< Ezekieli 5 >

1 “Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
“And you, son of man, take a sharp weapon for yourself, take the barber’s razor for yourself, and you have caused [it] to pass over your head, and over your beard, and you have taken weighing scales for yourself, and apportioned them.
2 Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
You burn a third part with fire in the midst of the city, at the fullness of the days of the siege; and you have taken the third part, you strike with a weapon around it; and the third part you scatter to the wind, and I draw out a weapon after them.
3 Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
And you have taken there a few in number—and have bound them in your skirts;
4 Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
and you take of them again, and have cast them into the midst of the fire, and have burned them in the fire—out of it comes forth a fire to all the house of Israel.”
5 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
Thus said Lord YHWH: “This [is] Jerusalem, I have set her in the midst of the nations, And the lands [are] around her.
6 Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
And she changes My judgments into wickedness more than the nations, And My statutes more than the lands that [are] around her, For they have kicked against My judgments, And My statutes—they have not walked in them.”
7 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
Therefore, thus said Lord YHWH: “Because of your multiplying above the nations that [are] around you, You have not walked in My statutes, And you have not done My judgments, According to the judgments of the nations that [are] around you, you have not done.”
8 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
Therefore, thus said Lord YHWH: “Behold, I [am] against you, even I, And I have done judgments in your midst, Before the eyes of the nations.
9 Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
And I have done in you that which I have not done, And the like of which I do not do again, Because of all your abominations.
10 Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
Therefore fathers eat sons in your midst, And sons eat their fathers, And I have done judgments in you, And have scattered all your remnant to every wind.
11 Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
Therefore, [as] I live,” a declaration of Lord YHWH, “Because you have defiled My sanctuary With all your detestable things, And with all your abominations, Therefore I also diminish you, And My eye does not pity, and I do not spare.
12 Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
Your third part dies by pestilence, And are consumed by famine in your midst, And the third part fall by sword around you, And the third part I scatter to every wind, And I draw out a sword after them.
13 “Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
And My anger has been completed, And I have caused My fury to rest on them, And I have been comforted, And they have known that I, YHWH, have spoken in My zeal, In My completing My fury on them.
14 “Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
And I give you for a ruin, And for a reproach among nations that [are] around you, Before the eyes of everyone passing by.
15 Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
And it has been a reproach and a reviling, An instruction and an astonishment, To nations that [are] around you, In My doing judgments in you, In anger and fury, and in furious reproofs, I, YHWH, have spoken.
16 Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
In My sending the evil arrows of famine among them, That have been for destruction, That I send to destroy you, And I am adding famine on you, And I have broken your staff of bread.
17 Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”
And I have sent famine and evil beasts on you, And they have bereaved you, And pestilence and blood pass over on you, And I bring a sword in against you, I, YHWH, have spoken!”

< Ezekieli 5 >