< Ezra 5 >
1 Ndipo nabii Hagai na nabii Zekaria mzao wa Ido, wakawatolea unabii Wayahudi waliokuwa Yuda na Yerusalemu kwa jina la Mungu wa Israeli, aliyekuwa pamoja nao.
Og Profeterne, Profeten Haggaj og Sakarias, Iddo's Søn, profeterede for Jøderne, som vare i Juda og Jerusalem, i Israels Guds Navn, som var over dem.
2 Ndipo Zerubabeli mwana wa Shealtieli na Yeshua mwana wa Yosadaki wakaanza kujenga tena nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Nao manabii wa Mungu walikuwa pamoja nao, wakiwasaidia.
Da gjorde Serubabel, Sealthiels Søn, og Jesua, Jozadaks Søn, sig rede og begyndte at bygge Guds Hus, som var i Jerusalem, og med dem de Guds Profeter, som styrkede dem.
3 Wakati ule Tatenai mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao waliwaendea, wakawauliza, “Ni nani aliyewapa ruhusa ya kujenga tena Hekalu hili na kurudishia upya kama lilivyokuwa?”
Paa den Tid kom Thatnaj, Landshøvdingen paa denne Side Floden, og Sthar-Bosnaj og deres Selskab til dem og sagde til dem: Hvo har givet eder Befaling om at bygge dette Hus og at fuldføre denne Mur?
4 Pia waliwauliza, “Je, majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani?”
Da sagde vi altsaa til dem, hvad de Mænd hed, som byggede denne Bygning.
5 Lakini jicho la Mungu wao lilikuwa likiwaangalia wazee wa Wayahudi, nao hawakuzuiliwa kujenga mpaka taarifa ikaandikwa kwa Dario na majibu yake kupokelewa.
Og over Jødernes Ældste var deres Guds Øje, og man forhindrede dem ikke, indtil der kom Befaling fra Darius, og man da sendte dem Brev tilbage derom.
6 Hii ni nakala ya barua ile Tatenai, mtawala wa ngʼambo ya mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao maafisa wa ngʼambo ya mto Frati waliyompelekea Mfalme Dario.
Afskriften af Brevet, som Thatnaj, Landshøvdingen paa denne Side Floden, og Sthar-Bosnaj og hans Selskab, de fra Afarsakta, som vare paa den Side Floden, sendte til Kong Darius; —
7 Taarifa waliyompelekea ilisomeka kama ifuatavyo: Kwa Mfalme Dario: Salamu kwa moyo mkunjufu.
de sendte Beretningen til ham, og saaledes var der skrevet i den: Kong Darius ønske vi al Fred!
8 Inampasa Mfalme ajue kwamba tulikwenda katika eneo la Yuda, kwenye Hekalu la Mungu mkuu. Watu wanalijenga kwa mawe makubwa na kuweka mbao kwenye kuta. Kazi inafanyika kwa bidii na inaendelea kwa haraka chini ya uongozi wao.
Det være Kongen vitterligt, at vi kom til det Landskab Juda, til den store Guds Hus, og at man bygger det med storø Stene og lægger Træ i Væggene, og at Arbejdet gaar rask frem og lykkes ved deres Hænder.
9 Tuliwauliza viongozi, “Ni nani aliyewapa ruhusa kujenga upya Hekalu hili na kurejeza hali ya jengo kama lilivyokuwa?”
Da spurgte vi disse. Ældste ad og sagde saaledes til dem: Hvo har givet eder Befaling om at bygge dette Hus og at fuldføre denne Mur?
10 Pia tuliwauliza majina yao, ili tukuandikie kukujulisha majina ya viongozi wao.
Vi spurgte og om deres Navne for at give dig dem til Kende, at vi kunde skrive de Mænds Navne, som vare deres Øverster.
11 Hili ndilo jibu walilotupa: “Sisi ni watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunalijenga upya Hekalu ambalo lilijengwa miaka mingi iliyopita, lile ambalo mfalme mkuu wa Israeli alilijenga na kulikamilisha.
Og de gave os saadant Svar tilbage og sagde: Vi ere Himmelens og Jordens Guds Tjenere og bygge et Hus, som var fordum bygget, for mange Aar siden; thi en stor Konge i Israel havde bygget det og fuldført det.
12 Lakini kwa sababu baba zetu walimkasirisha Mungu wa mbinguni, basi aliwatia mkononi mwa Nebukadneza, Mkaldayo, mfalme wa Babeli, ambaye aliliharibu Hekalu hili na kuwaondoa watu na kuwapeleka uhamishoni huko Babeli.
Men efterdi vore Fædre havde fortørnet Himmelens Gud, gav han dem i Kongen af Babel, Kaldæeren Nebukadnezars Haand, og denne nedbrød dette Hus og førte Folket bort til Babel.
13 “Pamoja na hayo, katika mwaka wa kwanza wa kutawala Koreshi mfalme wa Babeli, Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujengwa upya nyumba hii ya Mungu.
Men i Kongen af Babel, Kyrus's første Aar, gav Kong Kyrus Befaling at bygge dette Guds Hus.
14 Yeye hata aliviondoa vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu, kutoka Hekalu la Babeli ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka ndani ya Hekalu huko Yerusalemu na kuvileta katika Hekalu la Babeli. “Vyombo hivyo Mfalme Koreshi alimkabidhi mtu aliyeitwa Sheshbaza, ambaye Koreshi alikuwa amemteua awe mtawala,
Ja, ogsaa de Guds Hus's Kar, som vare af Guld og Sølv, hvilke Nebukadnezar havde udtaget af Templet, som var i Jerusalem, og ført til Templet i Babel, dem udtog Kong Kyrus af Templet i Babel, og de bleve givne en, hvis Navn var Sesbazar, hvilken han satte til Landshøvding.
15 naye akamwambia, ‘Chukua vyombo hivi uende ukaviweke ndani ya Hekalu huko Yerusalemu. Nawe uijenge upya nyumba ya Mungu mahali pake.’
Og han sagde til ham: Tag disse Kar, gak bort og bring dem ind i Templet, som er i Jerusalem, og lad Guds Hus bygges paa sit Sted!
16 Hivyo huyu Sheshbaza alikuja na kuweka misingi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu. Tangu siku hiyo hadi sasa imekuwa ikiendelea kujengwa lakini bado haijamalizika.”
Da kom den samme Sesbazar, han lagde Grundvolden til Guds Hus, som er i Jerusalem; og fra da af og indtil nu bygges det og er ikke fuldført.
17 Sasa kama ikimpendeza mfalme, uchunguzi na ufanyike katika kumbukumbu za maandishi ya ufalme mjini Babeli, kuona kama kweli Mfalme Koreshi alitoa amri ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika Yerusalemu. Kisha tunaomba mfalme na atutumie uamuzi wake kuhusu jambo hili.
Og dersom det nu synes godt for Kongen, saa lad der blive eftersøgt i Kongens Skatkammer, som er i Babel, om det er saa, at der er given Befaling af Kong Kyrus om at bygge dette Guds Hus i Jerusalem, og man sende os Kongens Vilje derom!