< Ezra 4 >

1 Adui za Yuda na Benyamini waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni wanajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli,
Bvt the aduersaries of Iudah and Beniamin heard, that the children of the captiuitie builded the Temple vnto the Lord God of Israel.
2 wakamjia Zerubabeli na viongozi wa jamaa, nao wakasema, “Turuhusuni tuwasaidie kujenga, kwa sababu sisi tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu wakati wa Esar-Hadoni mfalme wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”
And they came to Zerubbabel, and to the chiefe fathers, and sayd vnto them, We wil builde with you: for we seeke the Lord your God as ye do, and we haue sacrificed vnto him since the time of Esar Haddon king of Asshur, which brought vs vp hither.
3 Lakini Zerubabeli, Yeshua na viongozi wengine wa jamaa ya Israeli wakawajibu, “Ninyi hamna sehemu nasi katika kujenga Hekalu la Mungu wetu. Sisi peke yetu tutajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli, kama Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi alivyotuagiza.”
Then Zerubbabel, and Ieshua, and the rest of the chiefe fathers of Israel, sayde vnto them, It is not for you, but for vs to buyld the house vnto our God: for we our selues together wil buylde it vnto the Lord God of Israel, as king Cyrus the king of Persia hath commanded vs.
4 Ndipo watu waliowazunguka wakajipanga kuwakatisha tamaa watu wa Yuda na kuwafanya waogope walipokuwa wakiendelea na ujenzi.
Wherefore the people of the land discouraged the people of Iudah, and troubled them in buylding,
5 Wakaajiri washauri kuwapinga katika kazi yao, nao wakaipinga mipango yao wakati wote wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi hadi wakati wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
And they hired counsellers against them, to hinder their deuise, all the dayes of Cyrus King of Persia, euen vntill the reigne of Darius King of Persia.
6 Mnamo mwanzo wa utawala wa Ahasuero, hao adui waliandika mashtaka dhidi ya watu wa Yuda na Yerusalemu.
And in the reigne of Ahashuerosh (in the beginning of his reigne) wrote they an accusation against the inhabitants of Iudah and Ierusalem.
7 Pia katika siku za utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli pamoja na wenzao waliandika barua kwa Artashasta. Barua hiyo iliandikwa kwa mwandiko wa Kiaramu na katika lugha ya Kiaramu.
And in the daies of Artahshashte, Mithredath, Tabeel, and the rest of their companions wrote when it was peace, vnto Artahshashte king of Persia, and the writing of the letter was the Aramites writing, and the thing declared was in the language of the Aramites.
8 Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai waliandika barua kwa Mfalme Artashasta dhidi ya watu wa Yerusalemu kama ifuatavyo:
Rehum the chancelour, and Shimshai the scribe wrote a letter against Ierusalem to Artahshashte the King, in this sort.
9 Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai, pamoja na wenzao, yaani mahakimu na maafisa walio juu ya watu kuanzia Tripoli, Uajemi, Ereki na Babeli, Waelami wa Shushani,
Then wrote Rehum the chauncelour, and Shimshai the scribe, and their companions Dinaie, and Apharsathcaie, Tarpelaie, Apharsaie, Archeuaie, Bablaie, Shushanchaie, Dehaue, Elmaie,
10 na watu wengine ambao mheshimiwa Asur-Banipali aliwahamisha na kuwakalisha katika mji wa Samaria na mahali pengine Ngʼambo ya Mto Frati.
And the rest of the people whom the great and noble Asnappar brought ouer, and set in the cities of Samaria, and other that are beyonde the Riuer and Cheeneth.
11 (Hii ndiyo nakala ya barua waliyompelekea.) Kwa Mfalme Artashasta, Kutoka kwa watumishi wako, watu wa Ngʼambo ya Mto Frati:
This is the copie of the letter that they sent vnto King Artahshashte, THY SERVANTS the men beyond the Riuer and Cheeneth, salute thee.
12 Yapasa Mfalme ajue kuwa Wayahudi waliopanda kuja kwetu kutoka kwenu, wamekwenda Yerusalemu nao wanaujenga upya ule mji wa uasi na uovu. Wanajenga kuta upya na kukarabati misingi yake.
Be it knowen vnto the King that ye Iewes, which came vp from thee to vs, are come vnto Ierusalem (a citie rebellious and wicked) and buylde, and lay the foundations of the walles, and haue ioyned the foundations.
13 Zaidi ya hayo, mfalme yampasa ajue kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikafanywa upya, hakutakuwa na ulipaji wa kodi wala ada au ushuru, hivyo hazina za mfalme zitaathirika.
Be it knowen nowe vnto the King, that if this citie be built, and the foundations of the walles layed, they will not giue tolle, tribute, nor custome: so shalt thou hinder the Kings tribute.
14 Sisi sasa kwa kuwa tunawajibika kwa jumba la kifalme na kwamba siyo sawasawa kwetu kuona mfalme akidharauliwa, basi tunatuma ujumbe huu kumtaarifu mfalme,
Nowe therefore because wee haue bene brought vp in the Kings palace, it was not meete for vs to see the Kings dishonour: for this cause haue we sent and certified the King,
15 ili kwamba ufanyike uchunguzi kwenye kumbukumbu ya maandishi ya waliokutangulia. Katika kumbukumbu hizi utagundua kwamba mji huu ni wa maasi, unaowataabisha wafalme na majimbo, ni mahali pa maasi tangu zamani. Ndiyo maana mji huu uliharibiwa.
That one may searche in the booke of the Chronicles of thy fathers, and thou shalt finde in the booke of the Chronicles, and perceiue that this citie is rebellious and noysome vnto Kings and prouinces, and that they haue moued sedition of olde time, for the which cause this citie was destroyed.
16 Tunamjulisha mfalme kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikifanywa upya, hutabakiwa na chochote Ngʼambo ya Mto Frati.
Wee certifie the King therefore, that if this citie be buylded, and the foundation of the walles layd, by this meanes the portion beyonde the Riuer shall not be thine.
17 Mfalme alirudisha jibu hili: Kwa Rehumu, afisa msimamizi, mwandishi Shimshai na wenzenu wote wanaoishi katika Samaria na penginepo Ngʼambo ya Mto Frati: Salamu.
The King sent an answere vnto Rehum the Chauncelour, and Shimshai the Scribe, and so the rest of their companions that dwelt in Samaria, and vnto the other beyond the Riuer, Shelam and Cheeth.
18 Barua mliyotutumia imesomwa na kutafsiriwa mbele yangu.
The letter which yee sent vnto vs, hath bene openly read before me,
19 Nilitoa amri na uchunguzi ukafanyika na imegundulika kwamba mji huu una historia ndefu ya maasi dhidi ya wafalme na pamekuwa mahali pa maasi na uchochezi.
And I haue commanded and they haue searched, and founde, that this citie of olde time hath made insurrection against kings, and hath rebelled, and rebellion hath bene committed therein.
20 Yerusalemu umepata kuwa na wafalme wenye nguvu wakitawala nchi yote iliyo Ngʼambo ya Mto Frati, wakitoza kodi, ada na ushuru huko.
There haue bene mightie kings also ouer Ierusalem, which haue ruled ouer all beyonde the Riuer, and tolle, tribute, and custome was giuen vnto them.
21 Kwa hiyo toeni amri kwa watu hawa wasimamishe ujenzi, ili kwamba mji huu usiendelee kujengwa hadi nitakapoagiza.
Make ye now a decree, that those men may cease, and that the citie be not buylt, till I haue giuen another commandement.
22 Mwe waangalifu msipuuze jambo hili. Kwa nini kuruhusu tishio hili kuendelea na kusababisha hasara kwa ufalme?
Take heede nowe that ye fayle not to doe this: why should domage grow to hurt the King?
23 Mara waliposomewa nakala ya barua ya Mfalme Artashasta, Rehumu na Shimshai aliyekuwa mwandishi na wenzao, walikwenda mara moja kwa Wayahudi huko Yerusalemu na kuwalazimisha kwa nguvu kusimamisha ujenzi.
When the copie of king Artahshashtes letter was read before Rehum and Shimshai the scribe, and their companions, they went vp in all the haste to Ierusalem vnto the Iewes, and caused them to cease by force and power.
24 Hivyo kazi ya ujenzi wa nyumba ya Mungu huko Yerusalemu ikasimamishwa kabisa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
Then ceased the worke of the house of God, which was in Ierusalem, and did stay vnto the second yeere of Darius King of Persia.

< Ezra 4 >