< Ezekieli 9 >
1 Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
Puis il cria d'une voix forte moi l'entendant, et il dit: faites approcher ceux qui ont commission contre la ville, chacun avec son instrument de destruction dans sa main.
2 Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu, linalotazama kaskazini kila mmoja na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Pamoja nao alikuwepo mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande mmoja. Wakaingia ndani ya Hekalu wakasimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
Et voici six hommes venaient de devers le chemin de la haute porte qui regarde vers l'Aquilon, et chacun avait en sa main son instrument de destruction; et il y avait au milieu d'eux un homme vêtu de lin, qui avait un cornet d'écrivain sur ses reins; et ils entrèrent, et se tinrent auprès de l'autel d'airain.
3 Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Bwana akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi aliyekuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja,
Alors la gloire du Dieu d'Israël s'éleva de dessus le Chérubin sur lequel elle était, [et vint] sur le seuil de la maison, et il cria à l'homme qui était vêtu de lin, [et] qui avait le cornet d'écrivain sur ses reins.
4 akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
Et l'Eternel lui dit: passe par le milieu de la ville, par le milieu de Jérusalem, et marque [la lettre] Thau sur les fronts des hommes qui gémissent et qui soupirent à cause de toutes les abominations qui se commettent au dedans d'elle.
5 Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
Et il dit aux autres, moi l'entendant: passez par la ville après lui, et frappez; que votre œil n'épargne [personne], et n'ayez point de compassion.
6 Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
Tuez tout, les vieillards, les jeunes gens, les vierges, les petits enfants, et les femmes; mais n'approchez point d'aucun de ceux sur lesquels sera [la lettre] Thau, et commencez par mon Sanctuaire. Ils commencèrent donc par les vieillards qui [étaient] devant la maison.
7 Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze kumbi zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda wakaanza kuua watu mjini kote.
Et il leur dit: profanez la maison, et remplissez les parvis de gens tués; sortez, et ils sortirent, et frappèrent par la ville.
8 Wakati walikuwa wakiwaua watu, nami nilikuwa nimeachwa peke yangu, nikaanguka kifudifudi, nikapiga kelele nikisema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
Or il arriva que comme ils frappaient, je demeurai là, et m'étant prosterné le visage contre terre, je criai, et dis: Ah! ah! Seigneur Eternel! t'en vas-tu donc détruire tous les restes d'Israël, en répandant ta fureur sur Jérusalem?
9 Bwana akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Bwana ameiacha nchi, Bwana hauoni.’
Et il me dit: l'iniquité de la maison d'Israël et de Juda est excessivement grande, et le pays est rempli de meurtres, et la ville remplie de crimes; car ils ont dit: l'Eternel a abandonné le pays, et l'Eternel ne [nous] voit point.
10 Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwaachilia lakini nitaleta juu ya vichwa vyao, yale waliyoyatenda.”
Et quant à moi, mon œil aussi ne [les] épargnera point, et je n'en aurai point de compassion; je leur rendrai leur train sur leur tête.
11 Ndipo mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani safi na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja, akarudi na kutoa taarifa akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”
Et voici, l'homme vêtu de lin, qui avait le cornet sur ses reins, rapporta ce qui avait été fait, et il dit: J'ai fait comme tu m'as commandé.