< Ezra 10 >

1 Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana.
Pendant qu'Esdras priait et se confessait, pleurant et se prosternant devant la maison de Dieu, une très grande assemblée d'hommes, de femmes et d'enfants s'assembla auprès de lui de la part d'Israël, car le peuple pleurait très amèrement.
2 Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli.
Shecania, fils de Jehiel, l'un des fils d'Élam, répondit à Esdras: « Nous avons péché contre notre Dieu et nous avons épousé des femmes étrangères parmi les peuples du pays. Mais maintenant, il y a de l'espoir pour Israël à ce sujet.
3 Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria.
Maintenant, faisons donc alliance avec notre Dieu pour répudier toutes les femmes et celles qui sont nées d'elles, selon le conseil de mon seigneur et de ceux qui tremblent devant l'ordre de notre Dieu. Qu'il en soit fait selon la loi.
4 Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”
Lève-toi, car l'affaire est entre tes mains et nous sommes avec toi. Prends courage, et fais-le. »
5 Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa.
Alors Esdras se leva et fit jurer aux chefs des prêtres, aux lévites et à tout Israël qu'ils feraient selon cette parole. Et ils jurèrent.
6 Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.
Esdras se leva de devant la maison de Dieu et entra dans la chambre de Jehohanan, fils d'Eliashib. Quand il y arriva, il ne mangea pas de pain et ne but pas d'eau, car il était en deuil à cause de la faute des exilés.
7 Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu.
On publia dans tout Juda et Jérusalem une annonce à tous les enfants de la captivité, pour qu'ils se rassemblent à Jérusalem,
8 Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.
et que quiconque ne viendrait pas dans les trois jours, selon le conseil des princes et des anciens, perdrait tous ses biens, et serait lui-même séparé de l'assemblée des captifs.
9 Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa.
Et tous les hommes de Juda et de Benjamin se rassemblèrent à Jérusalem dans les trois jours. C'était le neuvième mois, le vingtième jour du mois; et tout le peuple était assis sur la place large, devant la maison de Dieu, tremblant à cause de cette affaire et à cause de la grande pluie.
10 Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli.
Le prêtre Esdras se leva et leur dit: « Vous avez commis une faute, vous avez épousé des femmes étrangères, et vous avez aggravé la culpabilité d'Israël.
11 Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”
Maintenant, confessez-vous à Yahvé, le Dieu de vos pères, et faites sa volonté. Séparez-vous des peuples du pays et des femmes étrangères. »
12 Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema.
Alors toute l'assemblée répondit d'une voix forte: « Nous devons faire ce que tu as dit à notre sujet.
13 Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili.
Mais le peuple est nombreux, et c'est un temps de grande pluie, et nous ne pouvons pas rester dehors. Ce n'est pas l'œuvre d'un jour ou deux, car nous avons beaucoup transgressé dans cette affaire.
14 Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.”
Maintenant, que nos chefs soient désignés pour toute l'assemblée, et que tous ceux qui sont dans nos villes et qui ont épousé des femmes étrangères viennent à des heures fixes, et avec eux les anciens de chaque ville et ses juges, jusqu'à ce que l'ardente colère de notre Dieu se détourne de nous, jusqu'à ce que cette affaire soit résolue. »
15 Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.
Seuls Jonathan, fils d'Asahel, et Jahzeia, fils de Tikva, s'y opposèrent; Meshullam et Shabbethai, le Lévite, les aidèrent.
16 Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo.
Les enfants de la captivité firent ainsi. Le prêtre Esdras, avec certains chefs de famille, selon les maisons de leurs pères, et tous selon leurs noms, furent mis à part; ils s'assirent le premier jour du dixième mois pour examiner la question.
17 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.
Ils en finirent avec tous les hommes qui avaient épousé des femmes étrangères, le premier jour du premier mois.
18 Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni: Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.
Parmi les fils des prêtres, il s'en trouvait qui avaient épousé des femmes étrangères: des fils de Jeshua, fils de Jozadak, et de ses frères: Maaséja, Éliézer, Jarib et Guedalia.
19 (Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)
Ils donnèrent leur main pour répudier leurs femmes; et, étant coupables, ils offrirent un bélier du troupeau pour leur faute.
20 Kutoka wazao wa Imeri: Hanani na Zebadia.
Des fils d'Immer: Hanani et Zebadiah.
21 Kutoka wazao wa Harimu: Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.
Des fils de Harim: Maaséja, Élie, Shemahia, Jehiel et Ozias.
22 Kutoka wazao wa Pashuri: Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.
Des fils de Pashhur: Elioénaï, Maaséja, Ismaël, Nethanel, Jozabad et Elasah.
23 Miongoni mwa Walawi: Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.
Parmi les Lévites: Jozabad, Shimei, Kelaiah (appelé aussi Kelita), Pethahiah, Juda et Eliezer.
24 Kutoka waimbaji: Eliashibu. Kutoka mabawabu: Shalumu, Telemu na Uri.
Des chanteurs: Eliashib. Des gardiens: Shallum, Telem, et Uri.
25 Miongoni mwa Waisraeli wengine: Kutoka wazao wa Paroshi: Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.
D'Israël: Des fils de Parosh: Ramia, Izzia, Malkija, Mijamin, Eléazar, Malkija et Benaja.
26 Kutoka wazao wa Elamu: Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.
Des fils d'Elam: Mattania, Zacharie, Jehiel, Abdi, Jeremoth et Élie.
27 Kutoka wazao wa Zatu: Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.
Des fils de Zattu: Eliœnai, Eliashib, Mattaniah, Jeremoth, Zabad et Aziza.
28 Kutoka uzao wa Bebai: Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.
Des fils de Bébaï: Jehohanan, Hanania, Zabbai et Athlaï.
29 Kutoka wazao wa Bani: Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.
Des fils de Bani: Meshullam, Malluch, Adaiah, Jashub, Sheal et Jeremoth.
30 Kutoka wazao wa Pahath-Moabu: Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.
Des fils de Pahathmoab: Adna, Chelal, Benaiah, Maaseiah, Mattaniah, Bezalel, Binnui et Manassé.
31 Kutoka wazao wa Harimu: Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni,
Des fils de Harim: Éliézer, Ischija, Malkija, Schemaeja, Shimeon,
32 Benyamini, Maluki, na Shemaria.
Benjamin, Malluch et Shemaria.
33 Kutoka wazao wa Hashumu: Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.
Des fils de Hashum: Mattenai, Mattattah, Zabad, Eliphelet, Jeremai, Manasseh et Shimei.
34 Kutoka wazao wa Bani: Maadai, Amramu, Ueli,
Des fils de Bani: Maadaï, Amram, Uel,
35 Benaya, Bedeya, Keluhi,
Benaja, Bedeja, Cheluhi,
36 Vania, Meremothi, Eliashibu,
Vania, Meremoth, Eliashib,
37 Matania, Matenai na Yaasu.
Mattania, Mattenai, Jaasu,
38 Kutoka wazao wa Binui: Shimei,
Bani, Binnui, Shimei,
39 Shelemia, Nathani, Adaya,
Shelemiah, Nathan, Adaiah,
40 Maknadebai, Shashai, Sharai,
Machnadebai, Shashai, Sharai,
41 Azareli, Shelemia, Shemaria,
Azarel, Shelemiah, Shemariah,
42 Shalumu, Amaria na Yosefu.
Shallum, Amaria, et Joseph.
43 Kutoka wazao wa Nebo: Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.
Des fils de Nebo: Jeiel, Mattithiah, Zabad, Zebina, Iddo, Joël et Benaja.
44 Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.
Tous ceux-là avaient pris des femmes étrangères. Certains d'entre eux avaient des femmes dont ils avaient des enfants.

< Ezra 10 >