< Ezra 3 >

1 Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
İsrailliler kendi kentlerine yerleştikten sonra, yedinci ay Yeruşalim'de tek vücut halinde toplandılar.
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu.
Yosadak oğlu Yeşu ve kâhin olan kardeşleri, Şealtiel oğlu Zerubbabil'le kardeşleri İsrail'in Tanrısı'nın sunağını yeniden kurdular. Amaçları, Tanrı adamı Musa'nın yasası uyarınca, sunağın üzerinde yakmalık sunular sunmaktı.
3 Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni.
Çevrelerinde yaşayan halklardan korkmalarına karşın, sunağı eski temeli üzerine yeniden kurdular. Üzerinde RAB'be sabah, akşam öngörülen yakmalık sunuları sundular.
4 Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
Sonra yazılanlara uygun biçimde Çardak Bayramı'nı kutladılar. Kural uyarınca, her gün için belirlenen sayıya göre, yakmalık sunuları sundular.
5 Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana.
Bundan sonra da günlük yakmalık sunuyu, Yeni Ay sunularını, RAB'bin belirlediği bütün kutsal bayramların sunularını ve RAB'be gönülden verilen sunuları sundular.
6 Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
RAB'bin Tapınağı'nın temeli henüz atılmadığı halde, yedinci ayın birinci günü RAB'be yakmalık sunular sunmaya başladılar.
7 Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
İsrailliler taşçılarla marangozlara para ödediler. Ayrıca sedir tomruklarını Lübnan'dan denize indirerek Yafa'ya getirmeleri için Saydalılar'a ve Surlular'a yiyecek, içecek, zeytinyağı sağladılar. Bütün bunlara Pers Kralı Koreş izin vermişti.
8 Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
Tanrı'nın Yeruşalim'deki Tapınağı'na vardıktan sonra, ikinci yılın ikinci ayında Şealtiel oğlu Zerubbabil, Yosadak oğlu Yeşu ve bütün öteki kardeşleri, kâhinler, Levililer ve sürgünden Yeruşalim'e dönenlerin tümü işe başladılar. RAB'bin Tapınağı'nın yapımını denetlemek için yirmi ve daha yukarı yaştaki Levililer'i görevlendirdiler.
9 Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
Levililer'den Yeşu, oğulları ve kardeşleri, Yahuda soyundan Kadmiel ile oğulları, Henadat'ın oğullarıyla torunları Tanrı'nın Tapınağı'nın yapımında çalışanları denetleme işini hep birlikte yüklendiler.
10 Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
Yapıcılar RAB'bin Tapınağı'nın temelini atınca, İsrail Kralı Davut'un kuralı uyarınca kâhinler RAB'bi övmek için tören giysilerini giymiş olarak ellerinde borazanlarla, Levili Asafoğulları da zillerle yerlerini aldılar.
11 Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa.
RAB'be övgüler, şükranlar sunarak ezgi okudular: “RAB iyidir; İsrail'e sevgisi sonsuzdur.” RAB'bin Tapınağı'nın temeli atıldığı için herkes yüksek sesle RAB'bi övmeye başladı.
12 Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
Eski tapınağı görmüş birçok yaşlı kâhin, Levili ve boy başı tapınağın temelinin atıldığını görünce hıçkıra hıçkıra ağladılar. Birçokları da sevinç çığlıkları attı.
13 Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.
Sevinç çığlıkları ağlama sesinden ayırt edilemiyordu. Çünkü halk avaz avaz bağırıyordu. Ses uzak yerlerden bile duyuluyordu.

< Ezra 3 >