< Ezra 4 >
1 Adui za Yuda na Benyamini waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni wanajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli,
Les adversaires de Juda et de Benjamin apprirent que les fils de la captivité construisaient un temple à Yahvé, le Dieu d'Israël.
2 wakamjia Zerubabeli na viongozi wa jamaa, nao wakasema, “Turuhusuni tuwasaidie kujenga, kwa sababu sisi tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu wakati wa Esar-Hadoni mfalme wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”
Ils s'approchèrent de Zorobabel et des chefs de famille, et leur dirent: « Laissez-nous construire avec vous, car nous cherchons votre Dieu comme vous, et nous lui offrons des sacrifices depuis le temps d'Esar Haddon, roi d'Assyrie, qui nous a fait monter ici. »
3 Lakini Zerubabeli, Yeshua na viongozi wengine wa jamaa ya Israeli wakawajibu, “Ninyi hamna sehemu nasi katika kujenga Hekalu la Mungu wetu. Sisi peke yetu tutajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli, kama Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi alivyotuagiza.”
Mais Zorobabel, Josué et le reste des chefs de famille d'Israël leur dirent: « Vous n'avez rien à faire avec nous pour bâtir une maison à notre Dieu; mais nous, ensemble, nous bâtirons à Yahvé, le Dieu d'Israël, comme le roi Cyrus, roi de Perse, nous l'a ordonné. »
4 Ndipo watu waliowazunguka wakajipanga kuwakatisha tamaa watu wa Yuda na kuwafanya waogope walipokuwa wakiendelea na ujenzi.
Alors les gens du pays affaiblirent les mains du peuple de Juda et le troublèrent dans ses travaux.
5 Wakaajiri washauri kuwapinga katika kazi yao, nao wakaipinga mipango yao wakati wote wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi hadi wakati wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
Ils engagèrent contre eux des conseillers pour faire échouer leurs projets, pendant toute la durée du règne de Cyrus, roi de Perse, et jusqu'au règne de Darius, roi de Perse.
6 Mnamo mwanzo wa utawala wa Ahasuero, hao adui waliandika mashtaka dhidi ya watu wa Yuda na Yerusalemu.
Sous le règne d'Assuérus, au début de son règne, ils écrivirent une accusation contre les habitants de Juda et de Jérusalem.
7 Pia katika siku za utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli pamoja na wenzao waliandika barua kwa Artashasta. Barua hiyo iliandikwa kwa mwandiko wa Kiaramu na katika lugha ya Kiaramu.
Au temps d'Artaxerxès, Bishlam, Mithredath, Tabeel et le reste de ses compagnons écrivirent à Artaxerxès, roi de Perse; la lettre fut écrite en syrien et remise en langue syrienne.
8 Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai waliandika barua kwa Mfalme Artashasta dhidi ya watu wa Yerusalemu kama ifuatavyo:
Rehum, le chancelier, et Shimshai, le scribe, ont écrit une lettre contre Jérusalem au roi Artaxerxès, comme suit.
9 Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai, pamoja na wenzao, yaani mahakimu na maafisa walio juu ya watu kuanzia Tripoli, Uajemi, Ereki na Babeli, Waelami wa Shushani,
Rehum, le chancelier, Shimshai, le scribe, et le reste de leurs compagnons, les Dinaïtes, les Apharsathchites, les Tarpélites, les Apharsites, les Archevites, les Babyloniens, les Shushanchites, les Dehaits, les Elamites,
10 na watu wengine ambao mheshimiwa Asur-Banipali aliwahamisha na kuwakalisha katika mji wa Samaria na mahali pengine Ngʼambo ya Mto Frati.
et le reste des nations que le grand et noble Osnappar a fait venir et installer dans la ville de Samarie, et dans le reste du pays au-delà du fleuve, et ainsi de suite, ont écrit.
11 (Hii ndiyo nakala ya barua waliyompelekea.) Kwa Mfalme Artashasta, Kutoka kwa watumishi wako, watu wa Ngʼambo ya Mto Frati:
C'est la copie de la lettre qu'ils ont envoyée: Au roi Artaxerxès, de la part de tes serviteurs, le peuple de l'autre côté du fleuve.
12 Yapasa Mfalme ajue kuwa Wayahudi waliopanda kuja kwetu kutoka kwenu, wamekwenda Yerusalemu nao wanaujenga upya ule mji wa uasi na uovu. Wanajenga kuta upya na kukarabati misingi yake.
Que le roi sache que les Juifs qui sont montés de chez vous sont venus chez nous à Jérusalem. Ils construisent la ville rebelle et mauvaise, ils ont achevé les murs et réparé les fondations.
13 Zaidi ya hayo, mfalme yampasa ajue kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikafanywa upya, hakutakuwa na ulipaji wa kodi wala ada au ushuru, hivyo hazina za mfalme zitaathirika.
Sachez maintenant au roi que si cette ville est construite et les murs achevés, ils ne paieront ni tribut, ni coutume, ni péage, et à la fin, cela fera du tort aux rois.
14 Sisi sasa kwa kuwa tunawajibika kwa jumba la kifalme na kwamba siyo sawasawa kwetu kuona mfalme akidharauliwa, basi tunatuma ujumbe huu kumtaarifu mfalme,
Or, comme nous mangeons le sel du palais et qu'il n'est pas convenable pour nous de voir le déshonneur du roi, nous avons envoyé et informé le roi,
15 ili kwamba ufanyike uchunguzi kwenye kumbukumbu ya maandishi ya waliokutangulia. Katika kumbukumbu hizi utagundua kwamba mji huu ni wa maasi, unaowataabisha wafalme na majimbo, ni mahali pa maasi tangu zamani. Ndiyo maana mji huu uliharibiwa.
afin que des recherches soient faites dans le livre des archives de tes pères. Vous verrez dans le livre des archives, et vous saurez que cette ville est une ville rebelle, et qu'elle fait du tort aux rois et aux provinces, et qu'on y a déclenché des rébellions dans le passé. C'est pourquoi cette ville a été détruite.
16 Tunamjulisha mfalme kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikifanywa upya, hutabakiwa na chochote Ngʼambo ya Mto Frati.
Nous informons le roi que si cette ville est construite et que ses murs sont achevés, vous n'aurez aucune possession au-delà du fleuve.
17 Mfalme alirudisha jibu hili: Kwa Rehumu, afisa msimamizi, mwandishi Shimshai na wenzenu wote wanaoishi katika Samaria na penginepo Ngʼambo ya Mto Frati: Salamu.
Alors le roi envoya une réponse à Rehum, le chancelier, et à Shimshai, le scribe, et au reste de leurs compagnons qui habitent à Samarie, et dans le reste du pays au-delà du fleuve: La paix.
18 Barua mliyotutumia imesomwa na kutafsiriwa mbele yangu.
La lettre que vous nous avez envoyée a été lue en toute clarté devant moi.
19 Nilitoa amri na uchunguzi ukafanyika na imegundulika kwamba mji huu una historia ndefu ya maasi dhidi ya wafalme na pamekuwa mahali pa maasi na uchochezi.
J'ai décrété, on a fait des recherches, et il a été constaté que cette ville s'est insurgée contre des rois dans le passé, et qu'il s'y est produit des rébellions et des révoltes.
20 Yerusalemu umepata kuwa na wafalme wenye nguvu wakitawala nchi yote iliyo Ngʼambo ya Mto Frati, wakitoza kodi, ada na ushuru huko.
Il y a eu aussi à Jérusalem des rois puissants qui ont régné sur tout le pays au-delà du fleuve, et on leur a payé des tributs, des coutumes et des péages.
21 Kwa hiyo toeni amri kwa watu hawa wasimamishe ujenzi, ili kwamba mji huu usiendelee kujengwa hadi nitakapoagiza.
Prends maintenant un décret pour faire cesser ces hommes, et que cette ville ne soit pas bâtie jusqu'à ce qu'un décret soit pris par moi.
22 Mwe waangalifu msipuuze jambo hili. Kwa nini kuruhusu tishio hili kuendelea na kusababisha hasara kwa ufalme?
Veillez à ne pas vous relâcher en le faisant. Pourquoi le dommage se développerait-il au détriment des rois?
23 Mara waliposomewa nakala ya barua ya Mfalme Artashasta, Rehumu na Shimshai aliyekuwa mwandishi na wenzao, walikwenda mara moja kwa Wayahudi huko Yerusalemu na kuwalazimisha kwa nguvu kusimamisha ujenzi.
Et lorsque la copie de la lettre du roi Artaxerxès fut lue devant Rehum, Shimshai le scribe et leurs compagnons, ils se rendirent en hâte à Jérusalem auprès des Juifs et les obligèrent à cesser par la force des armes.
24 Hivyo kazi ya ujenzi wa nyumba ya Mungu huko Yerusalemu ikasimamishwa kabisa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
Alors on cessa de travailler à la maison de Dieu qui est à Jérusalem. Il s'arrêta jusqu'à la deuxième année du règne de Darius, roi de Perse.