< Ezekieli 8 >

1 Katika siku ya tano ya mwezi wa sita mwaka wa sita, baada ya kupelekwa uhamishoni nilipokuwa nimeketi katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenyezi ulikuja juu yangu.
La sixième année, au sixième mois, le cinquième jour du mois, comme j'étais assis dans ma maison, et que les anciens de Juda étaient assis devant moi, la main du Seigneur Yahvé tomba là sur moi.
2 Nikatazama, nikaona umbo mfano wa mwanadamu. Kutokana na kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kuelekea chini alifanana na moto. Kuanzia kwenye kiuno kuelekea juu sura yake kama chuma kingʼaavyo kikiwa ndani ya moto.
Alors je vis, et voici, une ressemblance comme l'apparence du feu - depuis l'apparence de sa taille et en bas, du feu, et depuis sa taille et en haut, comme l'apparence de l'éclat, comme du métal incandescent.
3 Akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono, akaniinua kwa kushika nywele za kichwa changu. Roho akaniinua juu kati ya nchi na mbingu nikiwa katika maono ya Mungu akanichukua mpaka Yerusalemu, kwenye ingilio la lango la upande wa kaskazini ya ukumbi wa ndani, mahali iliposimama ile sanamu ichocheayo wivu.
L'Esprit m'éleva entre la terre et le ciel, et me conduisit, dans les visions de Dieu, à Jérusalem, à l'entrée de la porte du parvis intérieur, du côté du nord, où se trouvait le siège de l'image de la jalousie, qui excite la jalousie.
4 Hapo mbele yangu palikuwa na utukufu wa Mungu wa Israeli, kama utukufu ule niliouona katika maono kule ua wa ndani.
Et voici, la gloire du Dieu d'Israël était là, selon l'aspect que j'avais vu dans la plaine.
5 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, tazama kuelekea kaskazini.” Hivyo nikatazama na kwenye ingilio upande wa kaskazini wa lango la madhabahu, nikaona sanamu hii ya wivu.
Et il me dit: « Fils d'homme, lève les yeux, maintenant, sur le chemin du nord. » Je levai les yeux vers le nord, et je vis, au nord de la porte de l'autel, cette image de la jalousie dans l'entrée.
6 Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, je, unaona yale wanayofanya, haya mambo ya machukizo kabisa nyumba ya Israeli wanayotenda hapa, ambayo yatanifanya niende mbali na mahali pangu patakatifu? Lakini utaona vitu ambavyo vinachukiza zaidi hata kuliko hivi.”
Il me dit: « Fils d'homme, vois-tu ce qu'ils font? Même les grandes abominations que la maison d'Israël commet ici, pour que je m'éloigne de mon sanctuaire? Mais tu verras encore d'autres grandes abominations. »
7 Kisha akanileta mpaka ingilio la ukumbi. Nikatazama, nami nikaona tundu ukutani.
Il me conduisit à l'entrée du parvis; et quand je regardai, voici, il y avait un trou dans la muraille.
8 Akaniambia, “Mwanadamu, sasa toboa kwenye ukuta huu.” Ndipo nikatoboa ule ukuta, nikaona hapo pana mlango.
Il me dit alors: « Fils d'homme, creuse maintenant dans la muraille. » Quand j'ai creusé dans le mur, j'ai vu une porte.
9 Naye akaniambia, “Ingia ndani, ukaone maovu na machukizo wanayofanya humu.”
Il me dit: « Entre, et vois les méchantes abominations qu'ils commettent ici. »
10 Hivyo nikaingia ndani na kutazama, nikaona kuta zote zimechorwa kila aina ya vitu vitambaavyo na ya wanyama wachukizao wa kila aina na sanamu zote za nyumba ya Israeli.
J'entrai donc et je regardai, et je vis toutes sortes de reptiles, d'animaux abominables et toutes les idoles de la maison d'Israël, représentées sur la muraille.
11 Mbele yao walisimama wazee sabini wa nyumba ya Israeli, naye Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja alikuwa na chetezo mkononi na moshi wa harufu nzuri ya uvumba ulikuwa unapanda juu.
Soixante-dix hommes parmi les anciens de la maison d'Israël se tenaient devant eux. Au milieu d'eux se tenait Jaazania, fils de Shaphan, chacun ayant son encensoir à la main; et l'odeur de la nuée d'encens montait.
12 Akaniambia, “Mwanadamu, umeona wanayoyafanya wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mmoja kwenye sehemu yake mwenyewe ya kufanyia ibada za sanamu yake? Wao husema, ‘Bwana hatuoni, Bwana ameiacha nchi.’”
Alors il me dit: « Fils d'homme, as-tu vu ce que font dans l'obscurité les anciens de la maison d'Israël, chacun dans sa chambre d'images? Car ils disent: « Yahvé ne nous voit pas. L'Éternel a abandonné le pays. »
13 Akasema tena, “Bado utaona machukizo wanayofanya ambayo ni makubwa kuliko haya.”
Il me dit aussi: « Tu verras encore une fois les grandes abominations qu'ils commettent. »
14 Ndipo akanileta mpaka ingilio la lango la kaskazini la nyumba ya Bwana, nami nikaona wanawake wameketi hapo, wakimwombolezea Tamuzi.
Et il me conduisit à l'entrée de la porte de la maison de l'Éternel, qui était du côté du nord; et je vis les femmes assises là, pleurant sur Tammuz.
15 Akaniambia, “Unaliona hili, mwanadamu? Utaona vitu ambavyo ni machukizo kuliko hili.”
Et il me dit: « As-tu vu cela, fils d'homme? Tu verras encore de plus grandes abominations que celles-ci. »
16 Ndipo akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani wa nyumba ya Bwana, nako huko katika ingilio la Hekalu, kati ya baraza na madhabahu, walikuwepo wanaume wapatao ishirini na watano. Wakiwa wamelipa kisogo Hekalu la Bwana na kuelekeza nyuso zao upande wa mashariki, wakilisujudia jua huko mashariki.
Il me conduisit dans le parvis intérieur de la maison de l'Éternel, et je vis à l'entrée du temple de l'Éternel, entre le portique et l'autel, environ vingt-cinq hommes qui tournaient le dos au temple de l'Éternel et le visage vers l'orient. Ils adoraient le soleil vers l'est.
17 Akaniambia, “Je, umeona hili mwanadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo wanayoyafanya hapa? Je, ni lazima pia waijaze nchi dhuluma na kuendelea siku zote kunikasirisha? Watazame wanavyonibania pua kana kwamba ninanuka!
Puis il me dit: « As-tu vu cela, fils de l'homme? Est-ce une chose légère pour la maison de Juda que de commettre les abominations qu'elle commet ici? Car ils ont rempli le pays de violence, et ils se sont retournés pour m'irriter. Voici, ils portent la branche à leur nez.
18 Kwa hiyo nitashughulika nao kwa hasira, sitawaonea huruma wala kuwaachilia. Wajapopiga makelele masikioni mwangu, sitawasikiliza.”
C'est pourquoi j'agirai aussi avec colère. Mon œil n'épargnera pas, je n'aurai pas de pitié. Même s'ils crient à mes oreilles d'une voix forte, je ne les écouterai pas. »

< Ezekieli 8 >