< Ezekieli 9 >

1 Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
Saa hørte jeg ham raabe med vældig Røst: »Byens Hjemsøgelse nærmer sig, og hver har sit Mordvaaben i Haanden!«
2 Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu, linalotazama kaskazini kila mmoja na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Pamoja nao alikuwepo mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande mmoja. Wakaingia ndani ya Hekalu wakasimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
Og se, seks Mænd kom fra den øvre Nordport, hver med sin Stridshammer i Haanden, og een iblandt dem bar linned Klædebon og havde et Skrivetøj ved sin Lænd; og de kom og stillede sig ved Siden af Kobberalteret.
3 Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Bwana akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi aliyekuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja,
Men Israels Guds Herlighed havde hævet sig fra Keruberne, som den hvilede paa, og flyttet sig hen til Templets Tærskel; og han raabte til Manden i det linnede Klædebon og med Skrivetøjet ved Lænden,
4 akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
og HERREN sagde til ham: »Gaa midt igennem Byen, igennem Jerusalem, og sæt et Mærke paa de Mænds Pander, der sukker og jamrer over alle de Vederstyggeligheder, som øves i dets Midte!«
5 Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
Og til de andre hørte jeg ham sige: »Gaa efter ham ud gennem Byen og hug ned! Vis ingen Medynk eller Skaansel!
6 Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
Oldinge og Ynglinge, Jomfruer, Børn og Kvinder skal I hugge ned og udrydde; men ingen af dem, der bærer Mærket, maa I røre! Begynd ved min Helligdom!« Saa begyndte de med de Ældste, som stod foran Templet,
7 Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze kumbi zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda wakaanza kuua watu mjini kote.
Og han sagde til dem: »Gør Templet urent, fyld Forgaardene med dræbte og drag saa ud!« Og de drog ud og huggede ned i Byen.
8 Wakati walikuwa wakiwaua watu, nami nilikuwa nimeachwa peke yangu, nikaanguka kifudifudi, nikapiga kelele nikisema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
Men medens de huggede ned og jeg var ene tilbage, faldt jeg paa mit Ansigt og raabte: »Ak, Herre, HERRE vil du da tilintetgøre alt, hvad der er levnet af Israel, ved at udøse din Vrede over Jerusalem?«
9 Bwana akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Bwana ameiacha nchi, Bwana hauoni.’
Han svarede: »Israels og Judas Hus's Brøde er saare, saare stor, thi Landet er fuldt af Blodskyld og Byen af Retsbrud; thi de siger, at HERREN har forladt Byen, og at HERREN intet ser.
10 Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwaachilia lakini nitaleta juu ya vichwa vyao, yale waliyoyatenda.”
Derfor viser jeg heller ingen Medynk eller Skaansel, men gengælder dem deres Færd.«
11 Ndipo mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani safi na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja, akarudi na kutoa taarifa akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”
Og se, Manden i det linnede Klædebon og med Skrivetøjet ved Lænden kom tilbage og meldte: »Jeg har gjort, som du bød.«

< Ezekieli 9 >