< Ezekieli 1 >

1 Katika mwaka wa thelathini, mwezi wa nne, siku ya tano ya mwezi, wakati nilipokuwa miongoni mwa hao waliokuwa uhamishoni kando ya Mto Kebari, mbingu zilifunguka nami nikaona maono ya Mungu.
Stalo se pak třidcátého léta, čtvrtého měsíce, dne pátého, když jsem byl mezi zajatými u řeky Chebar, že otevřína byla nebesa, a viděl jsem vidění Boží.
2 Katika siku ya tano ya mwezi, ilikuwa mwaka wa tano wa kuhamishwa kwa Mfalme Yehayakini,
Pátého dne téhož měsíce, pátého léta zajetí krále Joachina,
3 neno la Bwana lilimjia Ezekieli kuhani, mwana wa Buzi, kando ya Mto Kebari, katika nchi ya Wakaldayo. Huko mkono wa Bwana ulikuwa juu yake.
V pravdě stalo se slovo Hospodinovo k Ezechielovi knězi, synu Buzi, v zemi Kaldejské u řeky Chebar, a byla nad ním ruka Hospodinova.
4 Nilitazama, nikaona dhoruba kubwa ikitoka kaskazini, wingu kubwa sana pamoja likiwa na umeme wa radi likiwa limezungukwa na mwanga mkali. Katikati ya huo moto kulikuwa kama rangi ya manjano ya chuma kinapokuwa ndani ya moto.
I viděl jsem, a aj, vítr tuhý přicházel od půlnoci, a oblak veliký, a oheň plápolající, a okolo něho byl blesk, a z prostředku jeho jako nějaká velmi prudká světlost, z prostředku toho ohně.
5 Katika ule moto kulikuwa na kitu kinachofanana na viumbe vinne vyenye uhai. Katika kuonekana kwake vilikuwa na umbo mfano wa mwanadamu,
Z prostředku jeho také ukázalo se podobenství čtyř zvířat, jejichž takový byl způsob: Podobenství člověka měli.
6 lakini kila kimoja kilikuwa na nyuso nne na mabawa manne.
A po čtyřech tvářích jedno každé, a po čtyřech křídlích jedno každé mělo.
7 Miguu yao ilikuwa imenyooka, nyayo za miguu yao zilikuwa kama kwato za miguu ya ndama, nazo zilimetameta kama shaba iliyosuguliwa.
Jejichž nohy nohy přímé, ale zpodek noh jejich jako zpodek nohy telecí, a blyštěly se podobně jako ocel pulerovaná.
8 Chini ya mabawa yao katika pande zao nne walikuwa na mikono ya mwanadamu. Wote wanne walikuwa na nyuso na mabawa,
Ruce pak lidské pod křídly jejich, po čtyřech stranách jejich, a tváři jejich i křídla jejich na čtyřech těch stranách.
9 nayo mabawa yao yaligusana. Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja, hawakugeuka walipokuwa wanatembea.
Spojena byla křídla jejich jednoho s druhým. Neobracela se, když šla; jedno každé přímo na svou stranu šlo.
10 Kuonekana kwa nyuso zao kulikuwa hivi: Kila mmoja wa wale wanne alikuwa na uso wa mwanadamu na kwa upande wa kulia kila mmoja alikuwa na uso wa simba, upande wa kushoto alikuwa na uso wa ngʼombe pia kila mmoja alikuwa na uso wa tai.
Podobenství pak tváří jejich s předu tvář lidská, a tvář lvová po pravé straně každého z nich; tvář pak volovou po levé straně všech čtvero, též tvář orličí s zadu mělo všech čtvero z nich.
11 Hivyo ndivyo zilivyokuwa nyuso zao. Mabawa yao yalikunjuliwa kuelekea juu, kila mmoja alikuwa na mabawa mawili ambayo kila moja liligusa bawa la mwenzake kila upande na mabawa mengine mawili yakifunika mwili wake.
A tváři jejich i křídla jejich pozdvižena byla zhůru. Každé zvíře dvě křídla pojilo s křídly dvěma druhého, dvěma pak přikrývala těla svá.
12 Kila mmoja alikwenda kuelekea mbele moja kwa moja. Popote roho alipotaka kwenda, ndipo walipokwenda pasipo kugeuka.
A každé přímo na svou stranu šlo. Kamkoli ukazoval duch, aby šla, tam šla, neuchylovala se, když chodila.
13 Kuonekana kwa vile viumbe hai katikati kulikuwa kama makaa ya mawe yanayowaka au kama mienge. Moto ule ulikuwa ukienda mbele na nyuma katikati ya vile viumbe, ulikuwa na mwangaza mkali na katikati ya ule moto kulitoka kimulimuli kama umeme wa radi.
Podobnost také těch zvířat na pohledění byla jako uhlí řeřavého, na pohledění jako pochodně. Kterýžto oheň ustavičně chodil mezi zvířaty, a ten oheň měl blesk, a z téhož ohně vycházelo blýskání.
14 Vile viumbe vilipiga mbio kwenda na kurudi, kama vimulimuli vya umeme wa radi.
Také ta zvířata běhala, a navracovala se jako prudké blýskání.
15 Nilipokuwa nikitazama vile viumbe hai, niliona gurudumu moja juu ya ardhi kando ya kila kiumbe kikiwa na nyuso zake nne.
A když jsem hleděl na ta zvířata, a aj, kolo jedno bylo na zemi při zvířatech u čtyř tváří jednoho každého z nich.
16 Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa hayo magurudumu na muundo wake: yalingʼaa kama zabarajadi, nayo yote manne yalifanana. Kila gurudumu lilikuwa na gurudumu jingine ndani yake.
Na pohledění byla kola, a udělání jich jako barva tarsis, a podobnost jednostejnou měla všecka ta kola, a byla na pohledění i udělání jejich, jako by bylo kolo u prostřed kola.
17 Yalipokwenda yalielekea upande wowote wa pande nne walipoelekea wale viumbe, magurudumu hayakuzunguka wakati viumbe vile vilipokwenda.
Na čtyři strany své jíti majíce, chodila, a neuchylovala se, když šla.
18 Kingo zake zilikuwa ndefu kwenda juu na za kutisha, nazo zote nne zilijawa na macho pande zote.
A loukoti své, i vysokost měla, že hrůza z nich šla, a šínové jejich vůkol všech čtyř kol plní byli očí.
19 Vile viumbe hai vilipokwenda, magurudumu yaliyokuwa kando yao yalisogea na wakati hivyo viumbe hai vilipoinuka kutoka ardhini magurudumu nayo yaliinuka.
Když pak chodila zvířata, chodila kola podlé nich, a když se vznášela zvířata vzhůru od země, vznášela se i kola.
20 Mahali popote roho alipokwenda wale viumbe nao walikwenda, nayo magurudumu yaliinuka pamoja navyo, kwa sababu roho ya vile viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Kdekoli chtěl Duch, aby šla, tam šla; kde Duch chtěl jíti, i kola vznášela se naproti nim, nebo duch zvířat byl v kolách.
21 Wakati viumbe vile viliposogea, nayo magurudumu yalisogea, viumbe viliposimama kimya, nayo pia yalisimama kimya, viumbe vilipoinuka juu ya nchi magurudumu yaliinuliwa pamoja navyo kwa kuwa roho ya hivyo viumbe hai alikuwa ndani ya hayo magurudumu.
Když ona šla, šla, a když ona stála, stála, a když se vznášela od země, vznášela se také kola s nimi, nebo duch zvířat byl v kolách.
22 Juu ya vichwa vya hao viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa eneo lililokuwa wazi, lililokuwa angavu kabisa na lenye kutisha.
Podobenství pak oblohy bylo nad hlavami zvířat jako podobenství křištálu roztaženého nad hlavami jejich svrchu.
23 Chini ya hiyo nafasi mabawa yao yalitanda moja kuelekea jingine, kila mmoja alikuwa na mabawa mengine mawili yaliyofunika mwili wake.
A pod oblohou křídla jejich pozdvižená byla, jedno připojené k druhému. Každé mělo dvě, jimiž se přikrývalo, každé, pravím, mělo dvě, jimiž přikrývalo tělo své.
24 Viumbe wale waliposogea nilisikia sauti ya mabawa yao, kama ngurumo ya maji yaendayo kasi, kama sauti ya Mwenyezi, kama makelele ya jeshi. Waliposimama kimya walishusha mabawa yao.
I slyšel jsem zvuk křídel jejich jako zvuk vod mnohých, jako zvuk Všemohoucího, když chodila, zvuk hluku jako zvuk vojska. Když pak stála, spustila křídla svá.
25 Ndipo ikaja sauti toka juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao, waliposimama mabawa yao yakiwa yameshushwa.
Byl také zvuk svrchu nad oblohou, kteráž byla nad hlavou jejich, když stála a spustila křídla svá.
26 Juu ya ile nafasi ya wazi iliyokuwa juu ya vichwa vyao kulikuwa na kitu mfano wa kiti cha enzi cha yakuti samawi. Na juu ya kile kiti cha enzi kulikuwa na umbo mfano wa mwanadamu.
Svrchu pak na obloze, kteráž byla nad hlavou jejich, bylo podobenství trůnu, na pohledění jako kámen zafirový, a nad podobenstvím trůnu na něm svrchu, na pohledění jako tvárnost člověka.
27 Nikaona kwamba kutokana na kile nilichoona kama kiuno chake kuelekea juu alionekana kama chuma inayowaka kana kwamba imejaa moto na kuanzia kiuno kwenda chini alionekana kama moto na mwanga mkali ulimzunguka.
I viděl jsem na pohledění jako velmi prudkou světlost, a u vnitřku jejím vůkol na pohledění jako oheň, od bedr jeho vzhůru; od bedr pak jeho dolů viděl jsem na pohledění jako oheň, a blesk vůkol něho.
28 Kama vile kuonekana kwa upinde wa mvua mawinguni siku ya mvua, ndivyo ulivyokuwa ule mngʼao uliomzunguka. Hivi ndivyo ilivyokuwa kuonekana kwa utukufu wa Bwana. Nilipouona, nikaanguka kifudifudi, nikasikia sauti ya mtu anaongea.
Na pohledění jako duha, kteráž bývá na oblace v čas deště, takový na pohledění byl blesk vůkol. To bylo vidění podobenství slávy Hospodinovy. Kteréžto viděv, padl jsem na tvář svou, a slyšel jsem hlas mluvícího.

< Ezekieli 1 >