< Ezekieli 1 >

1 Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
Et il arriva que, en ma trentième année, le quatrième mois, le cinquième jour du mois, j'étais assis au milieu des captifs, sur le fleuve Chobar; et les cieux furent ouverts, et j'eus les visions de Dieu.
2 Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
Le cinquième jour de ce mois, en cette année, la cinquième de la captivité du roi Joakim,
3 neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
La parole du Seigneur vint à Ezéchiel, fils de Buzi, le prêtre, en la terre des Chaldéens, sur le fleuve Chobar. Et la main du Seigneur fut sur moi.
4 Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
Et je vis, et voilà qu'un vent violent vint de l'aquilon, et avec lui une grande nuée, et tout alentour une lueur et un feu brillant, et, au milieu, comme une vision d'émail au milieu du feu, et cet émail était lumineux.
5 Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
Et au milieu du feu il y avait comme la ressemblance de quatre animaux, et voici leur aspect: il y avait en eux la ressemblance d'un homme;
6 lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
Et à chacun quatre faces, et à chacun quatre ailes,
7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
Et leurs jambes étaient droites, et leurs pieds ailés; et ils lançaient des étincelles, comme de l'airain brillant. Et leurs ailes étaient légères,
8 Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
Et il y avait une main d'homme sous leurs ailes, aux quatre côtés.
9 nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
Et les faces de ces quatre animaux ne se retournaient pas, quand ils marchaient; ils allaient chacun droit devant sa face.
10 Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
Et voici la ressemblance de leurs faces: une face d'homme et une face de lion à droite des quatre, une face de veau à gauche des quatre, et une face d'aigle aux quatre.
11 Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
Et quatre ailes étaient étendues au-dessus d'eux; deux de ces ailes les joignaient l'un à l'autre, et deux couvraient leur corps.
12 Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
Et chacun marchait droit en avant; où le vent allait, ils allaient, et ils ne se retournaient pas.
13 Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
Et au milieu des animaux, il y avait comme une vision de charbons en feu, comme une vision de lampes courant ensemble entre les animaux, et une flamme éclatante, et de la flamme sortaient des éclairs.
14 Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
Et je vis, et voilà qu'il y avait une roue sur la terre auprès des quatre animaux,
15 Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
Et je vis, et voilà qu'il y avait une roue sur la terre auprès des quatre animaux,
16 Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
Et l'aspect des roues était comme l'aspect de Tharsis, et toutes les quatre étaient semblables. Et elles étaient faites comme s'il y avait eu une roue dans une roue.
17 Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
Et elles allaient sur leurs quatre parties, et elles ne se retournaient pas en marchant,
18 Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
Ni elles ni leurs moyeux; et elles étaient hautes; et je vis leurs parties, et leurs moyeux étaient remplis d'yeux, aux quatre circonférences.
19 Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
Et quand les animaux marchaient, les quatre roues à côté d'eux marchaient, et quand les animaux s'élevaient au-dessus de terre, les roues s'élevaient.
20 Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Et partout où était la nuée, là aussi le vent soufflait; et les roues marchaient et s'élevaient avec les animaux; car un souffle de vie était dans les roues.
21 Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Quand les animaux marchaient, elles marchaient; quand ils s'arrêtaient, elles s'arrêtaient, et quand ils s'élevaient au-dessus de la terre, elles s'élevaient avec eux; car un souffle de vie était dans les roues.
22 Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
Et au-dessus de la tête des animaux il y avait une image comme celle d'un firmament, semblable à du cristal, qui s'étendait au-dessus de leurs ailes.
23 Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
Et, au-dessus du firmament, leurs ailes étaient étendues, battant l'une contre l'autre, et celles de dessous couvrant leurs corps.
24 Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
Et j'entendis le bruit de leurs ailes pendant qu'ils marchaient, comme la voix des grandes eaux; et quand ils s'arrêtaient, leurs ailes se reposaient.
25 Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
Et voilà qu'une voix sortit du firmament qui était au-dessus de leurs tètes,
26 Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
Et qui ressemblait à un saphir, et qui supportait l'image d'un trône, sur lequel était une image semblable à un homme.
27 Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
Et je vis comme une vision d'émail, depuis ses reins jusqu'en haut; et depuis ses reins jusqu'en bas je vis une vision de feu, et sa lueur formait un cercle,
28 Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.
Semblable à l'arc qui est dans la nuée les jours de pluie; telle était la forme de cette lueur en cercle. C'est ainsi que je vis l'image de la gloire du Seigneur; je la vis, et je tombai la face contre terre, et j'entendis la voix d'un esprit qui parlait.

< Ezekieli 1 >