< Ezekieli 8 >
1 Katika siku ya tano ya mwezi wa sita mwaka wa sita, baada ya kupelekwa uhamishoni nilipokuwa nimeketi katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenyezi ulikuja juu yangu.
Or il arriva en la sixième année, au sixième mois, au cinquième jour du mois, que, lorsque j’étais assis dans ma maison, et que les vieillards de Juda étaient assis devant moi, tomba là sur moi la main du Seigneur Dieu.
2 Nikatazama, nikaona umbo mfano wa mwanadamu. Kutokana na kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kuelekea chini alifanana na moto. Kuanzia kwenye kiuno kuelekea juu sura yake kama chuma kingʼaavyo kikiwa ndani ya moto.
Et je vis, et voilà la ressemblance d’un homme, comme l’aspect d’un feu; de l’aspect de ses reins et au-dessous c’était du feu; et des reins et au-dessus, comme l’aspect d’une splendeur, comme la vue du succin.
3 Akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono, akaniinua kwa kushika nywele za kichwa changu. Roho akaniinua juu kati ya nchi na mbingu nikiwa katika maono ya Mungu akanichukua mpaka Yerusalemu, kwenye ingilio la lango la upande wa kaskazini ya ukumbi wa ndani, mahali iliposimama ile sanamu ichocheayo wivu.
Et la ressemblance d’une main envoyée par cet homme me saisit par une boucle de cheveux de ma tête; et un esprit m’éleva entre le ciel et la terre, et m’amena à Jérusalem dans une vision de Dieu, près de la porte intérieure qui regardait du côté de l’aquilon, où était placée l’idole de la jalousie, pour provoquer la jalousie.
4 Hapo mbele yangu palikuwa na utukufu wa Mungu wa Israeli, kama utukufu ule niliouona katika maono kule ua wa ndani.
Et voici que là était la gloire du Dieu d’Israël, selon la vision que j’avais vue dans la plaine.
5 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, tazama kuelekea kaskazini.” Hivyo nikatazama na kwenye ingilio upande wa kaskazini wa lango la madhabahu, nikaona sanamu hii ya wivu.
Et il me dit: Fils d’un homme, lève tes yeux vers la voie de l’aquilon. Et je levai mes yeux vers la voie de l’aquilon; et voilà que du côté de l’aquilon de la porte de l’autel était l’idole de la jalousie à l’entrée même.
6 Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, je, unaona yale wanayofanya, haya mambo ya machukizo kabisa nyumba ya Israeli wanayotenda hapa, ambayo yatanifanya niende mbali na mahali pangu patakatifu? Lakini utaona vitu ambavyo vinachukiza zaidi hata kuliko hivi.”
Et il me dit: Fils d’un homme, vois-tu, toi, ce que font ceux-ci, les grandes abominations que la maison d’Israël fait ici, afin que je me retire loin de mon sanctuaire? et si tu te tournes encore, tu verras des abominations plus grandes.
7 Kisha akanileta mpaka ingilio la ukumbi. Nikatazama, nami nikaona tundu ukutani.
Et il me conduisit à l’entrée du parvis, et voilà que je vis un trou dans la muraille.
8 Akaniambia, “Mwanadamu, sasa toboa kwenye ukuta huu.” Ndipo nikatoboa ule ukuta, nikaona hapo pana mlango.
Et il me dit: Fils d’un homme, perce la muraille. Et lorsque j’eus percé la muraille, parut une porte.
9 Naye akaniambia, “Ingia ndani, ukaone maovu na machukizo wanayofanya humu.”
Et il me dit: Entre, et vois les abominations horribles que ces gens font ici.
10 Hivyo nikaingia ndani na kutazama, nikaona kuta zote zimechorwa kila aina ya vitu vitambaavyo na ya wanyama wachukizao wa kila aina na sanamu zote za nyumba ya Israeli.
Et étant entré, je vis, et voici que toute sorte d’images de reptiles et d’animaux, l’abomination et toutes les idoles de la maison d’Israël étaient peintes sur la muraille tout autour.
11 Mbele yao walisimama wazee sabini wa nyumba ya Israeli, naye Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja alikuwa na chetezo mkononi na moshi wa harufu nzuri ya uvumba ulikuwa unapanda juu.
Et soixante-dix d’entre les anciens de la maison d’Israël se tenaient debout devant les peintures, et Jézonias, fils de Saphan, était au milieu d’eux; et chacun d’eux avait un encensoir en sa main; et une vapeur comme un nuage s’élevait de l’encens.
12 Akaniambia, “Mwanadamu, umeona wanayoyafanya wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mmoja kwenye sehemu yake mwenyewe ya kufanyia ibada za sanamu yake? Wao husema, ‘Bwana hatuoni, Bwana ameiacha nchi.’”
Et il me dit: Certes tu vois, fils d’un homme, ce que les anciens de la maison d’Israël font dans les ténèbres, chacun dans le secret de sa chambre; car ils disent: Le Seigneur ne nous voit point; le Seigneur a délaissé la terre.
13 Akasema tena, “Bado utaona machukizo wanayofanya ambayo ni makubwa kuliko haya.”
Et il me dit: Si tu te tournes encore, tu verras des abominations plus grandes que celles que ces gens font.
14 Ndipo akanileta mpaka ingilio la lango la kaskazini la nyumba ya Bwana, nami nikaona wanawake wameketi hapo, wakimwombolezea Tamuzi.
Et il me conduisit à l’entrée de la porte de la maison du Seigneur, qui regardait du côté de l’aquilon, et voici que là les femmes étaient assises pleurant Adonis.
15 Akaniambia, “Unaliona hili, mwanadamu? Utaona vitu ambavyo ni machukizo kuliko hili.”
Et il me dit: Certes, tu as vu, fils d’un homme; si tu te tournes encore, tu verras des abominations plus grandes que celles-ci.
16 Ndipo akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani wa nyumba ya Bwana, nako huko katika ingilio la Hekalu, kati ya baraza na madhabahu, walikuwepo wanaume wapatao ishirini na watano. Wakiwa wamelipa kisogo Hekalu la Bwana na kuelekeza nyuso zao upande wa mashariki, wakilisujudia jua huko mashariki.
Et il me conduisit dans le parvis intérieur de la maison du Seigneur; et voilà qu’à l’entrée du temple du Seigneur, entre le vestibule et l’autel, environ vingt-cinq hommes tournant le dos au temple du Seigneur, et la face vers l’orient; et ils adoraient vers le lever du soleil.
17 Akaniambia, “Je, umeona hili mwanadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo wanayoyafanya hapa? Je, ni lazima pia waijaze nchi dhuluma na kuendelea siku zote kunikasirisha? Watazame wanavyonibania pua kana kwamba ninanuka!
Et il me dit: Certes, tu as vu, fils d’un homme; est-ce peu à la maison de Juda d’avoir fait les abominations qu’ils ont faites ici, puisque remplissant la terre d’iniquité, ils se sont appliqués à m’irriter? et voici qu’ils approchent le rameau de leurs narines.
18 Kwa hiyo nitashughulika nao kwa hasira, sitawaonea huruma wala kuwaachilia. Wajapopiga makelele masikioni mwangu, sitawasikiliza.”
Ainsi donc moi aussi j’agirai dans ma fureur; mon œil n’épargnera pas, je n’aurai pas de pitié; et lorsqu’ils crieront à mes oreilles à haute voix, je ne les écouterai point.