< Ezekieli 8 >

1 Katika siku ya tano ya mwezi wa sita mwaka wa sita, baada ya kupelekwa uhamishoni nilipokuwa nimeketi katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenyezi ulikuja juu yangu.
Sürgünlüğün altıncı yılı, altıncı ayın beşinci günü evde Yahuda'nın ileri gelenleriyle otururken Egemen RAB'bin eli bana dokundu.
2 Nikatazama, nikaona umbo mfano wa mwanadamu. Kutokana na kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kuelekea chini alifanana na moto. Kuanzia kwenye kiuno kuelekea juu sura yake kama chuma kingʼaavyo kikiwa ndani ya moto.
Baktım, insana benzer birini gördüm: Görünüşü, belinden aşağısı ateşi andırıyor, belinden yukarısı maden gibi ışıldıyordu.
3 Akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono, akaniinua kwa kushika nywele za kichwa changu. Roho akaniinua juu kati ya nchi na mbingu nikiwa katika maono ya Mungu akanichukua mpaka Yerusalemu, kwenye ingilio la lango la upande wa kaskazini ya ukumbi wa ndani, mahali iliposimama ile sanamu ichocheayo wivu.
Eli andıran bir şey uzatıp beni saçlarımdan tuttu. Ruh beni yerle gök arasına kaldırdı ve Tanrı'dan gelen görümlerde Yeruşalim'e, iç avlunun kuzeye bakan kapısının giriş bölümüne götürdü. Tanrı'nın kıskançlığını uyandıran kıskançlık putu orada dikiliydi.
4 Hapo mbele yangu palikuwa na utukufu wa Mungu wa Israeli, kama utukufu ule niliouona katika maono kule ua wa ndani.
Ovada gördüğüm görümdeki gibi, İsrail'in Tanrısı'nın görkemi oradaydı.
5 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, tazama kuelekea kaskazini.” Hivyo nikatazama na kwenye ingilio upande wa kaskazini wa lango la madhabahu, nikaona sanamu hii ya wivu.
Sonra bana, “Ey insanoğlu, kuzeye bak!” dedi. Baktım, sunak kapısının kuzeye bakan giriş bölümünde duran kıskançlık putunu gördüm.
6 Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, je, unaona yale wanayofanya, haya mambo ya machukizo kabisa nyumba ya Israeli wanayotenda hapa, ambayo yatanifanya niende mbali na mahali pangu patakatifu? Lakini utaona vitu ambavyo vinachukiza zaidi hata kuliko hivi.”
Bana, “İnsanoğlu, ne yaptıklarını görüyor musun?” dedi, “Tapınağımdan uzaklaşayım diye İsrail halkı çok iğrenç şeyler yapıyor. Bundan daha iğrenç şeyler göreceksin.”
7 Kisha akanileta mpaka ingilio la ukumbi. Nikatazama, nami nikaona tundu ukutani.
Beni avlunun giriş bölümüne getirdi. Baktım, duvarda bir delik gördüm.
8 Akaniambia, “Mwanadamu, sasa toboa kwenye ukuta huu.” Ndipo nikatoboa ule ukuta, nikaona hapo pana mlango.
Bana, “Haydi duvarı del, insanoğlu” dedi. Duvarı deldim, orada bir kapı gördüm.
9 Naye akaniambia, “Ingia ndani, ukaone maovu na machukizo wanayofanya humu.”
Bana, “İçeri gir de burada yaptıkları kötü ve iğrenç şeyleri gör” dedi.
10 Hivyo nikaingia ndani na kutazama, nikaona kuta zote zimechorwa kila aina ya vitu vitambaavyo na ya wanyama wachukizao wa kila aina na sanamu zote za nyumba ya Israeli.
Böylece içeriye girip baktım. Duvarın her yanına çeşit çeşit sürüngen, iğrenç hayvan şekilleri ve İsrail halkının bütün putları oyulmuştu.
11 Mbele yao walisimama wazee sabini wa nyumba ya Israeli, naye Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja alikuwa na chetezo mkononi na moshi wa harufu nzuri ya uvumba ulikuwa unapanda juu.
İsrail ileri gelenlerinden yetmiş kişiyle Şafan oğlu Yaazanya orada, putların önünde duruyordu. Her birinin elinde bir buhurdan vardı; buhurun kokusu bulut gibi yükseliyordu.
12 Akaniambia, “Mwanadamu, umeona wanayoyafanya wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mmoja kwenye sehemu yake mwenyewe ya kufanyia ibada za sanamu yake? Wao husema, ‘Bwana hatuoni, Bwana ameiacha nchi.’”
“İnsanoğlu, İsrail halkının ileri gelenlerinin kendi putlarının odalarında, karanlıkta neler yaptıklarını gördün mü?” dedi, “Onlar, ‘RAB bizi görmüyor, RAB ülkeyi bıraktı’ diyorlar.”
13 Akasema tena, “Bado utaona machukizo wanayofanya ambayo ni makubwa kuliko haya.”
Bana yine, “Daha iğrenç şeyler yaptıklarını da göreceksin” dedi.
14 Ndipo akanileta mpaka ingilio la lango la kaskazini la nyumba ya Bwana, nami nikaona wanawake wameketi hapo, wakimwombolezea Tamuzi.
Bundan sonra beni RAB'bin Tapınağı'nın kuzeye bakan kapısının giriş bölümüne götürdü. Orada oturup Tammuz için ağlayan kadınları gördüm.
15 Akaniambia, “Unaliona hili, mwanadamu? Utaona vitu ambavyo ni machukizo kuliko hili.”
Bana, “İnsanoğlu, bunu gördün mü? Bundan daha iğrenç şeyler de göreceksin” dedi.
16 Ndipo akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani wa nyumba ya Bwana, nako huko katika ingilio la Hekalu, kati ya baraza na madhabahu, walikuwepo wanaume wapatao ishirini na watano. Wakiwa wamelipa kisogo Hekalu la Bwana na kuelekeza nyuso zao upande wa mashariki, wakilisujudia jua huko mashariki.
Beni RAB'bin Tapınağı'nın iç avlusuna götürdü. Tapınağın girişinde, eyvanla sunak arasında yirmi beş kadar adam vardı. Sırtlarını RAB'bin Tapınağı'na, yüzlerini doğuya dönmüş, güneşe tapınıyorlardı.
17 Akaniambia, “Je, umeona hili mwanadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo wanayoyafanya hapa? Je, ni lazima pia waijaze nchi dhuluma na kuendelea siku zote kunikasirisha? Watazame wanavyonibania pua kana kwamba ninanuka!
Bana, “İnsanoğlu, bunları gördün mü?” dedi, “Yahuda halkı burada yaptığı iğrenç şeyler yetmiyormuş gibi, ülkeyi zorbalıkla doldurup beni sürekli öfkelendiriyor. Bak, dalı nasıl burunlarına uzatıyorlar!
18 Kwa hiyo nitashughulika nao kwa hasira, sitawaonea huruma wala kuwaachilia. Wajapopiga makelele masikioni mwangu, sitawasikiliza.”
Bundan ötürü onlara öfkeyle davranacak, acımayacağım, onları esirgemeyeceğim. Yüksek sesle beni çağırsalar bile onları dinlemeyeceğim.”

< Ezekieli 8 >