< Ezekieli 47 >

1 Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la Hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha Hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa Hekalu ulielekea mashariki). Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa Hekalu, kusini mwa madhabahu.
Ensuite il me ramena à la porte de la maison: et voici, de l'eau jaillissait sous le seuil de la maison du côté de l'orient, car la façade de la maison était tournée à l'orient; et l'eau descendait par dessous le côté droit de la maison au midi de l'autel.
2 Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini.
Et il m'emmena par la porte du nord, et il me fit traverser en dehors jusqu'à la porte extérieure par le chemin qui avait la direction de l'orient, et voici, l'eau jaillissait du côté droit.
3 Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000 kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
Quand l'homme sortit du côté de l'orient, il avait un cordeau en sa main, et il mesura mille coudées, et il me fit traverser l'eau, et l'eau me mouillait les extrémités.
4 Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni.
Puis il mesura mille coudées et me fit traverser l'eau, et j'avais de l'eau jusqu'aux genoux. Ensuite il mesura mille coudées, et me fit traverser, et j'avais de l'eau jusqu'aux reins.
5 Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kuvuka.
Et il mesura encore mille coudées; c'était une rivière que je ne pouvais traverser, car l'eau était profonde; c'était une eau où l'on pouvait nager, un torrent que l'on ne pouvait passer.
6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.
Et il me dit: As-tu vu, fils de l'homme? et il me ramena au bord de la rivière.
7 Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto.
Y étant revenu, je vis sur le bord de la rivière des arbres en très grand nombre d'un côté et de l'autre.
8 Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Araba, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Bahari, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi.
Et il me dit: Cette eau s'écoulera du côté du canton oriental, descendra dans la plaine et se jettera dans la mer: c'est dans la mer qu'elle se jettera, et les eaux de la mer seront rendues saines.
9 Popote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako.
Et toutes les espèces des êtres animés qui se meuvent, vivront partout où coulera la rivière; et il y aura des poissons en très grand nombre; car si cette eau arrive quelque part, tout sera sain et vivant partout où pénétrera la rivière:
10 Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuu
et des pêcheurs s'y tiendront, d'En-Gueddi à En-Eglaïm étendant leurs filets; il y aura des poissons d'espèces diverses, pareils aux poissons de la grande mer et en très grand nombre.
11 Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi.
Ses marais et ses lagunes ne seront point assainis; ils sont abandonnés au sel.
12 Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za mto huu. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.”
Et sur la rivière, sur ses bords de part et d'autre, croîtront toutes sortes d'arbres fruitiers; leur feuillage ne se flétrira point, et leurs fruits ne s'épuiseront point; tous les mois ils mûriront, parce que leurs eaux sortiront du sanctuaire; et leurs fruits seront une nourriture, et leurs feuilles un médicament.
13 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu.
Ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Voici les limites d'après lesquelles vous partagerez le pays entre les douze tribus d'Israël: pour Joseph, deux parts;
14 Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu.
d'ailleurs vos lots seront égaux pour l'un comme pour l'autre. Car de ma main levée j'ai juré de le donner à vos pères, et ce pays vous est dévolu en héritage.
15 “Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo-Hamathi hadi maingilio ya Sedadi.
Or, voici la frontière du pays: Au nord, depuis la grande mer, le chemin de Hethlon jusqu'à Tsédad,
16 Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi), hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani.
Hamath, Bérotha, Sibraïm située entre la frontière de Damas et la frontière de Hamath, et Hatser-Hattikon située aux confins de l'Hauran.
17 Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasar-Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini.
Et la frontière sera depuis la mer à Hatsar-Enon, frontière de Damas, et le nord, au nord, et la frontière de Hamath. C'est là le côté du nord.
18 Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi bahari ya mashariki na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki.
Et le côté oriental est entre l'Hauran et Damas; et le Jourdain entre Galaad et le pays d'Israël: de la frontière vous mesurerez jusqu'à la mer orientale. C'est là le côté de l'orient.
19 Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba-Kadeshi, kisha utaambaa na Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini.
Le côté méridional sera depuis Thamar, jusques aux Eaux de querelle, Kadès, jusqu'au torrent d'Egypte vers la grande mer. C'est le côté du midi.
20 Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo-Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi.
Et le côté occidental sera la grande mer, depuis la frontière jusque vis-à-vis de Hamath. C'est le côté occidental.
21 “Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli.
C'est ce pays que vous diviserez entre vous selon les tribus d'Israël,
22 Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.
et vous le partagerez au sort par héritages entre vous et les étrangers domiciliés parmi vous, qui auront engendré des fils parmi vous, et vous les regarderez comme indigènes, comme enfants d'Israël; ils partageront au sort avec vous parmi les tribus d'Israël.
23 Katika kabila lolote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema Bwana Mwenyezi.
C'est dans la tribu où l'étranger sera domicilié, que vous lui donnerez son lot, dit le Seigneur, l'Éternel.

< Ezekieli 47 >