< Ezekieli 5 >

1 “Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
Og du Menneskesøn tag dig et skarbt sværd, brug det som Ragekniv og lad det gå over dit Hoved og dit Skæg; tag dig så en Vægtskål og del Håret.
2 Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
En Tredjedel skal du brænde i et Bål midt i Byen, når Belejringens Dage er omme; en Tredjedel skal du tage og slå den med Sværdet rundt om Byen; og en Tredjedel skal du sprede for Vinden; så drager jeg Sværdet bag dem.
3 Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
Derefter skal du tage lidt deraf og svøbe det ind i din kappeflig;
4 Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
og deraf skal du atter tage noget og kaste det midt ind i Ilden og brænde det. Og du skal sige til hele Israels Hus:
5 “Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
Så siger den Herre HERREN: Dette er Jerusalem; jeg satte det midt iblandt Folkene, omgivet af lande.
6 Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
Men det var gudløst og genstridigt mod mine Lovbud mere end Folkene og mod mine Vedtægter mere end Landene rundt om; thi de lod hånt om mine Lovbud og vandrede ikke efter mine Vedtægter.
7 “Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
Derfor, så siger den Herre HERREN: Fordi I var mere genstridige end Folkene rundt om og ikke vandrede efter mine Vedtægter eller holdt mine Lovbud, men gjorde efter de omboende Folks Lovbud,
8 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
derfor, så siger den Herre HERREN: Se, jeg kommer over dig og holder Dom i din Midte for Folkenes Øjne.
9 Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
For alle dine Vederstyggeligheders Skyld vil jeg gøre med dig, hvad jeg aldrig har gjort og aldrig vil gøre Mage til.
10 Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
Derfor skal Fædre æde deres Børn i din Midte og Børn deres Fædre; jeg holder Dom over dig, og alle, som er til Rest i dig, spreder jeg for alle Vinde.
11 Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
Derfor, så sandt jeg lever, lyder det fra den Herre HERREN: Sandelig, fordi du gjorde min Helligdom uren med alle dine væmmelige Guder og Vederstyggeligheder, vil jeg også støde dig fra mig uden Medynk eller Skånsel.
12 Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
En Tredjedel af dig skal dø af Pest og omkomme af Hunger i din Midte, en Tredjedel skal falde for Sværdet rundt om dig, og en Tredjedel spreder jeg for alle Vinde og drager Sværdet bag dem.
13 “Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
Min Vrede skal udtømme sig, og jeg vil køle min Harme på dem og tage Hævn, så de skal kende at jeg, HERREN, har talet i min Nidkærhed, når jeg udtømmer min Vrede over dem.
14 “Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
Jeg gør dig til en Grushob og til Spot blandt Folkene rundt om, for Øjnene af enhver, som drager forbi.
15 Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
Du skal blive til Spot og Hån, til Advarsel og Rædsel for Folkene rundt om, når jeg holder Dom over dig i Vrede og Harme og harm fuld Revselse. Jeg, HERREN, har talet!
16 Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
Når jeg sender Hungerens onde Pile mod eder, og de, som jeg sender for af ødelægge eder, volder Ødelæggelse, og jeg lader Hungeren tage til, da sønderbryder jeg Brødets Støttestav for eder
17 Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”
og sender Hunger over eder og Rovdyr, som skal affolke dig; Pest og Blodsudgydelse skal hjemsøge dig, og jeg bringer Sværd over dig. Jeg, HERREN, har talet.

< Ezekieli 5 >