< Ezekieli 1 >

1 Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
Ottuzinchi yili, tötinchi ayning beshinchi künide, men Kéwar deryasigha sürgün qilin’ghanlar arisida turghan mezgilde, mana asmanlar échilip, men Xudaning alamet körünüshlirini kördüm.
2 Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
Tötinchi ayning beshinchi küni — Yehoakinning sürgün bolghanliqining beshinchi yili idi —
3 neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
Kaldiylerning zéminida, Kéwar deryasi boyida, Buzining oghli Ezakiyal kahin’gha Perwerdigarning sözi keldi — shu yerde Perwerdigarning qoli uning wujudigha qondi.
4 Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
Men kördüm, mana! Shimaldin boran-chapqun kötürüldi; yoghan bir bulut we uni orap turghan bir ot, uning etrapida bir yoruqluq julalinip turatti; otturisidin, yeni shu ot ichidin, issiqtin julalan’ghan parqiraq mistek bir körünüsh köründi.
5 Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
Yene uning otturisidin, töt hayat mexluq köründi; ularning körünüshi shundaq idiki: — ularda insanning qiyapiti bar idi;
6 lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
ularning herbirining töttin yüzi bar idi; herbirining töttin qaniti bar idi.
7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
Ularning tüptüz putliri bar idi; tapanliri bolsa mozayning tuyaqlirigha oxshaytti; ular parqiritilghan mistek parlap turatti.
8 Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
Töt yénida, qanatliri astida insanningkidek birdin qoli bar idi; tötisining herbirining töttin yüzi we töttin qaniti bar idi;
9 nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
ularning qanatliri bir-birige tutash idi; ular yürgende héchyaqqa burulmaytti; ular hemmisi udul aldigha yüretti.
10 Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
Ularning yüz körünüshliri insanningkidek idi; u tötisining ong teripide shirningkidek yüzi bar idi; tötisining sol teripide buqiningkidek yüzi bar idi; tötisining bürkütningkidek yüzimu bar idi.
11 Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
Ularning yüzliri ene shundaq idi. Qanatliri yuqirida kérilip turatti; herbirining ikki qaniti ikki teripidiki mexluqning qanitigha tutishatti; yene ikki qaniti öz ténini yépip turatti.
12 Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
Ularning herbiri udulgha qarap mangatti; ularda bolghan roh nege barimen dése, ular shu yerge mangatti; ular mangghanda héchqaysi terepke burulmaytti.
13 Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
Hayat mexluqlarning qiyapiti bolsa, köyüp yalqunlap turghan otning choghidek, mesh’ellerdek idi; mushu ot uyan-buyan aylinip mexluqlar arisida yüretti; ot intayin yalqunluq idi, ottin chaqmaqlar chéqip turatti;
14 Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
hayat mexluqlar chaqmaqtek pal-pul qilip uyaqtin-buyaqqa yügürüp turatti.
15 Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
Men hayat mexluqlargha qaridim, mana hayat mexluqlarning herbirining yénida yerde turidighan, ularning yüzige udullan’ghan birdin chaq turatti;
16 Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
chaqlarning shekli we yasilishi béril yaqutning körünüshide idi; tötisining birxilla körünüshi bar idi; ularning shekli we yasilishi bolsa, chaqning ichide chaq bardek idi.
17 Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
Mexluqlar mangghanda, ular yüzlen’gen töt teripining hemmisige udul mangatti; mangghanda ular héch burulmaytti.
18 Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
Chaqlarning ultangliri bolsa, intayin égiz hem dehshetlik idi; ular tötisining ultanglirining pütün etrapi közler bilen tolghanidi.
19 Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
Hayat mexluqlar mangghanda, chaqlar ulargha yandiship mangatti; hayat mexluqlar yerdin kötürülgende, chaqlarmu kötürületti.
20 Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Roh nege mang dése, ular shu yerge mangatti — démek, ularning rohi [Rohqa] egiship mangatti. Chaqlar ular bilen teng kötürületti; chünki mexluqlarning rohi chaqlirida idi.
21 Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Mexluqlar mangghanda, chaqlarmu mangatti; mexluqlar toxtighanda, chaqlarmu toxtaytti; ular yerdin kötürülginide, chaqlarmu ulargha qoshulup teng kötürületti; chünki hayat mexluqlarning rohi chaqlarda idi.
22 Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
Hayat mexluqlarning bashliri üstide bir yoghan köz yetküsiz gümbezge oxshaydighan bir nerse turatti; u xrustaldek dehshetlik parqirap, ularning béshi üstide yéyilip turatti.
23 Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
Bu gümbezdek nersining astida ularning qanatliri kérilip, bir-birige tégiship turatti; herbir mexluqning öz ténining ikki yénini yapidighan ikkidin qaniti bar idi.
24 Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
Ular mangghanda, men qanatlirining sadasini anglidim — u ulugh sularning sharqirighan sadasidek, Hemmige Qadirning awazidek — qoshunning yürüsh qiliwatqan chaghdiki süren-shawqunlirining sadasidek idi; ular toxtap turghan chaghlarda, ular qanatlirini töwen’ge chüshüretti.
25 Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
We ularning béshi üstidiki gümbezdek nerse üstidin bir awaz anglandi. Ular toxtap turghan chaghlarda, ular qanatlirini töwen’ge chüshüretti.
26 Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
Ularning béshi üstidiki gümbezdek nerse üstide, kök yaqut kebi bir textning siymasi turatti; bu text siymasining üstide, tolimu yuqirida, insan qiyapitide körün’gen bir zat turatti.
27 Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
We men bu zatni bélining üsti teripining turqi mistek parqirghan, etrapini ot orap turghan qiyapettiki bir körünüshte kördüm; we bélining asti teripining turqi, otning qiyapitide idi, uning etrapida küchlük yoruqluq turatti.
28 Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.
Bu etrapida turghan küchlük yoruqluqning körünüshi bolsa, yamghurluq künidiki bulutta peyda bolghan hesen-hösenning körünüshidek idi. Bu bolsa Perwerdigarning shan-sheripining qiyapitining körünüshi idi. Buni körüpla men düm yiqildim; we men sözlewatqan birsining awazini anglidim.

< Ezekieli 1 >