< Ezekieli 8 >
1 Katika siku ya tano ya mwezi wa sita mwaka wa sita, baada ya kupelekwa uhamishoni nilipokuwa nimeketi katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenyezi ulikuja juu yangu.
Pripetilo se je v šestem letu, v šestem mesecu, na peti dan meseca, ko sem sedèl v svoji hiši in so starešine Juda sedeli pred menoj, da je tam name padla roka Gospoda Boga.
2 Nikatazama, nikaona umbo mfano wa mwanadamu. Kutokana na kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kuelekea chini alifanana na moto. Kuanzia kwenye kiuno kuelekea juu sura yake kama chuma kingʼaavyo kikiwa ndani ya moto.
Potem sem pogledal in glej, podoba kakor videz ognja. Od videza njenih ledij, celó navzdol, ogenj; in od njenih ledij, celó navzgor, kakor videz sijaja, kot barva jantarja.
3 Akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono, akaniinua kwa kushika nywele za kichwa changu. Roho akaniinua juu kati ya nchi na mbingu nikiwa katika maono ya Mungu akanichukua mpaka Yerusalemu, kwenye ingilio la lango la upande wa kaskazini ya ukumbi wa ndani, mahali iliposimama ile sanamu ichocheayo wivu.
Iztegnil je obliko roke in me prijel za koder moje glave, in duh me je dvignil med zemljo in nebo in me v Božjih videnjih privedel k Jeruzalemu, k durim notranjih velikih vrat, ki gledajo proti severu, kjer je bil sedež podobe ljubosumnosti, ki izziva k ljubosumnosti.
4 Hapo mbele yangu palikuwa na utukufu wa Mungu wa Israeli, kama utukufu ule niliouona katika maono kule ua wa ndani.
Glej, tam je bila slava Izraelovega Boga, glede na videnje, ki sem ga videl na ravnini.
5 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, tazama kuelekea kaskazini.” Hivyo nikatazama na kwenye ingilio upande wa kaskazini wa lango la madhabahu, nikaona sanamu hii ya wivu.
Potem mi je rekel: »Človeški sin, povzdigni sedaj svoje oči proti severu.« Tako sem povzdignil svoje oči proti severu in glej proti severu, pri velikih vratih oltarja, ta podoba ljubosumnosti na vhodu.
6 Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, je, unaona yale wanayofanya, haya mambo ya machukizo kabisa nyumba ya Israeli wanayotenda hapa, ambayo yatanifanya niende mbali na mahali pangu patakatifu? Lakini utaona vitu ambavyo vinachukiza zaidi hata kuliko hivi.”
Nadalje mi je rekel: »Človeški sin, ali vidiš, kaj počno? Celó velike ogabnosti, ki jih Izraelova hiša grešno počenja tukaj, da bi jaz moral oditi daleč proč od svojega svetišča? Toda ponovno se obrni in videl boš večje ogabnosti.«
7 Kisha akanileta mpaka ingilio la ukumbi. Nikatazama, nami nikaona tundu ukutani.
Privedel me je k dvornim vratom in ko sem pogledal, glej, luknja v zidu.
8 Akaniambia, “Mwanadamu, sasa toboa kwenye ukuta huu.” Ndipo nikatoboa ule ukuta, nikaona hapo pana mlango.
Potem mi je rekel: »Človeški sin, koplji sedaj v steno.« In ko sem kopál v steno, sem zagledal vrata.
9 Naye akaniambia, “Ingia ndani, ukaone maovu na machukizo wanayofanya humu.”
In rekel mi je: »Vstopi in poglej zlobne ogabnosti, ki jih tukaj počno.«
10 Hivyo nikaingia ndani na kutazama, nikaona kuta zote zimechorwa kila aina ya vitu vitambaavyo na ya wanyama wachukizao wa kila aina na sanamu zote za nyumba ya Israeli.
Tako sem vstopil in videl; in glej, vsakršne oblike plazečih stvari in gnusnih zveri in vseh malikov Izraelove hiše, upodobljenih po steni naokoli.
11 Mbele yao walisimama wazee sabini wa nyumba ya Israeli, naye Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja alikuwa na chetezo mkononi na moshi wa harufu nzuri ya uvumba ulikuwa unapanda juu.
In tam je pred njimi stalo sedemdeset mož, izmed starcev Izraelove hiše in v njihovi sredi je stal Jaazanjá, sin Šafána. Z vsakim moškim je bila v njegovi roki njegova kadilnica; in gost oblak kadila se je dvigal.
12 Akaniambia, “Mwanadamu, umeona wanayoyafanya wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mmoja kwenye sehemu yake mwenyewe ya kufanyia ibada za sanamu yake? Wao husema, ‘Bwana hatuoni, Bwana ameiacha nchi.’”
Potem mi je rekel: »Človeški sin, ali si videl kaj starci Izraelove hiše počno v temi, vsak mož v sobah svojih podob? Kajti pravijo: › Gospod nas ne vidi; Gospod je zapustil zemljo.‹«
13 Akasema tena, “Bado utaona machukizo wanayofanya ambayo ni makubwa kuliko haya.”
Prav tako mi je rekel: »Ponovno se obrni in videl boš večje ogabnosti, ki jih počno.«
14 Ndipo akanileta mpaka ingilio la lango la kaskazini la nyumba ya Bwana, nami nikaona wanawake wameketi hapo, wakimwombolezea Tamuzi.
Potem me je privedel k durim velikih vrat Gospodove hiše, ki so bila proti severu; in glej, tam so sedele ženske, jokajoče za Tamúzom.
15 Akaniambia, “Unaliona hili, mwanadamu? Utaona vitu ambavyo ni machukizo kuliko hili.”
Potem mi je rekel: »Ali si videl to, oh človeški sin? Ponovno se obrni in videl boš večje ogabnosti, kot so te.«
16 Ndipo akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani wa nyumba ya Bwana, nako huko katika ingilio la Hekalu, kati ya baraza na madhabahu, walikuwepo wanaume wapatao ishirini na watano. Wakiwa wamelipa kisogo Hekalu la Bwana na kuelekeza nyuso zao upande wa mashariki, wakilisujudia jua huko mashariki.
In privedel me je na notranji dvor Gospodove hiše in glej, pri vratih Gospodovega templja, med preddverjem in oltarjem, je bilo okoli petindvajset mož, s svojimi hrbti proti Gospodovemu templju in svojimi obrazi proti vzhodu; in oboževali so sonce proti vzhodu.
17 Akaniambia, “Je, umeona hili mwanadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo wanayoyafanya hapa? Je, ni lazima pia waijaze nchi dhuluma na kuendelea siku zote kunikasirisha? Watazame wanavyonibania pua kana kwamba ninanuka!
Potem mi je rekel: »Si videl to, oh človeški sin? Ali je lahka stvar za Judovo hišo, da zagrešijo ogabnosti, ki jih tukaj zagrešujejo? Kajti deželo so napolnili z nasiljem in vrnili so se, da me izzivajo k jezi. In glej, vejico dajejo pod svoj nos.
18 Kwa hiyo nitashughulika nao kwa hasira, sitawaonea huruma wala kuwaachilia. Wajapopiga makelele masikioni mwangu, sitawasikiliza.”
Zatorej bom tudi jaz postopal v razjarjenosti. Moje oko ne bo prizanašalo niti ne bom imel usmiljenja, in četudi jokajo z močnim glasom v moja ušesa, jih vendar ne bom slišal.«