< Ezra 2 >

1 Basi hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
Now these are the sons of the province who went up out of the captivity of those who had been carried away, whom Nebuchadnezzar the king of Babylon had carried away to Babylon, and who returned to Jerusalem and Judah, every man to his city,
2 wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana): Orodha ya wanaume kati ya watu wa Israeli ilikuwa:
who came with Zerubbabel, Jeshua, Nehemiah, Seraiah, Reelaiah, Mordecai, Bilshan, Mispar, Bigvai, Rehum, Baanah. The number of the men of the people of Israel:
3 wazao wa Paroshi 2,172
The sons of Parosh, two thousand a hundred seventy-two.
4 wazao wa Shefatia 372
The sons of Shephatiah, three hundred seventy-two.
5 wazao wa Ara 775
The sons of Arah, seven hundred seventy-five.
6 wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,812
The sons of Pahath-moab, of the sons of Jeshua and Joab, two thousand eight hundred and twelve.
7 wazao wa Elamu 1,254
The sons of Elam, a thousand two hundred fifty-four.
8 wazao wa Zatu 945
The sons of Zattu, nine hundred forty-five.
9 wazao wa Zakai 760
The sons of Zaccai, seven hundred and sixty.
10 wazao wa Bani 642
The sons of Bani, six hundred forty-two.
11 wazao wa Bebai 623
The sons of Bebai, six hundred twenty-three.
12 wazao wa Azgadi 1,222
The sons of Azgad, a thousand two hundred twenty-two.
13 wazao wa Adonikamu 666
The sons of Adonikam, six hundred sixty-six.
14 wazao wa Bigwai 2,056
The sons of Bigvai, two thousand fifty-six.
15 wazao wa Adini 454
The sons of Adin, four hundred fifty-four.
16 wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
The sons of Ater, of Hezekiah, ninety-eight.
17 wazao wa Besai 323
The sons of Bezai, three hundred twenty-three.
18 wazao wa Yora 112
The sons of Jorah, a hundred and twelve.
19 wazao wa Hashumu 223
The sons of Hashum, two hundred twenty-three.
20 wazao wa Gibari 95
The sons of Gibbar, ninety-five.
21 watu wa Bethlehemu 123
The sons of Bethlehem, a hundred twenty-three.
22 watu wa Netofa 56
The men of Netophah, fifty-six.
23 watu wa Anathothi 128
The men of Anathoth, a hundred twenty-eight.
24 watu wa Azmawethi 42
The sons of Azmaveth, forty-two.
25 wazao wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
The sons of Kiriath-arim, Chephirah, and Beeroth, seven hundred and forty-three.
26 wazao wa Rama na Geba 621
The sons of Ramah and Geba, six hundred twenty-one.
27 watu wa Mikmashi 122
The men of Michmas, a hundred twenty-two.
28 watu wa Betheli na Ai 223
The men of Bethel and Ai, two hundred twenty-three.
29 wazao wa Nebo 52
The sons of Nebo, fifty-two.
30 wazao wa Magbishi 156
The sons of Magbish, a hundred fifty-six.
31 wazao wa Elamu ile ingine 1,254
The sons of the other Elam, a thousand two hundred fifty-four.
32 wazao wa Harimu 320
The sons of Harim, three hundred and twenty.
33 wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 725
The sons of Lod, Hadid, and Ono, seven hundred twenty-five.
34 wazao wa Yeriko 345
The sons of Jericho, three hundred forty-five.
35 wazao wa Senaa 3,630
The sons of Senaah, three thousand and six hundred and thirty.
36 Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
The priests: the sons of Jedaiah, of the house of Jeshua, nine hundred seventy-three.
37 wazao wa Imeri 1,052
The sons of Immer, a thousand fifty-two.
38 wazao wa Pashuri 1,247
The sons of Pashhur, a thousand two hundred forty-seven.
39 wazao wa Harimu 1,017
The sons of Harim, a thousand and seventeen.
40 Walawi: wazao wa Yeshua na Kadmieli (kupitia jamaa ya Hodavia) 74
The Levites: the sons of Jeshua and Kadmiel, of the sons of Hodaviah, seventy-four.
41 Waimbaji: wazao wa Asafu 128
The singers: the sons of Asaph, a hundred twenty-eight.
42 Mabawabu wa lango la Hekalu: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 139
The sons of the porters: the sons of Shallum, the sons of Ater, the sons of Talmon, the sons of Akkub, the sons of Hatita, the sons of Shobai, in all a hundred thirty-nine.
43 Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
The Nethinim: the sons of Ziha, the sons of Hasupha, the sons of Tabbaoth,
44 wazao wa Kerosi, Siaha, Padoni,
the sons of Keros, the sons of Siaha, the sons of Padon,
45 wazao wa Lebana, Hagaba, Akubu,
the sons of Lebanah, the sons of Hagabah, the sons of Akkub,
46 wazao wa Hagabu, Shalmai, Hanani,
the sons of Hagab, the sons of Shamlai, the sons of Hanan,
47 wazao wa Gideli, Gahari, Reaya,
the sons of Giddel, the sons of Gahar, the sons of Reaiah,
48 wazao wa Resini, Nekoda, Gazamu,
the sons of Rezin, the sons of Nekoda, the sons of Gazzam,
49 wazao wa Uza, Pasea, Besai,
the sons of Uzza, the sons of Paseah, the sons of Besai,
50 wazao wa Asna, Meunimu, Nefusimu,
the sons of Asnah, the sons of Meunim, the sons of Nephisim,
51 wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
the sons of Bakbuk, the sons of Hakupha, the sons of Harhur,
52 wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
the sons of Bazluth, the sons of Mehida, the sons of Harsha,
53 wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
the sons of Barkos, the sons of Sisera, the sons of Temah,
54 wazao wa Nesia na Hatifa.
the sons of Neziah, the sons of Hatipha.
55 Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Hasaferethi, Peruda,
The sons of Solomon's servants: the sons of Sotai, the sons of Hassophereth, the sons of Peruda,
56 wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
the sons of Jaalah, the sons of Darkon, the sons of Giddel,
57 wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Ami.
the sons of Shephatiah, the sons of Hattil, the sons of Pochereth-hazzebaim, the sons of Ami.
58 Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
All the Nethinim and the sons of Solomon's servants were three hundred ninety-two.
59 Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
And these were those who went up from Tel-melah, Tel-harsha, Cherub, Addan, and Immer, but they could not show their fathers' houses, and their seed, whether they were of Israel:
60 wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 652
the sons of Delaiah, the sons of Tobiah, the sons of Nekoda, six hundred fifty and two.
61 Kutoka miongoni mwa makuhani: Wazao wa Hobaya, Hakosi, Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
And of the sons of the priests: the sons of Habaiah, the sons of Hakkoz, the sons of Barzillai who took a wife of the daughters of Barzillai the Gileadite, and was called after their name.
62 Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
These sought their registration among those that were reckoned by genealogy, but they were not found. Therefore they were deemed polluted and put away from the priesthood.
63 Mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
And the governor said to them that they should not eat of the most holy things till there stood up a priest with Urim and with Thummim.
64 Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
The whole assembly together was forty-two thousand three hundred and sixty,
65 tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 200.
besides their men-servants and their maid-servants, of whom there were seven thousand three hundred thirty-seven. And they had two hundred singing men and singing women.
66 Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,
Their horses were seven hundred thirty-six, their mules, two hundred forty-five,
67 ngamia 435 na punda 6,720.
their camels, four hundred thirty-five, their donkeys, six thousand seven hundred and twenty.
68 Walipofika kwenye nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika eneo lake.
And some of the heads of fathers, when they came to the house of Jehovah which is in Jerusalem, offered willingly for the house of God to set it up in its place.
69 Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000 za dhahabu, mane 5,000 za fedha, na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hiyo.
They gave after their ability into the treasury of the work sixty-one thousand darics of gold, and five thousand pounds of silver, and one hundred priests' garments.
70 Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na watumishi wa Hekalu waliishi katika miji yao wenyewe, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao.
So the priests, and the Levites, and some of the people, and the singers, and the porters, and the Nethinim, dwelt in their cities, and all Israel in their cities.

< Ezra 2 >