< Ezra 10 >

1 Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana.
Då Esra så bad, bekände och gret, och låg inför Guds hus, församlade sig till honom utaf Israel en ganska stor menighet af män, qvinnor och barn; förty folket gret svårliga.
2 Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli.
Och Sechania, Jehiels son, af Elams barn, svarade, och sade till Esra: Si, vi hafve förtagit oss emot vår Gud, att vi hafve tagit oss främmande hustrur utaf landsens folk; men här är ännu hopp derom i Israel.
3 Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria.
Så låt oss nu göra ett förbund med vårom Gud, så att vi utdrifve alla hustrur, och dem som af dem födde äro, efter Herrans råd, och deras som frukta vår Guds bud, att man må göra efter lagen.
4 Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”
Så statt nu upp; ty det hörer dig till: Vi vilje vara med dig; var vid en god tröst, och gör så.
5 Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa.
Då stod Esra upp, och tog en ed af de öfversta Presterna, och Leviterna, och hela Israel, att de skulle göra efter detta talet. Och de svoro det.
6 Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.
Och Esra stod upp inför Guds hus, och gick in uti Johanans, Eljasibs sons, kammar. Och då han ditkom, åt han intet bröd, och drack intet vatten; förty han sörjde öfver deras öfverträdelse, som i fängelset varit hade.
7 Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu.
Och de läto utropa i Juda och Jerusalem, till all fängelsens barn, att de skulle församla sig till Jerusalem.
8 Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.
Och hvilken som icke komme innan tre dagar, efter öfverstarnas och de äldstas råd, hans ägodelar skulle alla tillspillogifvas, och han afskiljas ifrå fångarnas menighet.
9 Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa.
Då församlade sig alle Juda män och BenJamin till Jerusalem, innan tre dagar; det är, på tjugonde dagen i den nionde månadenom. Och allt folket satt uppå gatone inför Guds hus, och bäfvade för detta ärendes skull, och för regnet.
10 Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli.
Och Esra Presten stod upp, och sade till dem: I hafven förtagit eder, i det att I hafven tagit främmande hustrur, på det I skullen ännu föröka Israels skuld.
11 Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”
Så bekänner nu Herran edra fäders Gud, och görer det honom ljuft är, och skiljer eder ifrå landsens folk, och ifrå de främmande hustrur.
12 Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema.
Då svarade hela menigheten, och sade med höga röst: Ske såsom du oss sagt hafver.
13 Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili.
Men folket är mycket, och regnväder, och kan icke stå ute; så är det icke heller ens eller två dagars gerning; ty vi hafve sådana öfverträdelse mycken gjort.
14 Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.”
Låt oss beställa våra öfverstar i hela menighetene, att alle de i våra städer, som främmande hustrur tagit hafva, komma på bestämd tid; och de äldste i hvar staden, och deras domare med, tilldess vår Guds vrede må ifrån oss vänd varda i denna sakene.
15 Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.
Då vordo beställde Jonathan, Asahels son, och Jahesia, Thikva son, öfver denna saken; och Mesullam, och Sabbethai Leviterna hulpo dem.
16 Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo.
Och fängelsens barn gjorde alltså. Och Presten Esra, och de ypperste fäderne i deras fäders hus, och alle de nu nämnde äro, afskiljde sig, och satte sig på första dagen i tionde månadenom till att ransaka om detta ärendet.
17 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.
Och de uträttade det på alla de män, som främmande hustrur hade, på första dagen i första månadenom.
18 Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni: Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.
Och vordo funne ibland Presternas barn, som främmande hustrur tagit hade, nämliga ibland Jesua barn, Jozadaks sons, och hans bröder: Maaseja, Elieser, Jarib och Gedalia.
19 (Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)
Och de gåfvo deras hand deruppå, att de ville utdrifva hustrurna; och till deras skuldoffer offra en vädur för sina skuld.
20 Kutoka wazao wa Imeri: Hanani na Zebadia.
Ibland Immers barn: Hanani och Sebadia.
21 Kutoka wazao wa Harimu: Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.
Ibland Harims barn: Maaseja, Elia, Semaja, Jehiel och Ussia.
22 Kutoka wazao wa Pashuri: Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.
Ibland Pashurs barn: Eljoenai, Maaseja, Ismael, Nethaneel, Josabad och Eleasa.
23 Miongoni mwa Walawi: Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.
Ibland Leviterna: Josabad, Simei och Kelaja, den är Kelita; Pethabja, Juda och Elieser.
24 Kutoka waimbaji: Eliashibu. Kutoka mabawabu: Shalumu, Telemu na Uri.
Ibland sångarena: Eljasib. Ibland dörravaktarena: Sallum, Telem och Uri.
25 Miongoni mwa Waisraeli wengine: Kutoka wazao wa Paroshi: Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.
Utaf Israel: Ibland Paros barn: Ramia, Jissija, Malchija, Mijamin, Eleazar, Malchija och Benaja.
26 Kutoka wazao wa Elamu: Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.
Ibland Elams barn: Mattania, Zacharia, Jehiel, Abdi, Jeremoth och Elia.
27 Kutoka wazao wa Zatu: Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.
Ibland Sattu barn: Eljoenai, Eljasib, Mattania, Jeremoth, Sabad och Asisa.
28 Kutoka uzao wa Bebai: Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.
Ibland Bebai barn: Johanan, Hanania, Sabbai och Athlai.
29 Kutoka wazao wa Bani: Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.
Ibland Bani barn: Mesullam, Malluch, Adaja, Jasub, Seal och Jeramoth.
30 Kutoka wazao wa Pahath-Moabu: Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.
Ibland PahathMoabs barn: Adna, Chelal, Benaja, Maaseja, Mattania, Bezaleel, Binnui och Manasse.
31 Kutoka wazao wa Harimu: Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni,
Ibland Harims barn: Elieser, Jissija, Malchija, Semaja, Simeon,
32 Benyamini, Maluki, na Shemaria.
BenJamin, Malluch och Semaria.
33 Kutoka wazao wa Hashumu: Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.
Ibland Hasums barn: Mattenai, Mattatta, Sabad, Elipheleth, Jeremai, Manasse och Simi.
34 Kutoka wazao wa Bani: Maadai, Amramu, Ueli,
Ibland Bani barn: Maadai, Amram, Uel,
35 Benaya, Bedeya, Keluhi,
Benaja, Bedja, Cheluhu,
36 Vania, Meremothi, Eliashibu,
Banja, Meremoth, Eljasib,
37 Matania, Matenai na Yaasu.
Mattania, Mattenai, Jaasav,
38 Kutoka wazao wa Binui: Shimei,
Bani, Binnui, Simi,
39 Shelemia, Nathani, Adaya,
Selemia, Nathan, Adaja,
40 Maknadebai, Shashai, Sharai,
Machnadbai, Sasai, Sarai,
41 Azareli, Shelemia, Shemaria,
Asareel, Selemia, Semaria,
42 Shalumu, Amaria na Yosefu.
Sallum, Amaria och Joseph.
43 Kutoka wazao wa Nebo: Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.
Ibland Nebo barn: Jegiel, Mattithia, Sabad, Sebina, Jaddai, Joel och Benaja.
44 Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.
Desse hade alle tagit främmande hustrur; och voro somlige ibland de samma hustrur, som barn födt hade.

< Ezra 10 >