie en son lieu.
16 Hivyo huyu Sheshbaza alikuja na kuweka misingi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu. Tangu siku hiyo hadi sasa imekuwa ikiendelea kujengwa lakini bado haijamalizika.”
Alors donc ce Sassabasar vint, et posa les fondements du temple de Dieu à Jérusalem, et, depuis ce temps-là jusqu’à présent, on le bâtit, et il n’est pas encore achevé.
17 Sasa kama ikimpendeza mfalme, uchunguzi na ufanyike katika kumbukumbu za maandishi ya ufalme mjini Babeli, kuona kama kweli Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika Yerusalemu. Kisha tunaomba mfalme na atutumie uamuzi wake kuhusu jambo hili.
Maintenant donc, s’il semble bon au roi, qu’il recherche dans la bibliothèque du roi, qui est à Babylone, s’il a été ordonné par le roi Cyrus que la maison de Dieu serait rebâtie à Jérusalem, et qu’il nous envoie la volonté du roi sur cela.

< Ezra 5 >