< Ezra 10 >

1 Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana.
Et comme Esdras priait, et comme, en pleurant et priant, il élevait la voix devant le temple du Seigneur, la nombreuse Église d'Israël se rassembla auprès de lui, hommes, femmes et jeunes gens; et le peuple pleura, et en pleurant il éleva la voix.
2 Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli.
Et Sechénias, fils de Jehel, des fils d'Elam, prit la parole, et il dit à Esdras: Nous avons violé la loi de notre Dieu, et nous avons épousé parmi les peuples de la terre promise des femmes étrangères; et maintenant, après cela, Israël espère encore.
3 Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria.
Faisons donc alliance avec notre Dieu; et, s'il le veut, chassons toutes ces femmes et ceux qui sont nés d'elles. Lève-toi, inspire-leur la crainte des commandements de notre Dieu, et qu'il soit fait selon la loi.
4 Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”
Lève-toi, car l'affaire te regarde, et nous sommes avec toi; sois fort et agis.
5 Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa.
Et Esdras se leva, et il fit prêter serment aux chefs, aux prêtres, aux lévites, à tout Israël, d'exécuter ses ordres, et ils le jurèrent.
6 Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.
Et Esdras se leva de devant le temple, et il alla au trésor gardé par Johanan, fils d'Elisub, et il y entra, et il ne mangea pas de pain, et il ne but point d'eau, car il pleurait sur l'infidélité des fils de l'exil.
7 Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu.
Et l'on fit dans Juda et à Jérusalem une proclamation qui disait: Tous les fils de l'exil se réuniront à Jérusalem.
8 Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.
Quiconque ne viendra pas dans trois jours, selon l'ordre des princes et des prêtres, tous ses biens seront anathématisés, et lui-même sera expulsé de l'Église des fils de l'exil.
9 Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa.
Tous les hommes de Juda et de Benjamin se rendirent donc à Jérusalem. On était au neuvième mois; le vingtième jour du même mois, tout le peuple se tint sur la place du temple de Dieu, à cause du trouble né de cette affaire, et à cause d'une tempête.
10 Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli.
Et Esdras, le prêtre, se leva, et il leur dit: Vous avez violé l'alliance, et vous avez épousé des femmes étrangères, pour ajouter aux péchés d'Israël.
11 Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”
Rendez maintenant gloire au Seigneur Dieu de vos pères, et faites ce qui est agréable à ses yeux; séparez-vous des peuples de la terre promise, et des femmes des étrangers.
12 Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema.
Et toute l'Église s'écria: Grande est pour nous cette parole de toi que nous devons accomplir.
13 Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili.
Mais le peuple est nombreux, le temps est à l'orage, et il n'est pas possible de se tenir dehors plus longtemps; d'ailleurs, ce n'est point l'œuvre d'un ou de deux jours, car, à ce sujet, nous avons multiplié nos fautes.
14 Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.”
Que nos chefs restent, et qu'ils aillent, au temps prescrit, en toutes les villes, pour tous ceux qui ont épousé des femmes étrangères; que dans chaque ville ils s'adjoignent les anciens et les juges, afin de détourner de nous la colère du Seigneur notre Dieu, au sujet de ce péché.
15 Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.
Or, il n'y eut avec moi que Jonathas, fils d'Azaêl, et Jasias, fils de Thécoé, et ils eurent pour aides Mesollam, et Sabbathaï, le lévite.
16 Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo.
Et voici ce que firent les chefs de l'exil: le prêtre Esdras et les chefs de familles paternelles furent désignés tous nominativement, et ils partirent le premier jour du dixième mois pour faire des enquêtes sur cette affaire.
17 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.
Et, le premier jour du premier mois, ils eurent fini, et connurent tous les hommes qui avaient épousé des femmes étrangères.
18 Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni: Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.
Et parmi eux furent trouvés des fils de prêtres nés de Josué, fils de Josédec et ses frères, savoir: Maasia, et Eliézer, et Jarib, et Gadalie.
19 (Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)
Et ils s'engagèrent à répudier leurs femmes, et ils donnèrent chacun un bélier de son troupeau, pour le péché.
20 Kutoka wazao wa Imeri: Hanani na Zebadia.
Il y eut des fils d'Emmer Anani et Zabdia;
21 Kutoka wazao wa Harimu: Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.
Et des fils d'Eram Masahel, Elia, Samaïa, et Ozias;
22 Kutoka wazao wa Pashuri: Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.
Et des fils de Phasur: Elionaï, Maasia, Ismaël, Nathanaël, Jozabad et Elasa;
23 Miongoni mwa Walawi: Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.
Et des lévites: Jozabad, Samu, Colia (le même que Colite), Phetheia, Judas et Eliézer;
24 Kutoka waimbaji: Eliashibu. Kutoka mabawabu: Shalumu, Telemu na Uri.
Et des chantres: Elisabadi; et des portiers, Solmen, Telmen et Oduth;
25 Miongoni mwa Waisraeli wengine: Kutoka wazao wa Paroshi: Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.
Et d'Israël, des fils de Phoros: Ramia, Azia, Melchia, Méamin, Eléazar, Asabie et Banaïa;
26 Kutoka wazao wa Elamu: Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.
Et des fils d'Hélam: Matthanias, Zacharie et Jahiel, Abdias, Jarimoth et Eue;
27 Kutoka wazao wa Zatu: Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.
Et des fils de Zathuca: Elionaï, Elisub, Matthanaï, Armoth, Zabad et Oziza;
28 Kutoka uzao wa Bebai: Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.
Et des fils de Bubeï. Johanan, Ananie, Zabu et Thali;
29 Kutoka wazao wa Bani: Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.
Et des fils de Banuï: Mosollam, Maluch, Adaïas, Jasub, Saluïa et Remoth;
30 Kutoka wazao wa Pahath-Moabu: Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.
Et des fils de Phaath-Moab Edné, Chalet, Banaïa, Maasia, Matthanias, Béséléel, Banuï et Manassé;
31 Kutoka wazao wa Harimu: Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni,
Et des fils d'Eram: Eliézer, Jésia, Melchia, Samaïas, Séméon,
32 Benyamini, Maluki, na Shemaria.
Benjamin, Baluch, Samaria;
33 Kutoka wazao wa Hashumu: Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.
Et des fils d'Asem: Metthanie, Matthatha, Zadab, Eliphalet, Jerami, Manassé, Sémeï;
34 Kutoka wazao wa Bani: Maadai, Amramu, Ueli,
Et des fils de Bani: Moodia, Amram, Uhel,
35 Benaya, Bedeya, Keluhi,
Banaïas, Badaïas, Helcias,
36 Vania, Meremothi, Eliashibu,
Vania, Marimoth, Eliasiph,
37 Matania, Matenai na Yaasu.
Matthanias, Matthanaï; et ainsi firent:
38 Kutoka wazao wa Binui: Shimei,
Les fils de Banui, et les fils de Sémeï,
39 Shelemia, Nathani, Adaya,
Et Sélémia, et Nathan, et Adaïa,
40 Maknadebai, Shashai, Sharai,
Machadnabu, Séseï, Sariu,
41 Azareli, Shelemia, Shemaria,
Ezriel, et Sélémia, et Samaria,
42 Shalumu, Amaria na Yosefu.
Et Sellum, Amaria, Joseph;
43 Kutoka wazao wa Nebo: Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.
Des fils de Nabu: Jahel, Matthanias, Zabad, Zebennas, Jadaï, Johel et Banaïa.
44 Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.
Tels furent ceux qui avaient épousé des femmes étrangères, et qui en avaient eu des enfants.

< Ezra 10 >