< Ezekieli 9 >

1 Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
And He crieth in mine ears — a loud voice — saying, 'Drawn near have inspectors of the city, and each his destroying weapon in his hand.'
2 Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu, linalotazama kaskazini kila mmoja na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Pamoja nao alikuwepo mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande mmoja. Wakaingia ndani ya Hekalu wakasimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
And lo, six men are coming from the way of the upper gate, that is facing the north, and each his slaughter-weapon in his hand, and one man in their midst is clothed with linen, and a scribe's inkhorn at his loins, and they come in, and stand near the brazen altar.
3 Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Bwana akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi aliyekuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja,
And the honour of the God of Israel hath gone up from off the cherub, on which it hath been, unto the threshold of the house.
4 akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
And He calleth unto the man who is clothed with linen, who hath the scribe's inkhorn at his loins, and Jehovah saith unto him, 'Pass on into the midst of the city, into the midst of Jerusalem, and thou hast made a mark on the foreheads of the men who are sighing and who are groaning for all the abominations that are done in its midst.'
5 Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
And to the others he said in mine ears, 'Pass on into the city after him, and smite; your eye doth not pity, nor do ye spare;
6 Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
aged, young man, and virgin, and infant, and women, ye do slay — to destruction; and against any man on whom [is] the mark ye do not go nigh, and from My sanctuary ye begin.'
7 Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze kumbi zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda wakaanza kuua watu mjini kote.
And they begin among the aged men who [are] before the house, and He saith unto them, 'Defile the house, and fill the courts with the wounded, go forth.' And they have gone forth and have smitten in the city.
8 Wakati walikuwa wakiwaua watu, nami nilikuwa nimeachwa peke yangu, nikaanguka kifudifudi, nikapiga kelele nikisema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
And it cometh to pass, as they are smiting, and I — I am left — that I fall on my face, and cry, and say, 'Ah, Lord Jehovah, art Thou destroying all the remnant of Israel, in Thy pouring out Thy wrath on Jerusalem?'
9 Bwana akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Bwana ameiacha nchi, Bwana hauoni.’
And He saith unto me, 'The iniquity of the house of Israel and Judah [is] very very great, and the land is full of blood, and the city hath been full of perverseness, for they have said: Jehovah hath forsaken the land, and Jehovah is not seeing.
10 Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwaachilia lakini nitaleta juu ya vichwa vyao, yale waliyoyatenda.”
And I also, Mine eye doth not pity, nor do I spare; their way on their own head I have put.'
11 Ndipo mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani safi na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja, akarudi na kutoa taarifa akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”
And lo, the man clothed with linen, at whose loins [is] the inkhorn, is bringing back word, saying, 'I have done as Thou hast commanded me.'

< Ezekieli 9 >