< Ezekieli 8 >
1 Katika siku ya tano ya mwezi wa sita mwaka wa sita, baada ya kupelekwa uhamishoni nilipokuwa nimeketi katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu, mkono wa Bwana Mwenyezi ulikuja juu yangu.
So it came about in the sixth year and the sixth month, in the fifth day of the month, as I sat in my house and the elders of Judah sat before me, that the hand of the Lord Yahweh again fell upon me there.
2 Nikatazama, nikaona umbo mfano wa mwanadamu. Kutokana na kile kilichoonekana kuwa kiuno chake kuelekea chini alifanana na moto. Kuanzia kwenye kiuno kuelekea juu sura yake kama chuma kingʼaavyo kikiwa ndani ya moto.
So I looked, and behold, there was a likeness with the appearance of a man. From the appearance of his hips downward there was fire. And from his hips upward there was the appearance of something shining, like glowing metal.
3 Akanyoosha kitu kilichoonekana kama mkono, akaniinua kwa kushika nywele za kichwa changu. Roho akaniinua juu kati ya nchi na mbingu nikiwa katika maono ya Mungu akanichukua mpaka Yerusalemu, kwenye ingilio la lango la upande wa kaskazini ya ukumbi wa ndani, mahali iliposimama ile sanamu ichocheayo wivu.
Then he reached out the form of a hand and took me by the hair of my head; the Spirit lifted me up between earth and heaven, and in visions from God, he brought me to Jerusalem, to the entrance of the inner northern gate, where the idol that provokes great jealousy was standing.
4 Hapo mbele yangu palikuwa na utukufu wa Mungu wa Israeli, kama utukufu ule niliouona katika maono kule ua wa ndani.
Then behold, the glory of the God of Israel was there, according to the vision I had seen on the plain.
5 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, tazama kuelekea kaskazini.” Hivyo nikatazama na kwenye ingilio upande wa kaskazini wa lango la madhabahu, nikaona sanamu hii ya wivu.
Then he said to me, “Son of man, lift up your eyes to the north.” So I lifted up my eyes to the north, and to the north of the gate leading to the altar, there in the entrance, was the idol of jealousy.
6 Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, je, unaona yale wanayofanya, haya mambo ya machukizo kabisa nyumba ya Israeli wanayotenda hapa, ambayo yatanifanya niende mbali na mahali pangu patakatifu? Lakini utaona vitu ambavyo vinachukiza zaidi hata kuliko hivi.”
So he said to me, “Son of man, do you see what they are doing? These are great abominations that the house of Israel is doing here to make me go far from my own sanctuary. But you will turn and see even greater abominations.”
7 Kisha akanileta mpaka ingilio la ukumbi. Nikatazama, nami nikaona tundu ukutani.
Then he brought me to the doorway of the courtyard, and I looked, and there was a hole in the wall.
8 Akaniambia, “Mwanadamu, sasa toboa kwenye ukuta huu.” Ndipo nikatoboa ule ukuta, nikaona hapo pana mlango.
He said to me, “Son of man, dig into this wall.” So I dug into the wall, and there was a door.
9 Naye akaniambia, “Ingia ndani, ukaone maovu na machukizo wanayofanya humu.”
Then he said to me, “Go and see the wicked abominations that they are doing here.”
10 Hivyo nikaingia ndani na kutazama, nikaona kuta zote zimechorwa kila aina ya vitu vitambaavyo na ya wanyama wachukizao wa kila aina na sanamu zote za nyumba ya Israeli.
So I went in and looked, and behold! There was every form of creeping thing and detestable beast! Every idol of the house of Israel was carved into the wall all around.
11 Mbele yao walisimama wazee sabini wa nyumba ya Israeli, naye Yaazania mwana wa Shafani alikuwa amesimama miongoni mwao. Kila mmoja alikuwa na chetezo mkononi na moshi wa harufu nzuri ya uvumba ulikuwa unapanda juu.
Seventy elders of the house of Israel were there, and Jaazaniah son of Shaphan was standing in their midst. They were standing in front of the images, and each man had his censer in his hand so that the smell of the cloud of incense went up.
12 Akaniambia, “Mwanadamu, umeona wanayoyafanya wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mmoja kwenye sehemu yake mwenyewe ya kufanyia ibada za sanamu yake? Wao husema, ‘Bwana hatuoni, Bwana ameiacha nchi.’”
He said to me, “Son of man, do you see what the elders of the house of Israel are doing in the dark? Each one does this in the hidden chamber of his idol, for they say, 'Yahweh does not see us! Yahweh has forsaken the land.'”
13 Akasema tena, “Bado utaona machukizo wanayofanya ambayo ni makubwa kuliko haya.”
Then he said to me, “Turn again and see the other great abominations that they are doing.”
14 Ndipo akanileta mpaka ingilio la lango la kaskazini la nyumba ya Bwana, nami nikaona wanawake wameketi hapo, wakimwombolezea Tamuzi.
Next he brought me to the entrance of the gate of Yahweh's house that was on the north side, and behold! The women were sitting there mourning for Tammuz.
15 Akaniambia, “Unaliona hili, mwanadamu? Utaona vitu ambavyo ni machukizo kuliko hili.”
So he said to me, “Do you see this, son of man? Turn again and see even greater abominations than these.”
16 Ndipo akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani wa nyumba ya Bwana, nako huko katika ingilio la Hekalu, kati ya baraza na madhabahu, walikuwepo wanaume wapatao ishirini na watano. Wakiwa wamelipa kisogo Hekalu la Bwana na kuelekeza nyuso zao upande wa mashariki, wakilisujudia jua huko mashariki.
He brought me into the inner courtyard of Yahweh's house, and behold! at the entrance of the temple of Yahweh between the portico and the altar, there were about twenty-five men with their backs toward the temple of Yahweh and their faces toward the east, and they were worshiping the sun.
17 Akaniambia, “Je, umeona hili mwanadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo wanayoyafanya hapa? Je, ni lazima pia waijaze nchi dhuluma na kuendelea siku zote kunikasirisha? Watazame wanavyonibania pua kana kwamba ninanuka!
He said to me, “Do you see this, son of man? Is it a little thing for the house of Judah to do these abominations that they are doing here? For they have filled the land with violence and they have turned again to provoke me to anger, putting the branch to their noses.
18 Kwa hiyo nitashughulika nao kwa hasira, sitawaonea huruma wala kuwaachilia. Wajapopiga makelele masikioni mwangu, sitawasikiliza.”
So I will also act among them; my eye will not have compassion, and I will not spare them. Though they cry in my ears with a loud voice, I will not hear them.”