< Ezekieli 8 >

1 Katika siku ya tano ya mwezi wa sita mwaka wa sita, baada ya kupelekwa uhamishoni nilipokuwa nimeketi katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenyezi ulikuja juu yangu.
La sixième année, le sixième mois, le cinquième jour du mois, comme j'étais assis dans ma maison, et que les Anciens de Juda étaient assis devant moi, alors la main du Seigneur Éternel descendit sur moi.
2 Nikatazama, nikaona umbo mfano wa mwanadamu. Kutokana na kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kuelekea chini alifanana na moto. Kuanzia kwenye kiuno kuelekea juu sura yake kama chuma kingʼaavyo kikiwa ndani ya moto.
Et je regardai, et voici, c'était une figure ayant l'aspect du feu; depuis ce qui paraissait être ses reins en bas, c'était du feu, et de ses reins en haut, c'était une espèce de splendeur, comme celle de l'airain brillant.
3 Akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono, akaniinua kwa kushika nywele za kichwa changu. Roho akaniinua juu kati ya nchi na mbingu nikiwa katika maono ya Mungu akanichukua mpaka Yerusalemu, kwenye ingilio la lango la upande wa kaskazini ya ukumbi wa ndani, mahali iliposimama ile sanamu ichocheayo wivu.
Et elle étendit la forme d'une main, et me saisit aux boucles de ma chevelure. Puis l'Esprit me souleva entre la terre et le ciel, et me conduisit à Jérusalem, en vision divine, à l'entrée de la porte intérieure, qui donne vers le nord, et où était placée la statue de la jalousie qui provoquait la jalousie [de l'Éternel].
4 Hapo mbele yangu palikuwa na utukufu wa Mungu wa Israeli, kama utukufu ule niliouona katika maono kule ua wa ndani.
Et voici, là se trouvait la gloire du Dieu d'Israël, pareille à la vision que j'en avais eue dans la vallée.
5 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, tazama kuelekea kaskazini.” Hivyo nikatazama na kwenye ingilio upande wa kaskazini wa lango la madhabahu, nikaona sanamu hii ya wivu.
Et Il me dit: Fils de l'homme, lève donc les yeux vers le nord! Et je levai les yeux vers le nord, et voici, au nord de la porte de l'autel, était cette statue de la jalousie, à l'entrée.
6 Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, je, unaona yale wanayofanya, haya mambo ya machukizo kabisa nyumba ya Israeli wanayotenda hapa, ambayo yatanifanya niende mbali na mahali pangu patakatifu? Lakini utaona vitu ambavyo vinachukiza zaidi hata kuliko hivi.”
Et Il me dit: Fils de l'homme, vois-tu ce qu'ils font? Ce sont de grandes abominations que la maison d'Israël fait ici, tellement que je vais m'éloigner de mon sanctuaire. Et tu reverras encore de grandes abominations.
7 Kisha akanileta mpaka ingilio la ukumbi. Nikatazama, nami nikaona tundu ukutani.
Puis Il me conduisit à l'entrée du parvis, et je regardai, et voici, il y avait un trou dans le mur.
8 Akaniambia, “Mwanadamu, sasa toboa kwenye ukuta huu.” Ndipo nikatoboa ule ukuta, nikaona hapo pana mlango.
Et Il me dit: Fils de l'homme, perce donc la muraille! Et je perçai la muraille et voici, il y avait une porte.
9 Naye akaniambia, “Ingia ndani, ukaone maovu na machukizo wanayofanya humu.”
Et Il me dit: Entre, et vois les abominations odieuses qu'ils font là!
10 Hivyo nikaingia ndani na kutazama, nikaona kuta zote zimechorwa kila aina ya vitu vitambaavyo na ya wanyama wachukizao wa kila aina na sanamu zote za nyumba ya Israeli.
Alors j'entrai et je regardai, et voici, c'étaient toutes sortes d'images de reptiles et d'animaux immondes, et toutes les espèces d'idoles de la maison d'Israël, dessinées sur la muraille tout à l'entour.
11 Mbele yao walisimama wazee sabini wa nyumba ya Israeli, naye Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja alikuwa na chetezo mkononi na moshi wa harufu nzuri ya uvumba ulikuwa unapanda juu.
Et soixante-dix hommes d'entre les Anciens de la maison d'Israël, entre autres Jaasénia, fils de Schaphan, debout au milieu d'eux, se tenaient devant elles, chacun son encensoir à la main, et le parfum d'un nuage d'encens s'élevait.
12 Akaniambia, “Mwanadamu, umeona wanayoyafanya wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mmoja kwenye sehemu yake mwenyewe ya kufanyia ibada za sanamu yake? Wao husema, ‘Bwana hatuoni, Bwana ameiacha nchi.’”
Et Il me dit: Vois-tu, fils de l'homme, ce que les Anciens de la maison d'Israël font dans les ténèbres, chacun dans leurs chambres couvertes de peintures! Car ils disent: L'Éternel ne nous voit pas! l'Éternel a abandonné le pays.
13 Akasema tena, “Bado utaona machukizo wanayofanya ambayo ni makubwa kuliko haya.”
Et Il me dit: Tu reverras encore les grandes abominations qu'ils commettent.
14 Ndipo akanileta mpaka ingilio la lango la kaskazini la nyumba ya Bwana, nami nikaona wanawake wameketi hapo, wakimwombolezea Tamuzi.
Puis Il me conduisit à l'entrée de la porte de la maison de l'Éternel, qui est du côté du nord, et voici, là se trouvaient assises les femmes, pleurant Thammuz.
15 Akaniambia, “Unaliona hili, mwanadamu? Utaona vitu ambavyo ni machukizo kuliko hili.”
Et Il me dit: As-tu vu, fils de l'homme? Tu reverras encore des abominations plus grandes que celles-là.
16 Ndipo akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani wa nyumba ya Bwana, nako huko katika ingilio la Hekalu, kati ya baraza na madhabahu, walikuwepo wanaume wapatao ishirini na watano. Wakiwa wamelipa kisogo Hekalu la Bwana na kuelekeza nyuso zao upande wa mashariki, wakilisujudia jua huko mashariki.
Alors Il me conduisit dans le parvis intérieur de la maison de l'Éternel, et voici, à l'entrée du temple de l'Éternel, entre le portique et l'autel, étaient environ vingt-cinq hommes, tournant le dos au temple de l'Éternel, et le visage du côté de l'orient: et ils adoraient à l'orient le Soleil.
17 Akaniambia, “Je, umeona hili mwanadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo wanayoyafanya hapa? Je, ni lazima pia waijaze nchi dhuluma na kuendelea siku zote kunikasirisha? Watazame wanavyonibania pua kana kwamba ninanuka!
Et Il me dit: As-tu vu, fils de l'homme? Est-ce trop peu pour la maison de Juda de faire les abominations qu'ils font ici, qu'ils remplissent encore le pays de violences, et qu'ils reviennent toujours à m'irriter? Et voici, ils tiennent le rameau contre leur nez.
18 Kwa hiyo nitashughulika nao kwa hasira, sitawaonea huruma wala kuwaachilia. Wajapopiga makelele masikioni mwangu, sitawasikiliza.”
Mais moi aussi j'agirai dans ma colère; je serai sans pitié et sans miséricorde; et quand ils crieront à mes oreilles à haute voix, je ne les entendrai pas.

< Ezekieli 8 >