< Ezekieli 5 >
1 “Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
And thou, son of man, take thee a sharp instrument, even a barber's razor, and cause it to pass upon thy head and thy beard; and take thee weighing-balances, and divide the hair.
2 Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
A third part shalt thou burn with fire in the midst of the city, when the days of the siege are fulfilled; and thou shalt take a third part and smite it round about with the sword; and a third part shalt thou scatter in the wind, and I will draw out a sword after them.
3 Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
Thou shalt also take thereof a small number, and bind them in thy skirts.
4 Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
And of these again take some and cast them into the fire, and burn them in the fire. From them shall a fire come forth upon the whole house of Israel.
5 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
Thus saith the Lord Jehovah: This is Jerusalem; in the midst of the nations have I set her, and countries are round about her.
6 Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
But she hath wickedly resisted my ordinances more than the nations, and my statutes more than the countries, that are round about her. For they have refused my ordinances, and have not walked in my statutes.
7 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
Therefore thus saith the Lord Jehovah: Because ye have been rebellious more than the nations that are round about you, and have not walked in my statutes, nor kept my ordinances, but have done according to the ordinances of the nations which are round about you,
8 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
therefore thus saith the Lord Jehovah: Behold I, even I, am against thee, and will execute judgments against thee in the sight of the nations.
9 Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
I will do to thee that which I have not yet done, and the like of which I shall not do again, because of all thine iniquities.
10 Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
Therefore the fathers shall eat the sons in the midst of thee, and the sons shall eat their fathers; and I will execute judgments in thee, and I will scatter the whole remnant of thee to all the winds.
11 Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
Therefore, as I live, saith the Lord Jehovah, because thou hast polluted my sanctuary with all thy detestable things, and with all thine abominations, therefore will I also withdraw mine eye from thee; neither will I spare, neither will I have any pity.
12 Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
A third part of thee shall die by the pestilence, or be consumed with hunger in the midst of thee; and a third part shall die by the sword round about thee; and a third part will I scatter to all the winds, and I will draw out a sword after them.
13 “Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
Thus shall mine anger be accomplished, and I will satiate my fury upon them, and receive satisfaction; and they shall know that I, Jehovah, have spoken it in my zeal, when I shall have accomplished my fury upon them.
14 “Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
Moreover, I will make thee a waste, and a reproach among the nations that are round about thee, in the sight of all that pass by.
15 Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
And thou shalt be a reproach, and a reviling, and a warning, and an astonishment to the nations that are round about thee, when I shall execute judgments upon thee in anger, and in fury, and in furious rebukes; —I, Jehovah, have spoken it; —
16 Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
when I shall send upon you the evil arrows of famine which bring destruction, which I send to destroy you, and increase the famine upon you, and break your staff of bread.
17 Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”
And I will send upon you famine, and evil beasts, which shall make thee childless; and pestilence and blood shall pass through thee; and the sword will I bring upon thee. I, Jehovah, have spoken it.