< Ezra 3 >

1 Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
And thanne the seuenthe monethe was comun, and the sones of Israel weren in her citees.
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu.
Therfor the puple was gaderid as o man in to Jerusalem. And Josue, the sone of Josedech, roos, and hise britheren, prestis, and Zorobabel, the sone of Salatiel, and hise britheren, and thei bildiden the auter of God of Israel for to offre therynne brent sacrifices, as it is writun in the lawe of Moises, the man of God.
3 Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni.
Forsothe thei settiden the auter on his foundementis, while the puplis of londis bi cumpas maden hem aferd, and thei offriden on that auter brent sacrifice to the Lord in the morewtid and euentid.
4 Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
And thei maden solempnytee of tabernaclis, as it is writun, and brent sacrifice ech dai bi ordre, `bi the werk of the dai comaundid in his dai.
5 Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana.
And after this thei offriden contynuel brent sacrifice, bothe in calendis and in alle solempnytees of the Lord, that weren halewid, and in alle solempnytees, in which yifte was offrid to the Lord bi fre wille.
6 Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
In the firste dai of the seuenthe monethe thei bigunnen to offre brent sacrifice to the Lord; certis the temple of God was not foundid yit.
7 Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
But thei yauen monei to heweris of stoon, and to liggeris of stoon, and thei yauen mete, and drynke, and oile, to men of Sidon, and `to men of Tire, that thei schulden brynge cedre trees fro the Liban to the see of Joppe, bi that that Cirus, kyng of Persis, hadde comaundid to hem.
8 Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
Forsothe in the secounde yeer of her comyng to the temple of God in Jerusalem, in the secounde monethe, Zorobabel, the sone of Salatiel, and Josue,
9 Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
the sone of Josedech, and othere of her britheren, preestis and dekenes, and alle that camen fro the caitifte in to Jerusalem, bigunnen; and thei ordeyneden dekenes, fro twenti yeer and aboue, for to haste the werk of the Lord; and Josue stood, and hise sones, and hise britheren, Cedynyel and hise sones, and the sones of Juda, as o man, to be bisi ouer hem that maden the werk in the temple of God; the sones of Benadab, her sones and her britheren, dekenes, `weren bisy.
10 Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
Therfor whanne the temple `of the Lord was foundid of stoon leggeris, prestis stoden in her ournement with trumpis, and dekenes, the sones of Asaph, in cymbalis, for to herie God bi the hond of Dauid, kyng of Israel.
11 Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa.
And thei sungen togidere in ympnes and knoulechyng to the Lord, For he is good, for his merci is with outen ende on Israel. And al the puple criede with greet cry, in preisynge the Lord, for the temple of the Lord was foundid.
12 Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
Also ful manye of the preestis, and of the dekenes, and the princes of fadris, and the eldre men, that hadden seyn the formere temple, whanne it was foundid, and this temple bifor her iyen, wepten with greet vois, and many men criynge in gladnesse reisiden the vois;
13 Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.
and no man myyte knowe the vois of cry of men beynge glad, and the vois of wepyng of the puple; for the puple criede togidere with greet cry, and the vois was herd afer.

< Ezra 3 >