< Ezra 5 >

1 Ndipo nabii Hagai na nabii Zekaria mzao wa Ido, wakawatolea unabii Wayahudi waliokuwa Yuda na Yerusalemu kwa jina la Mungu wa Israeli, aliyekuwa pamoja nao.
Then Haggai a Prophet and Zechariah the sonne of Iddo a Prophet prophecied vnto the Iewes that were in Iudah, and Ierusalem, in the name of the God of Israel, euen vnto them.
2 Ndipo Zerubabeli mwana wa Shealtieli na Yeshua mwana wa Yosadaki wakaanza kujenga tena nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Nao manabii wa Mungu walikuwa pamoja nao, wakiwasaidia.
Then Zerubbabel the sonne of Shealtiel, and Ieshua the sonne of Iozadak arose, and began to builde the house of God at Ierusalem, and with them were the Prophetes of God, which helped them.
3 Wakati ule Tatenai mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao waliwaendea, wakawauliza, “Ni nani aliyewapa ruhusa ya kujenga tena Hekalu hili na kurudishia upya kama lilivyokuwa?”
At the same time came to them Tatnai, which was captaine beyonde the Riuer, and Shether-boznai and their companions, and sayd thus vnto them, Who hath giuen you commandement to buylde this house, and to lay the foundations of these walles?
4 Pia waliwauliza, “Je, majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani?”
Then sayde we vnto them after this maner, What are the names of the men that buylde this buylding?
5 Lakini jicho la Mungu wao lilikuwa likiwaangalia wazee wa Wayahudi, nao hawakuzuiliwa kujenga mpaka taarifa ikaandikwa kwa Dario na majibu yake kupokelewa.
But the eye of their God was vpon the Elders of the Iewes, that they coulde not cause them to cease, till the matter came to Darius: and then they answered by letters thereunto.
6 Hii ni nakala ya barua ile Tatenai, mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao maafisa wa ngʼambo ya mto Frati waliyompelekea Mfalme Dario.
The copie of the letter, that Tatnai captaine beyond the Riuer, and Shether-boznai and his companions, Apharsechaie, (which were beyond the Riuer) sent vnto King Darius.
7 Taarifa waliyompelekea ilisomeka kama ifuatavyo: Kwa Mfalme Dario: Salamu kwa moyo mkunjufu.
They sent a letter vnto him, wherein it was written thus, VNTO DARIVS the king, all peace.
8 Inampasa Mfalme ajue kwamba tulikwenda katika eneo la Yuda, kwenye Hekalu la Mungu mkuu. Watu wanalijenga kwa mawe makubwa na kuweka mbao kwenye kuta. Kazi inafanyika kwa bidii na inaendelea kwa haraka chini ya uongozi wao.
Be it knowen vnto the King, that we went into the prouince of Iudea, to the house of the great God, which is builded with great stones, and beames are layde in the walles, and this worke is wrought speedily, and prospereth in their hands.
9 Tuliwauliza viongozi, “Ni nani aliyewapa ruhusa kujenga upya Hekalu hili na kurejeza hali ya jengo kama lilivyokuwa?”
Then asked we those Elders, and sayd vnto them thus, Who hath giuen you commandement to buylde this house, and to lay the foundation of these walles?
10 Pia tuliwauliza majina yao, ili tukuandikie kukujulisha majina ya viongozi wao.
We asked their names also, that we might certifie thee, and that we might write the names of the men that were their rulers.
11 Hili ndilo jibu walilotupa: “Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunalijenga upya Hekalu ambalo lilijengwa miaka mingi iliyopita, lile ambalo mfalme mkuu wa Israeli alilijenga na kulikamilisha.
But they answered vs thus, and sayd, We are the seruants of the God of heauen and earth, and buylde the house that was buylt of olde and many yeeres ago, which a great King of Israel builded, and founded it.
12 Lakini kwa sababu baba zetu walimkasirisha Mungu wa mbinguni, basi aliwatia mkononi mwa Nebukadneza, Mkaldayo, mfalme wa Babeli, ambaye aliliharibu Hekalu hili na kuwaondoa watu na kuwapeleka uhamishoni huko Babeli.
But after that our fathers had prouoked the God of heauen vnto wrath, he gaue them ouer into the hand of Nebuchadnezzar King of Babel the Caldean, and he destroyed this house, and caryed the people away captiue vnto Babel.
13 “Pamoja na hayo, katika mwaka wa kwanza wa kutawala Koreshi mfalme wa Babeli, Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujengwa upya nyumba hii ya Mungu.
But in the first yere of Cyrus King of Babel, King Cyrus made a decree to buylde this house of God.
14 Yeye hata aliviondoa vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu, kutoka Hekalu la Babeli ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka ndani ya Hekalu huko Yerusalemu na kuvileta katika Hekalu la Babeli. “Vyombo hivyo Mfalme Koreshi alimkabidhi mtu aliyeitwa Sheshbaza, ambaye Koreshi alikuwa amemteua awe mtawala,
And the vessels of golde and siluer of the house of God, which Nebuchadnezzar tooke out of the Temple, that was in Ierusalem, and brought them into the Temple of Babel, those did Cyrus the king take out of the Temple of Babel, and they gaue them vnto one Sheshbazzar by his name, whome he had made captaine.
15 naye akamwambia, ‘Chukua vyombo hivi uende ukaviweke ndani ya Hekalu huko Yerusalemu. Nawe uijenge upya nyumba ya Mungu mahali pake.’
And he sayde vnto him, Take these vessels and goe thy way, and put them in the Temple that is in Ierusalem, and let the house of God be buylt in his place.
16 Hivyo huyu Sheshbaza alikuja na kuweka misingi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu. Tangu siku hiyo hadi sasa imekuwa ikiendelea kujengwa lakini bado haijamalizika.”
Then came the same Sheshbazzar and layde the foundation of the house of God, which is in Ierusalem, and since that time euen vntill nowe, hath it bene in buylding, yet is it not finished.
17 Sasa kama ikimpendeza mfalme, uchunguzi na ufanyike katika kumbukumbu za maandishi ya ufalme mjini Babeli, kuona kama kweli Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika Yerusalemu. Kisha tunaomba mfalme na atutumie uamuzi wake kuhusu jambo hili.
Nowe therefore if it please the King, let there be searche made in the house of the Kings treasures, which is there in Babel, whether a decree hath bene made by King Cyrus, to build this house of God in Ierusalem, and let the King send his minde concerning this.

< Ezra 5 >