< Ezra 4 >
1 Adui za Yuda na Benyamini waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni wanajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli,
Der Judas og Benjamins Modstandere hørte, at de Folk, som havde været bortførte, byggede Templet for Herren, Israels Gud,
2 wakamjia Zerubabeli na viongozi wa jamaa, nao wakasema, “Turuhusuni tuwasaidie kujenga, kwa sababu sisi tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu wakati wa Esar-Hadoni mfalme wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”
da kom de frem til Serubabel og til Øversterne for Fædrenehusene og sagde til dem: Lader os bygge med eder; thi vi ville søge eders Gud, ligesom I, og vi have ofret til ham fra de Dage af, da Kongen af Assyrien, Asar-Haddon, førte os hid op.
3 Lakini Zerubabeli, Yeshua na viongozi wengine wa jamaa ya Israeli wakawajibu, “Ninyi hamna sehemu nasi katika kujenga Hekalu la Mungu wetu. Sisi peke yetu tutajenga Hekalu kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli, kama Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi alivyotuagiza.”
Men Serubabel og Jesua og de øvrige af Øversterne for Fædrenehusene for Israel sagde til dem: Det sømmer sig ikke, at I og vi bygge vor Guds Hus; men vi ville alene bygge for Herren, Israels Gud, som Kong Kyrus, Kongen af Persien, bød os.
4 Ndipo watu waliowazunguka wakajipanga kuwakatisha tamaa watu wa Yuda na kuwafanya waogope walipokuwa wakiendelea na ujenzi.
Og Folket i Landet gjorde, at Judas Folk lode Hænderne synke, og de forstyrrede dem i at bygge.
5 Wakaajiri washauri kuwapinga katika kazi yao, nao wakaipinga mipango yao wakati wote wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi hadi wakati wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
Og de tingede Raadgivere imod dem for at gøre deres Raad til intet i alle Kyrus's, Kongen af Persiens, Dage, og indtil Darius's, Kongen af Persiens, Regering.
6 Mnamo mwanzo wa utawala wa Ahasuero, hao adui waliandika mashtaka dhidi ya watu wa Yuda na Yerusalemu.
Og i Ahasverus's Regering, i hans Regerings Begyndelse, skreve de en Klage imod Indbyggerne i Juda og Jerusalem.
7 Pia katika siku za utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli pamoja na wenzao waliandika barua kwa Artashasta. Barua hiyo iliandikwa kwa mwandiko wa Kiaramu na katika lugha ya Kiaramu.
Og i Artakserkses's Dage skreve Bislam, Mithridates, Tabeel og de øvrige af hans Selskab til Artakserkses, Kongen i Persien, og Brevet var skrevet med syrisk Skrift og oversat paa Syrisk.
8 Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai waliandika barua kwa Mfalme Artashasta dhidi ya watu wa Yerusalemu kama ifuatavyo:
Rehum, Kansleren og Simsaj, Skriveren, skreve et Brev imod Jerusalem til Kong Artakserkses, saalydende:
9 Rehumu afisa msimamizi na mwandishi Shimshai, pamoja na wenzao, yaani mahakimu na maafisa walio juu ya watu kuanzia Tripoli, Uajemi, Ereki na Babeli, Waelami wa Shushani,
— Dengang var det, Rehum, Kansleren, og Simsaj, Skriveren, og de øvrige af deres Selskab, de af Dina og Afarsathka, Tarpela, Afarsa, Erek, Babel, Susan, Dehava, Elam
10 na watu wengine ambao mheshimiwa Asur-Banipali aliwahamisha na kuwakalisha katika mji wa Samaria na mahali pengine Ngʼambo ya Mto Frati.
og de øvrige Folk, som den store og navnkundige Osnappar forflyttede og satte i Samarias Stad, og de øvrige paa denne Side Floden, og saa videre. —
11 (Hii ndiyo nakala ya barua waliyompelekea.) Kwa Mfalme Artashasta, Kutoka kwa watumishi wako, watu wa Ngʼambo ya Mto Frati:
Dette er Afskriften af Brevet, som de sendte til ham, til Kong Artakserkses: Dine Tjenere, de Mænd paa denne Side Floden, og saa videre:
12 Yapasa Mfalme ajue kuwa Wayahudi waliopanda kuja kwetu kutoka kwenu, wamekwenda Yerusalemu nao wanaujenga upya ule mji wa uasi na uovu. Wanajenga kuta upya na kukarabati misingi yake.
Det skal være Kongen vitterligt, at Jøderne, som ere dragne op fra dig, ere komne til os til Jerusalem og bygge den oprørske og onde Stad og fuldføre Muren og udbedre Grunden,
13 Zaidi ya hayo, mfalme yampasa ajue kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikafanywa upya, hakutakuwa na ulipaji wa kodi wala ada au ushuru, hivyo hazina za mfalme zitaathirika.
Saa være det nu Kongen vitterligt, at dersom den Stad bliver bygget, og Murene blive fuldførte, da skulle de ikke ville give dig Skat, Told og aarlig Rente, og du skal lide Tab i Kongernes Indtægt.
14 Sisi sasa kwa kuwa tunawajibika kwa jumba la kifalme na kwamba siyo sawasawa kwetu kuona mfalme akidharauliwa, basi tunatuma ujumbe huu kumtaarifu mfalme,
Nu, efterdi vi have vor Løn fra Kongens Palads, og det ikke sømmer sig, at vi se paa Kongens Skade, derfor have vi sendt hen og lade Kongen det vide,
15 ili kwamba ufanyike uchunguzi kwenye kumbukumbu ya maandishi ya waliokutangulia. Katika kumbukumbu hizi utagundua kwamba mji huu ni wa maasi, unaowataabisha wafalme na majimbo, ni mahali pa maasi tangu zamani. Ndiyo maana mji huu uliharibiwa.
at man maa lede i dine Fædres Historiebog, at du kan finde i samme Historiebog og forfare, at den Stad er en genstridig Stad og skadelig for Konger og Lande, og at de have gjort Opstand derudi fra gammel Tid af; derfor er Staden ødelagt.
16 Tunamjulisha mfalme kwamba kama mji huu ukijengwa na kuta zake zikifanywa upya, hutabakiwa na chochote Ngʼambo ya Mto Frati.
Vi give Kongen til Kende, at hvis denne Stad bliver bygget og dens Mure fuldførte, da beholder du ingen Del paa denne Side Floden.
17 Mfalme alirudisha jibu hili: Kwa Rehumu, afisa msimamizi, mwandishi Shimshai na wenzenu wote wanaoishi katika Samaria na penginepo Ngʼambo ya Mto Frati: Salamu.
Kongen sendte Svar til Rehum, Kansleren, og Simsaj, Skriveren, og de øvrige af deres Selskab, som boede i Samaria, og til de øvrige paa denne Side Floden: Fred! og saa videre:
18 Barua mliyotutumia imesomwa na kutafsiriwa mbele yangu.
Det Brev, som I sendte til os, er klarlig læst for mig,
19 Nilitoa amri na uchunguzi ukafanyika na imegundulika kwamba mji huu una historia ndefu ya maasi dhidi ya wafalme na pamekuwa mahali pa maasi na uchochezi.
og der er af mig given Befaling, at man skulde lede, og man har fundet, at denne Stad har fra gammel Tid af sat sig op imod Konger, og at der er gjort Opstand og Frafald derudi.
20 Yerusalemu umepata kuwa na wafalme wenye nguvu wakitawala nchi yote iliyo Ngʼambo ya Mto Frati, wakitoza kodi, ada na ushuru huko.
Og der har været mægtige Konger i Jerusalem, som have hersket over alt det, som er paa hin Side Floden, saa at dem blev given Skat, Told og aarlig Rente.
21 Kwa hiyo toeni amri kwa watu hawa wasimamishe ujenzi, ili kwamba mji huu usiendelee kujengwa hadi nitakapoagiza.
Saa giver nu Befaling om at forhindre disse Mænd, at den Stad ikke bliver bygget, førend der bliver givet Befaling af mig.
22 Mwe waangalifu msipuuze jambo hili. Kwa nini kuruhusu tishio hili kuendelea na kusababisha hasara kwa ufalme?
Saa værer paamindede, at I ikke begaa en Forseelse herudi; hvorfor skal det fordærvelige faa Overhaand, Kongerne til Skade?
23 Mara waliposomewa nakala ya barua ya Mfalme Artashasta, Rehumu na Shimshai aliyekuwa mwandishi na wenzao, walikwenda mara moja kwa Wayahudi huko Yerusalemu na kuwalazimisha kwa nguvu kusimamisha ujenzi.
Der nu Afskriften af Kong Artakserkses's Brev blev læst for Rehum af Simsaj, Skriveren, og deres Selskab, da droge de hastelig til Jerusalem til Jøderne og forhindrede dem med Arm og Magt.
24 Hivyo kazi ya ujenzi wa nyumba ya Mungu huko Yerusalemu ikasimamishwa kabisa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dario mfalme wa Uajemi.
Da forhindredes Arbejdet paa Guds Hus, som var i Jerusalem, og det blev forhindret indtil Darius's, Kongen i Persiens, andet Regeringsaar.