< Ezra 10 >
1 Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana.
Therfor while Esdras preiede so, and bisouyte God, and wepte, and lai bifor the temple of God, a ful greet cumpenye of Israel, of men, and of wymmen, and of children, was gaderid to him; and the puple wepte bi myche weping.
2 Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli.
And Sechenye, the sone of Jehiel, of the sones of Helam, answeride, and seide to Esdras, We han trespasside ayens oure God, and han weddid wyues, alien wymmen, of `the puplis of the lond. And now, for penaunce is in Israel on this thing,
3 Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria.
smyte we boond of pees with `oure Lord God, and caste we awei alle `wyues aliens, and hem that ben borun of tho wyues, bi the wille of the Lord; and of hem that dreden the comaundement of oure God, `be it don bi the lawe.
4 Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”
Rise thou, it `is thin office to deme, and we schulen be with thee; be thou coumfortid, and do.
5 Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa.
Therfor Esdras roos, and chargide greetli the princes of prestis, and of dekenes, and of al Israel, to do after this word; and thei sworen.
6 Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.
And Esdras roos bifor the hows of God, and he yede to the bed of Johannan, sone of Eliasiph, and entride thidur; he eet not breed, and drank not watir; for he biweilide the trespassing of hem, that weren comun fro the caitifte.
7 Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu.
And a vois of hem was sent in to Juda and Jerusalem, to alle the sones of transmygracioun, that thei schulden be gaderid in to Jerusalem;
8 Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.
and ech man that cometh not in thre daies, bi the counsel of the princes and of eldre men, al his catel schal be takun awey fro him, and he schal be cast awei fro the cumpeny of transmygracioun.
9 Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa.
Therfor alle the men of Juda and of Beniamyn camen togidere in to Jerusalem in thre daies; thilke is the nynthe monethe, in the twentithe dai of the monethe; and al the puple sat in `the street of Goddis hows, and trembliden for synne and reyn.
10 Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli.
And Esdras, the preest, roos, and seide to hem, Ye han trespassid, and han weddid wyues, alien wymmen, that ye schulden `leie to on the trespas of Israel.
11 Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”
And now yyue ye knowlechyng to the Lord God of oure fadris, and do ye his pleasaunce, and be ye departid fro the puplis of the lond, and fro `wyues aliens.
12 Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema.
And al the multitude answeride, and seide with greet vois, Bi thi word to vs, so be it doon.
13 Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili.
Netheles for the puple is myche, and the tyme of reyn is, and we suffren not to stonde withoutforth, and it is not werk of o dai, nether of tweyne; for we han synned greetli in this word;
14 Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.”
`princes be ordeyned in al the multitude, and alle men in oure citees, that han weddid `wyues aliens, come in tymes ordeyned, and with hem come the eldere men, bi citee and citee, and the iugis therof, til the ire of oure God be turned awei fro vs on this synne.
15 Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.
Therfor Jonathan, the sone of Asahel, and Jaazie, the sone of Thecue, stoden on this thing; and Mosollam, and Sebethai, dekenes, helpiden hem.
16 Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo.
And the sones of transmygracioun diden so. And Esdras, the prest, and men, princes of meynees, yeden into the howsis of her fadris, and alle men bi her names; and thei saten in the firste dai of the tenthe monethe, for to seke the thing.
17 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.
And alle men weren endid, that hadden weddid `wyues aliens, `til to the firste dai of the firste monethe.
18 Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni: Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.
And there weren foundun of the sones of preestis, that weddiden `wyues aliens; of the sones of Josue, the sone of Josedech, and hise britheren, Maasie, and Eliezer, and Jarib, and Godolie.
19 (Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)
And thei yauen her hondis, that thei schulden caste out her wyues, and offre for her trespas a ram of the scheep.
20 Kutoka wazao wa Imeri: Hanani na Zebadia.
And of the sones of Semmer; Anam, and Zebedie.
21 Kutoka wazao wa Harimu: Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.
And of the sones of Serym; Maasie, and Helie, and Semeie, and Jehiel, and Ozie.
22 Kutoka wazao wa Pashuri: Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.
And of the sones of Phessur; Helioneai, Maasie, Hismael, Nathanael, and Jozabet, and Elasa.
23 Miongoni mwa Walawi: Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.
And of the sones of dekenes; Josabeth, and Semey, and Elaie; he is Calithaphataie; Juda, and Elezer.
24 Kutoka waimbaji: Eliashibu. Kutoka mabawabu: Shalumu, Telemu na Uri.
And of syngeris, Eliazub; and of porteris, Sellum, and Thellem, and Vry.
25 Miongoni mwa Waisraeli wengine: Kutoka wazao wa Paroshi: Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.
And of Israel, of the sones of Pharos; Remea, and Ezia, and Melchia, and Vnanym, and Eliezer, and Melchia, and Banea.
26 Kutoka wazao wa Elamu: Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.
And of the sones of Elam; Mathanye, and Zacharie, and Jehil, and Abdi, and Rymoth, and Helia.
27 Kutoka wazao wa Zatu: Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.
And of the sones of Zechua; Helioneay, Heliasib, Mathanye, and Jerymuth, and Zaeth, and Aziza.
28 Kutoka uzao wa Bebai: Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.
And of the sones of Bebai; Johannan, Ananye, Zabbai, Athalia.
29 Kutoka wazao wa Bani: Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.
And of the sones of Beny; Mosallam, and Melue, and Azaie, Jasub, and Saal, and Ramoth.
30 Kutoka wazao wa Pahath-Moabu: Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.
And of the sones of Phaeth; Moab, Edua, and Calal, Banaie, and Massie, Mathanye, Beseleel, and Bennun, and Manasse.
31 Kutoka wazao wa Harimu: Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni,
And of the sones of Erem; Elieer, Jesue, Melchie, Semeye, Symeon,
32 Benyamini, Maluki, na Shemaria.
Beniamyn, Maloth, Samarie.
33 Kutoka wazao wa Hashumu: Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.
And of the sones of Asom; Mathanai, Mathetha, Zabeth, Eliphelech, Jermai, Manasse, Semei.
34 Kutoka wazao wa Bani: Maadai, Amramu, Ueli,
Of the sones of Bany; Maddi, Amram, and Huel,
35 Benaya, Bedeya, Keluhi,
Baneas, and Badaie, Cheilian,
36 Vania, Meremothi, Eliashibu,
Biamna, Marymuth, and Eliasiph,
37 Matania, Matenai na Yaasu.
Mathanye, and Jasy,
38 Kutoka wazao wa Binui: Shimei,
and Bany, and Bennan, and Semei,
39 Shelemia, Nathani, Adaya,
and Salymas, and Nathan, and Daias,
40 Maknadebai, Shashai, Sharai,
Metuedabai, Sisai, Sarai,
41 Azareli, Shelemia, Shemaria,
Ezrel, and Seloman, Semerie,
42 Shalumu, Amaria na Yosefu.
Sellum, Amarie, Joseph.
43 Kutoka wazao wa Nebo: Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.
Of the sones of Nebny; Aiel, Mathatie, Zabed, Zabina, Jebdu, and Johel, Banai.
44 Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.
Alle these hadden take `wyues aliens, and of hem weren wymmen, that hadden bore children.