< Ezra 5 >

1 Ndipo nabii Hagai na nabii Zekaria mzao wa Ido, wakawatolea unabii Wayahudi waliokuwa Yuda na Yerusalemu kwa jina la Mungu wa Israeli, aliyekuwa pamoja nao.
Les prophètes, Aggée le prophète et Zacharie le fils d'Iddo, prophétisèrent aux Juifs qui étaient en Judée et à Jérusalem. Ils leur prophétisèrent au nom du Dieu d'Israël.
2 Ndipo Zerubabeli mwana wa Shealtieli na Yeshua mwana wa Yosadaki wakaanza kujenga tena nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Nao manabii wa Mungu walikuwa pamoja nao, wakiwasaidia.
Alors Zorobabel, fils de Shealtiel, et Josué, fils de Jozadak, se levèrent et commencèrent à bâtir la maison de Dieu qui est à Jérusalem; et avec eux les prophètes de Dieu, qui les aidaient.
3 Wakati ule Tatenai mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao waliwaendea, wakawauliza, “Ni nani aliyewapa ruhusa ya kujenga tena Hekalu hili na kurudishia upya kama lilivyokuwa?”
Au même moment, Tattenaï, gouverneur de l'autre côté du fleuve, vint vers eux, avec Shetharbozenaï et leurs compagnons, et leur demanda: « Qui vous a donné l'ordre de construire cette maison et d'achever ce mur? »
4 Pia waliwauliza, “Je, majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani?”
Ils demandèrent aussi les noms des hommes qui construisaient cette maison.
5 Lakini jicho la Mungu wao lilikuwa likiwaangalia wazee wa Wayahudi, nao hawakuzuiliwa kujenga mpaka taarifa ikaandikwa kwa Dario na majibu yake kupokelewa.
Mais l'œil de leur Dieu était sur les anciens des Juifs, et ils ne les firent pas cesser jusqu'à ce que l'affaire parvienne à Darius, et qu'une réponse leur soit donnée par lettre à ce sujet.
6 Hii ni nakala ya barua ile Tatenai, mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao maafisa wa ngʼambo ya mto Frati waliyompelekea Mfalme Dario.
Voici la copie de la lettre que Tattenaï, gouverneur de l'autre côté du fleuve, Schetharbozenaï et ses compagnons, les Apharsachites qui étaient de l'autre côté du fleuve, envoyèrent au roi Darius.
7 Taarifa waliyompelekea ilisomeka kama ifuatavyo: Kwa Mfalme Dario: Salamu kwa moyo mkunjufu.
Ils lui envoyèrent une lettre, dans laquelle était écrit: Au roi Darius, toute la paix.
8 Inampasa Mfalme ajue kwamba tulikwenda katika eneo la Yuda, kwenye Hekalu la Mungu mkuu. Watu wanalijenga kwa mawe makubwa na kuweka mbao kwenye kuta. Kazi inafanyika kwa bidii na inaendelea kwa haraka chini ya uongozi wao.
Sachez au roi que nous sommes allés dans la province de Juda, à la maison du grand Dieu, qui se construit avec de grosses pierres et dont les murs sont couverts de bois. Cet ouvrage se poursuit avec diligence et prospère entre leurs mains.
9 Tuliwauliza viongozi, “Ni nani aliyewapa ruhusa kujenga upya Hekalu hili na kurejeza hali ya jengo kama lilivyokuwa?”
Alors nous avons interrogé ces anciens, et nous leur avons dit ainsi: « Qui vous a donné l'ordre de construire cette maison et d'achever cette muraille? »
10 Pia tuliwauliza majina yao, ili tukuandikie kukujulisha majina ya viongozi wao.
Nous leur demandâmes aussi leurs noms, afin que nous puissions écrire les noms des hommes qui étaient à leur tête.
11 Hili ndilo jibu walilotupa: “Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunalijenga upya Hekalu ambalo lilijengwa miaka mingi iliyopita, lile ambalo mfalme mkuu wa Israeli alilijenga na kulikamilisha.
Ils nous répondirent en disant: « Nous sommes les serviteurs du Dieu du ciel et de la terre et nous bâtissons la maison qui a été construite il y a tant d'années, qu'un grand roi d'Israël a bâtie et achevée.
12 Lakini kwa sababu baba zetu walimkasirisha Mungu wa mbinguni, basi aliwatia mkononi mwa Nebukadneza, Mkaldayo, mfalme wa Babeli, ambaye aliliharibu Hekalu hili na kuwaondoa watu na kuwapeleka uhamishoni huko Babeli.
Mais après que nos pères eurent provoqué le Dieu du ciel à la colère, il les livra entre les mains de Nabuchodonosor, roi de Babylone, le Chaldéen, qui détruisit cette maison et emmena le peuple à Babylone.
13 “Pamoja na hayo, katika mwaka wa kwanza wa kutawala Koreshi mfalme wa Babeli, Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujengwa upya nyumba hii ya Mungu.
Mais la première année de Cyrus, roi de Babylone, le roi Cyrus donna l'ordre de construire cette maison de Dieu.
14 Yeye hata aliviondoa vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu, kutoka Hekalu la Babeli ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka ndani ya Hekalu huko Yerusalemu na kuvileta katika Hekalu la Babeli. “Vyombo hivyo Mfalme Koreshi alimkabidhi mtu aliyeitwa Sheshbaza, ambaye Koreshi alikuwa amemteua awe mtawala,
Les objets d'or et d'argent de la maison de Dieu, que Nabuchodonosor avait enlevés du temple de Jérusalem et transportés dans le temple de Babylone, le roi Cyrus les enleva aussi du temple de Babylone et les remit à un certain Sheshbazzar, qu'il avait nommé gouverneur.
15 naye akamwambia, ‘Chukua vyombo hivi uende ukaviweke ndani ya Hekalu huko Yerusalemu. Nawe uijenge upya nyumba ya Mungu mahali pake.’
Il lui dit: « Prends ces ustensiles, va les mettre dans le temple de Jérusalem, et que la maison de Dieu soit bâtie à sa place ».
16 Hivyo huyu Sheshbaza alikuja na kuweka misingi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu. Tangu siku hiyo hadi sasa imekuwa ikiendelea kujengwa lakini bado haijamalizika.”
Alors le même Sheshbazzar vint et posa les fondations de la maison de Dieu qui est à Jérusalem. Depuis ce temps-là, jusqu'à maintenant, elle a été construite, et pourtant elle n'est pas achevée.
17 Sasa kama ikimpendeza mfalme, uchunguzi na ufanyike katika kumbukumbu za maandishi ya ufalme mjini Babeli, kuona kama kweli Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika Yerusalemu. Kisha tunaomba mfalme na atutumie uamuzi wake kuhusu jambo hili.
Maintenant, si le roi le trouve bon, que l'on cherche dans la maison du trésor du roi, qui est là à Babylone, s'il est vrai qu'un décret a été pris par le roi Cyrus pour construire cette maison de Dieu à Jérusalem; et que le roi nous envoie son bon plaisir à ce sujet. »

< Ezra 5 >