< Ezekieli 47 >

1 Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la Hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha Hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa Hekalu ulielekea mashariki). Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa Hekalu, kusini mwa madhabahu.
آن مرد بار دیگر مرا به راه ورودی خانهٔ خدا آورد. دیدم رودخانه‌ای از زیر آستانهٔ خانهٔ خدا به طرف مشرق جاری است و از سمت راست خانه، یعنی از سمت جنوبی قربانی می‌گذرد.
2 Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini.
سپس، مرا از راه دروازهٔ شمالی از حیاط بیرون آورد و از آنجا دور زده، به دروازهٔ شرقی حیاط بیرونی رفتیم. در آنجا دیدم آب رودخانه از سمت جنوبی دروازهٔ شرقی جاری بود.
3 Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000 kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
آن مرد با چوب اندازه‌گیری خود پانصد متر در طول رودخانه به طرف شرق اندازه گرفت و در آنجا مرا با خود از آب عبور داد. آب در این نقطه از رودخانه به قوزک پایم می‌رسید.
4 Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni.
پانصد متر دیگر در طول رودخانه اندازه گرفت و باز به من گفت که از آن عبور کنم. این دفعه آب تا زانویم می‌رسید.
5 Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kuvuka.
پانصد متر دورتر از آن آب تا کمرم می‌رسید. پانصد متر دیگر پیمود و این بار رودخانه به قدری عمیق بود که نمی‌توانستم از آن عبور کنم و مجبور بودم شناکنان از آن بگذرم.
6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.
او به من گفت آنچه را که دیده‌ام به خاطر بسپارم؛ بعد مرا از کنار آن رودخانه بازگرداند.
7 Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto.
به هنگام بازگشت دیدم در دو طرف رودخانه درختان زیادی سبز شده‌اند!
8 Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Araba, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Bahari, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi.
او به من گفت: «این رودخانه از میان بیابان و درهٔ اردن به سمت شرق جاری است و به دریای مرده می‌ریزد و در آنجا آبهای شور را شفا می‌دهد و آنها را پاک و گوارا می‌گرداند.
9 Popote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako.
هر چیزی که با آب این رودخانه تماس پیدا کند، زنده می‌شود. ماهیان دریای مرده بی‌نهایت زیاد می‌شوند، چون آبهایش شفا می‌یابند. به هر جا که این آب جاری شود، در آنجا حیات پدید می‌آورد.
10 Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuu
ماهیگیران در ساحل دریای مرده می‌ایستند و از عین جدی تا عین عجلایم مشغول ماهیگیری می‌شوند. ساحل آن پر از تورهای ماهیگیری خواهد شد که برای خشک شدن، آنها را جلوی آفتاب پهن کرده‌اند. دریای مرده مثل دریای مدیترانه از انواع ماهیها پر خواهد شد.
11 Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi.
ولی مردابها و باتلاقهایش شفا نخواهند یافت، بلکه همان‌طور شور باقی خواهند ماند.
12 Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za mto huu. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.”
در سواحل دریای مرده انواع درختان میوه خواهند رویید که برگهایشان هرگز پژمرده نخواهند شد و درختان همیشه پر میوه خواهند بود و هر ماه محصول تازه به بار خواهند آورد، چون با آب رودخانه‌ای که از خانهٔ خدا جاری است، آبیاری خواهند شد. میوهٔ آنها خوراک مقوی و برگهای آنها شفابخش خواهد بود.»
13 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu.
خداوند یهوه می‌فرماید: «سرزمین اسرائیل باید به این ترتیب میان دوازده قبیلهٔ اسرائیل تقسیم شود: به قبیلهٔ یوسف (افرایم و منسی) دو قسمت داده شود،
14 Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu.
ولی به هر یک از قبیله‌های دیگر یک قسمت به طور مساوی داده شود. من برای پدرانتان قسم خورده بودم که این زمین را به ایشان بدهم، پس، حال، این زمین ملک شما خواهد بود.
15 “Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo-Hamathi hadi maingilio ya Sedadi.
«مرز شمالی از دریای مدیترانه تا شهر حتلون و از آنجا تا گذرگاه حمات و از آنجا تا شهر صدد ادامه می‌یابد،
16 Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi), hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani.
سپس به سمت بیروته و سبرایم که در مرز میان دمشق و حمات قرار دارند پیش می‌رود و به شهر تیکن که در سرحد حوران است، ختم می‌شود.
17 Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasar-Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini.
پس مرز شمالی از دریای مدیترانه تا شهر عینون در شرق خواهد بود و حمات و دمشق در شمال آن قرار خواهند داشت.
18 Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi bahari ya mashariki na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki.
«مرز شرقی، از شهر عینون تا کوه حوران خواهد بود. سپس از آنجا به سمت غرب پیچیده در دماغهٔ جنوبی دریای جلیل به رود اردن می‌رسد. از آنجا در امتداد رود اردن پیش می‌رود و از کنار دریای مرده گذشته به تامار می‌رسد و اسرائیل را از جلعاد جدا می‌کند. زمین حوران، دمشق و جلعاد در شرق آن قرار خواهند داشت.
19 Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba-Kadeshi, kisha utaambaa na Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini.
«مرز جنوبی از تامار تا چشمه‌های مریبوت قادش کشیده شده، از آنجا در مسیر رودخانهٔ مرزی مصر امتداد یافته، به دریای مدیترانه می‌رسد.
20 Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo-Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi.
«مرز غربی از انتهای مرز جنوبی آغاز شده در امتداد دریای مدیترانه ادامه می‌یابد و به مرز شمالی ختم می‌شود.
21 “Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli.
«زمین محدود میان این مرزها باید بین قبایل اسرائیل تقسیم شود.
22 Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.
زمین را چون یک ارث برای خودتان و برای غریبان و خانواده‌های ایشان که در میان شما هستند، تقسیم نمایید. آنها باید از همان حقوق و مزایای شما اسرائیلی‌ها برخوردار باشند.
23 Katika kabila lolote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema Bwana Mwenyezi.
سهم این غریبه‌ها باید از زمینهای قبیله‌ای که در آن زندگی می‌کنند، به ایشان داده شود. این را من که خداوند یهوه هستم گفته‌ام.»

< Ezekieli 47 >