< Ezra 3 >

1 Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
and to touch [the] month [the] seventh and son: descendant/people Israel in/on/with city and to gather [the] people like/as man one to(wards) Jerusalem
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu.
and to arise: rise Jeshua son: child Jozadak and brother: compatriot his [the] priest and Zerubbabel son: child Shealtiel and brother: male-relative his and to build [obj] altar God Israel to/for to ascend: offer up upon him burnt offering like/as to write in/on/with instruction Moses man [the] God
3 Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni.
and to establish: establish [the] altar upon base his for in/on/with terror upon them from people [the] land: country/planet (and to ascend: offer up *Q(K)*) upon him burnt offering to/for LORD burnt offering to/for morning and to/for evening
4 Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
and to make: do [obj] feast [the] booth like/as to write and burnt offering day: daily in/on/with day: daily in/on/with number like/as justice: judgement word: portion day: daily in/on/with day: daily his
5 Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana.
and after so burnt offering continually and to/for month: new moon and to/for all meeting: festival LORD [the] to consecrate: consecate and to/for all be willing voluntariness to/for LORD
6 Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
from day one to/for month [the] seventh to profane/begin: begin to/for to ascend: offer up burnt offering to/for LORD and temple LORD not to found
7 Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
and to give: give silver: money to/for to hew and to/for artificer and food and feast and oil to/for Sidonian and to/for Tyrian to/for to come (in): bring tree cedar from [the] Lebanon to(wards) sea Joppa like/as permission Cyrus king Persia upon them
8 Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
and in/on/with year [the] second to/for to come (in): come them to(wards) house: temple [the] God to/for Jerusalem in/on/with month [the] second to profane/begin: begin Zerubbabel son: child Shealtiel and Jeshua son: child Jozadak and remnant brother: male-relative their [the] priest and [the] Levi and all [the] to come (in): come from [the] captivity Jerusalem and to stand: appoint [obj] [the] Levi from son: aged twenty year and above [to] to/for to conduct upon work house: temple LORD
9 Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
and to stand: appoint Jeshua son: child his and brother: male-sibling his Kadmiel and son: child his son: child Judah like/as one to/for to conduct upon to make: [do] [the] work in/on/with house: temple [the] God son: child Henadad son: child their and brother: male-sibling their [the] Levi
10 Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
and to found [the] to build [obj] temple LORD and to stand: appoint [the] priest to clothe in/on/with trumpet and [the] Levi son: descendant/people Asaph in/on/with cymbal to/for to boast: praise [obj] LORD upon hand: power David king Israel
11 Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa.
and to sing in/on/with to boast: praise and in/on/with to give thanks to/for LORD for pleasant for to/for forever: enduring kindness his upon Israel and all [the] people to shout (shout *LB(ah)*) great: large in/on/with to boast: praise to/for LORD upon to found house: temple LORD
12 Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
and many from [the] priest and [the] Levi and head: leader [the] father [the] old which to see: see [obj] [the] house: temple [the] first in/on/with to found him this [the] house: temple in/on/with eye: seeing their to weep in/on/with voice great: large and many in/on/with shout in/on/with joy to/for to exalt voice
13 Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.
and nothing [the] people to recognize voice: sound shout [the] joy to/for voice: sound weeping [the] people for [the] people to shout shout great: large and [the] voice: sound to hear: hear till to/for from distant

< Ezra 3 >