< Ezra 3 >
1 Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
Et l'on touchait au septième mois, et les enfants d'Israël étaient dans [leurs] villes, et le peuple se rassembla comme un seul homme à Jérusalem.
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu.
Alors se levèrent Jésuah, fils de Jotsadac, et ses frères, les Prêtres, et Zorobabel, fils de Sealthiel, et ses frères, et ils bâtirent l'autel du Dieu d'Israël pour y offrir des holocaustes aux termes du texte de la Loi de Moïse, l'homme de Dieu.
3 Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni.
Et ils assirent l'autel sur ses fondements, parce qu'ils étaient sous la terreur que leur donnaient les peuples des pays [voisins], et ils y offrirent des holocaustes à l'Éternel, les holocaustes du matin et du soir.
4 Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
Et ils firent la fête des Loges aux termes du texte écrit, et offrirent jour par jour des holocaustes, selon le nombre voulu et le rite, l'ordinaire de chaque jour,
5 Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana.
et après cela les holocaustes perpétuels et ceux des nouvelles lunes et de toutes les solennités consacrées de l'Éternel, et pour tous ceux qui faisaient à l'Éternel des offrandes spontanées.
6 Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
A partir du premier jour du septième mois ils commencèrent à sacrifier les holocaustes à l'Éternel. Cependant les fondements du Temple de l'Éternel n'étaient point encore posés.
7 Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
Et ils donnèrent de l'argent aux tailleurs de pierre et aux charpentiers, et des vivres et des boissons et de l'huile aux Sidoniens et aux Tyriens pour qu'ils leur amenassent du bois de cèdre du Liban par mer à Joppe, selon l'autorisation qu'ils avaient reçue de Cyrus, roi de Perse.
8 Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
Et la seconde année depuis leur retour à la Maison de Dieu à Jérusalem, au second mois, commencèrent Zorobabel, fils de Sealthiel, et Jésuah, fils de Jotsadac, et le reste de leurs frères, les Prêtres et les Lévites et tous ceux qui de la captivité étaient revenus à Jérusalem, et ils établirent les Lévites de vingt ans et au-dessus pour présider à la bâtisse de la Maison de l'Éternel.
9 Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
Et Jésuah, ses fils et ses frères, Cadmiel et ses fils, fils de Juda, furent à leur poste comme un seul homme pour surveiller les ouvriers occupés à la maison de Dieu; [de même] les fils de Hènadad, leurs fils et leurs frères, les Lévites.
10 Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
Et lorsque les constructeurs posaient les fondements du Temple de l'Éternel, les Prêtres en costume portaient présence, avec des trompettes, ainsi que les Lévites, fils d'Asaph, avec des cymbales pour louer l'Éternel selon le mode de David, roi d'Israël.
11 Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa.
Et ils se répondaient en chantant, et en louant l'Éternel de ce qu'il est bon, et sa miséricorde éternelle envers Israël. Et tout le peuple acclama par une puissante acclamation à la louange de l'Éternel, la fondation de la Maison de l'Éternel.
12 Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
Mais plusieurs des Prêtres et des Lévites, et des chefs des maisons patriarcales, vieillards qui avaient vu la première Maison dans sa structure, quand cette maison fut devant leurs yeux, se mirent à pleurer à grand bruit; d'un autre côté plusieurs élevaient la voix en cris de joie.
13 Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.
Et le peuple ne pouvait distinguer entre le bruit des acclamations de joie et le bruit des pleurs dans le peuple; car le peuple poussait une immense clameur dont le bruit s'entendait au loin.