< Ezra 10 >

1 Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana.
Et comme Esdras priait et faisait la confession, pleurant et prosterné devant la Maison de Dieu, il se forma vers lui une assemblée très nombreuse d'Israélites, hommes, femmes et enfants; car le peuple versait d'abondantes larmes.
2 Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli.
Alors prit la parole Sechania, fils de Jehiel, des fils d'Eilam, et il dit à Esdras: Nous avons forfait contre notre Dieu en épousant des femmes étrangères des peuples de la terre, néanmoins il y a encore espoir pour Israël à cet égard.
3 Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria.
A présent nous voulons faire un pacte avec notre Dieu pour le renvoi de toutes ces femmes et de ce qui est né d'elles, — sur le conseil de monseigneur [Esdras] et de ceux qui révèrent les commandements de notre Dieu, afin qu'il soit fait selon la Loi.
4 Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”
Lève-toi! à toi l'affaire! et nous serons de ton côté. Courage! et agis!
5 Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa.
Alors Esdras se leva et fit jurer aux chefs des Prêtres, des Lévites et de tout Israël d'agir dans ce sens. Et ils prêtèrent le serment.
6 Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.
Et Esdras se leva de devant la Maison de Dieu, et se rendit dans la cellule de Jochanan, fils d'Eliasib, et il y alla et ne mangea point de pain et ne but point d'eau, parce qu'il était en deuil à cause du forfait des captifs.
7 Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu.
Et ils firent circuler en Juda et à Jérusalem la citation pour tous les fils de la captivité de se rassembler à Jérusalem.
8 Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.
Quant à celui qui ne paraîtrait pas dans l'espace de trois jours, selon le conseil des chefs et des Anciens, tous ses biens seraient confisqués et lui-même éliminé du corps des captifs.
9 Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa.
Alors tous les hommes de Juda et de Benjamin se rassemblèrent à Jérusalem dans l'espace de trois jours: c'était le neuvième mois, le vingtième du mois. Et tout le peuple prit séance dans la place de la Maison de Dieu, tremblant à cause de la question et à cause des pluies.
10 Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli.
Alors Esdras, le Prêtre, se leva et leur dit: Vous avez forfait en épousant des femmes étrangères, et avez ainsi ajouté à la culpabilité d'Israël.
11 Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”
Faites donc votre confession à l'Éternel, Dieu de vos pères, et exécutez sa volonté en vous séparant des peuples du pays et des femmes étrangères.
12 Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema.
Et toute l'Assemblée répondit et dit à voix forte: Oui, c'est comme tu nous le dis que nous devons agir!
13 Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili.
Mais le peuple est nombreux, et c'est la saison des pluies, et il n'y a pas moyen de rester en plein air, et ce n'est pas l'affaire d'un ni de deux jours; car nous avons abondamment manqué à cet égard.
14 Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.”
Que nos chefs soient donc les représentants de toute l'Assemblée; et tous ceux qui dans nos villes ont épousé des femmes étrangères, pourront venir à époques fixes, et avec eux les Anciens de chaque ville et ses Juges, jusqu'à ce que l'on ait détourné de nous la colère de notre Dieu, allumée pour cette raison.
15 Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.
Cependant Jonathan, fils de Hasahel, et Jahezia, fils de Thicva, firent opposition, et Mesullam et Sabthaï, le Lévite, les appuyèrent.
16 Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo.
Mais les fils de la captivité suivirent ce mode. Et l'on choisit Esdras, le Prêtre, et quelques-uns des chefs des maisons patriarcales, tous désignés par leurs noms.
17 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.
Et ils siégèrent le premier jour du dixième mois pour connaître de l'affaire. Et ils en finirent avec tous les hommes qui avaient épousé des femmes étrangères, le premier jour du premier mois.
18 Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni: Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.
Et parmi les fils de Prêtres qui avaient épousé des femmes étrangères, se trouvèrent des fils de Jésuah, fils de Jotsadac, et de ses frères, Mahaseïa et Éliézer et Jarib et Gedalia;
19 (Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)
et en donnant leur main ils s'engagèrent à renvoyer leurs femmes, et à offrir un bélier en sacrifice expiatoire pour leur faute;
20 Kutoka wazao wa Imeri: Hanani na Zebadia.
et des fils de Immer: Hanani et Zebadia;
21 Kutoka wazao wa Harimu: Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.
et des fils de Harim: Mahaseïa et Elia et Semaïa et Jehiel et Uzzia;
22 Kutoka wazao wa Pashuri: Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.
et des fils de Paschur: Elioénaï, Mahaseïa, Ismaël, Nathanaël, Jozabad et Eleasa;
23 Miongoni mwa Walawi: Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.
et des Lévites: Jozabad et Siméï et Kelaïa (c'est Kelita), Pethahia, Juda et Eliézer;
24 Kutoka waimbaji: Eliashibu. Kutoka mabawabu: Shalumu, Telemu na Uri.
et des Chantres: Eliasib; et des Portiers: Sallum et Télem et Uri;
25 Miongoni mwa Waisraeli wengine: Kutoka wazao wa Paroshi: Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.
et d'Israël, des fils de Paréos: Ramia et Jizzia et Malchiia et Mijamin et Eléazar et Malchiia et Benaïa;
26 Kutoka wazao wa Elamu: Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.
et des fils d'Eilam: Matthania, Zacharie et Jehiel et Abdi et Jerémoth et Elia;
27 Kutoka wazao wa Zatu: Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.
et des fils de Zatthu: Elioénaï, Eliasib, Matthania et Jerémoth et Zabad et Aziza;
28 Kutoka uzao wa Bebai: Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.
et des fils de Bébaï: Jochanan, Hanania, Zabbaï, Athlaï;
29 Kutoka wazao wa Bani: Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.
et des fils de Bani: Mesullam, Malluch et Adaïa, Jasub et Seal, Jeramoth;
30 Kutoka wazao wa Pahath-Moabu: Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.
et des fils de Pachath-Moab: Adna et Chelal, Benaïa, Mahaseïa, Matthania, Betsaleël et Binnuï et Manassé;
31 Kutoka wazao wa Harimu: Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni,
et des fils de Harim: Eliézer, Jissia, Malchia, Semaïa, Siméon,
32 Benyamini, Maluki, na Shemaria.
Benjamin, Malluch, Semaria;
33 Kutoka wazao wa Hashumu: Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.
des fils de Chasum: Mathnaï, Matthattha, Zabad, Eliphéleth, Jerémaï, Manassé, Siméï;
34 Kutoka wazao wa Bani: Maadai, Amramu, Ueli,
des fils de Bani: Maëdaï, Amram et Uel,
35 Benaya, Bedeya, Keluhi,
Benaïa, Bédia, Cheluhi;
36 Vania, Meremothi, Eliashibu,
et Naïa, Merémoth, Eliasib,
37 Matania, Matenai na Yaasu.
Matthania, Matthnaï et Jaësaï,
38 Kutoka wazao wa Binui: Shimei,
et Bani et Binnuï, Siméï
39 Shelemia, Nathani, Adaya,
et Sélémia et Nathan et Adaïa,
40 Maknadebai, Shashai, Sharai,
Machnadbaï, Sasaï, Saraï,
41 Azareli, Shelemia, Shemaria,
Azareël et Sélémia, Semaria,
42 Shalumu, Amaria na Yosefu.
Sallum, Amaria, Joseph;
43 Kutoka wazao wa Nebo: Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.
des fils de Nebo: Jehiel, Matthithia, Zabad, Zebina, Jaddaï et Joël, Benaïa.
44 Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.
Tous ceux-là avaient épousé des femmes étrangères, et il y en avait parmi ces femmes qui avaient apporté des fils.

< Ezra 10 >