< Ezekieli 9 >
1 Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
Alors il cria à mes oreilles d'une voix forte, en disant: « Fais approcher ceux qui ont la garde de la ville, chacun avec son arme de destruction à la main. »
2 Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu, linalotazama kaskazini kila mmoja na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Pamoja nao alikuwepo mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande mmoja. Wakaingia ndani ya Hekalu wakasimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
Et voici que six hommes arrivèrent par le chemin de la porte supérieure, qui se trouve vers le nord, chacun avec son arme de destruction à la main. Un homme au milieu d'eux était vêtu de lin, avec un cornet d'écrivain à son côté. Ils entrèrent et se placèrent à côté de l'autel de bronze.
3 Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Bwana akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi aliyekuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja,
La gloire du Dieu d'Israël monta du chérubin, où il se trouvait, jusqu'au seuil de la maison; et il appela l'homme vêtu de lin, qui tenait à son côté l'encornoir de l'écrivain.
4 akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
Yahvé lui dit: « Passe par le milieu de la ville, par le milieu de Jérusalem, et mets une marque sur le front des hommes qui soupirent et qui pleurent sur toutes les abominations qui se commettent dans son sein. »
5 Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
Aux autres, il dit à mon oreille: « Traversez la ville après lui, et frappez. Ne laissez pas votre œil épargner, et n'ayez pas de pitié.
6 Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
Tuez par interdit le vieillard, le jeune homme, la vierge, les petits enfants et les femmes; mais n'approchez pas de l'homme qui porte la marque. Commence par mon sanctuaire. » Puis ils se sont attaqués aux vieillards qui étaient devant la maison.
7 Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze kumbi zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda wakaanza kuua watu mjini kote.
Il leur dit: « Souillez la maison, et remplissez les parvis de morts. Sortez! » Ils sont sortis, et ont frappé dans la ville.
8 Wakati walikuwa wakiwaua watu, nami nilikuwa nimeachwa peke yangu, nikaanguka kifudifudi, nikapiga kelele nikisema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
Pendant qu'ils tuaient, et que je restais, je tombai sur ma face, et je criai, en disant: « Ah! Seigneur Yahvé! Détruiras-tu tout le reste d'Israël en déversant ta colère sur Jérusalem? »
9 Bwana akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Bwana ameiacha nchi, Bwana hauoni.’
Puis il me dit: « L'iniquité de la maison d'Israël et de Juda est extrêmement grande, le pays est plein de sang, et la ville pleine de perversion; car ils disent: « Yahvé a abandonné le pays, et Yahvé ne voit pas.
10 Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwaachilia lakini nitaleta juu ya vichwa vyao, yale waliyoyatenda.”
Quant à moi aussi, mon œil n'épargnera pas, je n'aurai pas de pitié, mais je ferai retomber leur voie sur leur tête. »
11 Ndipo mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani safi na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja, akarudi na kutoa taarifa akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”
Voici que l'homme vêtu de lin, qui tenait l'encornoir à son côté, fit son rapport en disant: « J'ai fait ce que tu m'as ordonné. »