< Ezra 4 >

1 Adui za Yuda na Benyamini waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni wanajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli,
Or les ennemis de Juda et de Benjamin apprirent que les enfants de la captivité rebâtissaient le temple de l'Éternel, le Dieu d'Israël.
2 wakamjia Zerubabeli na viongozi wa jamaa, nao wakasema, “Turuhusuni tuwasaidie kujenga, kwa sababu sisi tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu wakati wa Esar-Hadoni mfalme wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”
Ils vinrent vers Zorobabel et vers les chefs des pères, et leur dirent: Nous bâtirons avec vous; car nous invoquerons votre Dieu comme vous; et c'est à lui que nous sacrifions depuis le temps d'Ésar-Haddon, roi d'Assyrie, qui nous a fait monter ici.
3 Lakini Zerubabeli, Yeshua na viongozi wengine wa jamaa ya Israeli wakawajibu, “Ninyi hamna sehemu nasi katika kujenga Hekalu la Mungu wetu. Sisi peke yetu tutajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli, kama Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi alivyotuagiza.”
Mais Zorobabel, Jéshua, et les autres chefs des pères d'Israël, leur répondirent: Il ne convient pas que vous et nous, nous bâtissions une maison à notre Dieu; mais nous la bâtirons nous seuls à l'Éternel, le Dieu d'Israël, comme le roi Cyrus, roi de Perse, nous l'a commandé.
4 Ndipo watu waliowazunguka wakajipanga kuwakatisha tamaa watu wa Yuda na kuwafanya waogope walipokuwa wakiendelea na ujenzi.
Alors le peuple du pays rendit lâches les mains du peuple de Juda, en l'effrayant pour l'empêcher de bâtir;
5 Wakaajiri washauri kuwapinga katika kazi yao, nao wakaipinga mipango yao wakati wote wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi hadi wakati wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
Et ils soudoyèrent contre eux des conseillers pour dissiper leur entreprise, pendant tout le temps de Cyrus, roi de Perse, jusqu'au règne de Darius, roi de Perse.
6 Mnamo mwanzo wa utawala wa Ahasuero, hao adui waliandika mashtaka dhidi ya watu wa Yuda na Yerusalemu.
Puis, pendant le règne d'Assuérus, au commencement de son règne, ils écrivirent une accusation contre les habitants de Juda et de Jérusalem.
7 Pia katika siku za utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli pamoja na wenzao waliandika barua kwa Artashasta. Barua hiyo iliandikwa kwa mwandiko wa Kiaramu na katika lugha ya Kiaramu.
Et du temps d'Artaxerxès, Bishlam, Mithrédath, Tabéel, et les autres de leurs collègues, écrivirent à Artaxerxès, roi de Perse. La lettre fut écrite en caractères araméens et traduite en araméen.
8 Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai waliandika barua kwa Mfalme Artashasta dhidi ya watu wa Yerusalemu kama ifuatavyo:
Réhum, gouverneur, et Shimshaï, secrétaire, écrivirent donc en ces termes une lettre, touchant Jérusalem, au roi Artaxerxès:
9 Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai, pamoja na wenzao, yaani mahakimu na maafisa walio juu ya watu kuanzia Tripoli, Uajemi, Ereki na Babeli, Waelami wa Shushani,
Réhum, gouverneur et Shimshaï, secrétaire, et les autres de leurs collègues, Diniens, Apharsathkiens, Tarpéliens, Arphasiens, Arkéviens, Babyloniens, Susankiens, Déhaviens, Élamites,
10 na watu wengine ambao mheshimiwa Asur-Banipali aliwahamisha na kuwakalisha katika mji wa Samaria na mahali pengine Ngʼambo ya Mto Frati.
Et les autres peuples que le grand et illustre Osnapar a transportés et fait habiter dans la ville de Samarie, et autres villes de ce côté-ci du fleuve, - et ainsi de suite.
11 (Hii ndiyo nakala ya barua waliyompelekea.) Kwa Mfalme Artashasta, Kutoka kwa watumishi wako, watu wa Ngʼambo ya Mto Frati:
C'est ici la copie de la lettre qu'ils lui envoyèrent: Au roi Artaxerxès: Tes serviteurs, les gens de ce côté-ci du fleuve, - et ainsi de suite.
12 Yapasa Mfalme ajue kuwa Wayahudi waliopanda kuja kwetu kutoka kwenu, wamekwenda Yerusalemu nao wanaujenga upya ule mji wa uasi na uovu. Wanajenga kuta upya na kukarabati misingi yake.
Que le roi sache que les Juifs qui sont montés d'auprès de toi vers nous, sont venus à Jérusalem; qu'ils rebâtissent cette ville rebelle et méchante, qu'ils en relèvent les murailles et en restaurent les fondements.
13 Zaidi ya hayo, mfalme yampasa ajue kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikafanywa upya, hakutakuwa na ulipaji wa kodi wala ada au ushuru, hivyo hazina za mfalme zitaathirika.
Maintenant, que le roi sache que si cette ville est rebâtie et ses murailles relevées, on ne paiera plus de tribut, ni d'impôts, ni de péage, et que finalement elle portera dommage aux rois.
14 Sisi sasa kwa kuwa tunawajibika kwa jumba la kifalme na kwamba siyo sawasawa kwetu kuona mfalme akidharauliwa, basi tunatuma ujumbe huu kumtaarifu mfalme,
Or, comme nous mangeons le sel du palais, et qu'il n'est pas convenable que nous soyons témoins de ce dommage fait au roi, nous envoyons cette lettre au roi et lui faisons savoir ceci:
15 ili kwamba ufanyike uchunguzi kwenye kumbukumbu ya maandishi ya waliokutangulia. Katika kumbukumbu hizi utagundua kwamba mji huu ni wa maasi, unaowataabisha wafalme na majimbo, ni mahali pa maasi tangu zamani. Ndiyo maana mji huu uliharibiwa.
Qu'on cherche au livre des mémoires de tes pères, tu trouveras dans le livre des mémoires et tu apprendras que cette ville est une ville rebelle et pernicieuse aux rois et aux provinces, et que de tout temps on y a fait des séditions; c'est pour cela que cette ville a été détruite.
16 Tunamjulisha mfalme kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikifanywa upya, hutabakiwa na chochote Ngʼambo ya Mto Frati.
Nous faisons savoir au roi, que si cette ville est rebâtie et ses murailles relevées, tu n'auras plus de possessions de ce côté-ci du fleuve.
17 Mfalme alirudisha jibu hili: Kwa Rehumu, afisa msimamizi, mwandishi Shimshai na wenzenu wote wanaoishi katika Samaria na penginepo Ngʼambo ya Mto Frati: Salamu.
Le roi envoya cette réponse à Réhum, gouverneur, à Shimshaï, secrétaire, et à leurs autres collègues qui habitaient à Samarie, et autres lieux de ce côté-ci du fleuve: Salut, - et ainsi de suite.
18 Barua mliyotutumia imesomwa na kutafsiriwa mbele yangu.
La lettre que vous nous avez envoyée, a été exactement lue devant moi.
19 Nilitoa amri na uchunguzi ukafanyika na imegundulika kwamba mji huu una historia ndefu ya maasi dhidi ya wafalme na pamekuwa mahali pa maasi na uchochezi.
J'ai donné ordre, et on a cherché, et on a trouvé que, de tout temps, cette ville-là s'est élevée contre les rois, et qu'on y a fait des séditions et des révoltes;
20 Yerusalemu umepata kuwa na wafalme wenye nguvu wakitawala nchi yote iliyo Ngʼambo ya Mto Frati, wakitoza kodi, ada na ushuru huko.
Et qu'il y a eu des rois puissants à Jérusalem, qui ont dominé sur tout ce qui est au delà du fleuve, et qu'on leur payait le tribut, l'impôt et le péage.
21 Kwa hiyo toeni amri kwa watu hawa wasimamishe ujenzi, ili kwamba mji huu usiendelee kujengwa hadi nitakapoagiza.
Maintenant donc donnez l'ordre de faire cesser ces gens-là, afin que cette ville ne soit point rebâtie, jusqu'à ce qu'un ordre en soit donné de ma part.
22 Mwe waangalifu msipuuze jambo hili. Kwa nini kuruhusu tishio hili kuendelea na kusababisha hasara kwa ufalme?
Et gardez-vous de manquer d'agir d'après cela. Pourquoi s'accroîtrait le dommage au préjudice des rois?
23 Mara waliposomewa nakala ya barua ya Mfalme Artashasta, Rehumu na Shimshai aliyekuwa mwandishi na wenzao, walikwenda mara moja kwa Wayahudi huko Yerusalemu na kuwalazimisha kwa nguvu kusimamisha ujenzi.
Or, dès que la copie de la lettre du roi Artaxerxès eut été lue en la présence de Réhum, de Shimshaï, secrétaire, et de leurs collègues, ils s'en allèrent en hâte à Jérusalem vers les Juifs, et les firent cesser à main forte.
24 Hivyo kazi ya ujenzi wa nyumba ya Mungu huko Yerusalemu ikasimamishwa kabisa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
Alors l'ouvrage de la maison de Dieu, qui est à Jérusalem, cessa, et fut arrêté jusqu'à la seconde année du règne de Darius, roi de Perse.

< Ezra 4 >