< Ezekieli 9 >

1 Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
And he called out in ears my a voice great saying they have drawn near [the] punishments of the city and everyone [the] weapon of destruction his [is] in hand his.
2 Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu, linalotazama kaskazini kila mmoja na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Pamoja nao alikuwepo mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande mmoja. Wakaingia ndani ya Hekalu wakasimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
And there! six men [were] coming - from [the] direction of [the] gate upper which - [is] faced north-ward and everyone [the] weapon of shattering his [was] in hand his and a man one [was] in midst of them clothed linen and [the] writing-case of scribe [was] at hips his and they came and they stood beside [the] altar of bronze.
3 Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Bwana akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi aliyekuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja,
And [the] glory of - [the] God of Israel it was taken up from on the cherub which it had been on it to [the] threshold of the house and he called to the man who was clothed the linen whom writing-case of scribe [was] at hips his.
4 akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
And he said Yahweh (to him *Q(k)*) pass in [the] midst of the city in [the] midst of Jerusalem and you will mark a mark on [the] foreheads of the people who sigh and who groan on all the abominations which are done in [the] midst of it.
5 Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
And to these he said in ears my pass in the city after him and strike (not *Q(K)*) let it look with compassion (eye your *Q(K)*) and may not you show pity.
6 Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
Old [man] young man and virgin and little one[s] and women you will kill to destruction and to any person whom [is] on him the mark may not you draw near and from sanctuary my you will begin and they began with the men old who [were] before the house.
7 Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze kumbi zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda wakaanza kuua watu mjini kote.
And he said to them make unclean the house and fill the courts [those] slain go forth and they went forth and they struck in the city.
8 Wakati walikuwa wakiwaua watu, nami nilikuwa nimeachwa peke yangu, nikaanguka kifudifudi, nikapiga kelele nikisema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
And it was when were striking they and [was] remaining I and I fell! on face my and I cried out and I said alas! O Lord Yahweh ¿ about to destroy [are] you all [the] remnant of Israel when pouring out you rage your on Jerusalem.
9 Bwana akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Bwana ameiacha nchi, Bwana hauoni.’
And he said to me [the] iniquity of [the] house of Israel and Judah [is] great with muchness muchness and it has been filled the land blood and the city it is full perverseness for they have said he has forsaken Yahweh the land and not Yahweh [is] seeing.
10 Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwaachilia lakini nitaleta juu ya vichwa vyao, yale waliyoyatenda.”
And also I not it will look with compassion eye my and not I will show pity conduct their on own head their I will requite.
11 Ndipo mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani safi na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja, akarudi na kutoa taarifa akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”
And there! the man - clothed of the linen whom the writing-case [was] at hips his [was] bringing back a word saying I have done (according to all that *Q(K)*) you commanded me.

< Ezekieli 9 >