< Ezekieli 47 >

1 Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la Hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha Hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa Hekalu ulielekea mashariki). Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa Hekalu, kusini mwa madhabahu.
Puis il me fit retourner vers l'entrée de la maison, et voici des eaux qui sortaient de dessous le seuil de la maison vers l'Orient, car le devant de la maison [était vers] l'Orient; et ces eaux-là descendaient de dessous, du côté droit de la maison de devers le côté Méridional de l'autel.
2 Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini.
Puis il me fit sortir par le chemin de la porte qui regardait vers le Septentrion, et me fit faire le tour par le chemin extérieur jusqu'à la porte extérieure, [même jusques] au chemin qui regardait l'Orient, et voici, les eaux coulaient du côté droit.
3 Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000 kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
Quand cet homme commença de s'avancer vers l'Orient, il avait en sa main un cordeau, et il en mesura mille coudées; puis il me fit passer au travers de ces eaux-là, et elles me venaient jusqu'aux deux chevilles des pieds.
4 Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni.
Puis il mesura mille [autres coudées]; et il me fit passer au travers de ces eaux-là, et elles me venaient jusqu'aux deux genoux; puis il mesura mille [autres coudées]; et il me fit passer au travers de ces eaux-là, et elles me venaient jusques aux reins.
5 Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kuvuka.
Puis il mesura mille [autres] coudées; mais ces eaux-là étaient déjà] un torrent, que je ne pouvais passer à gué; car ces eaux-là s'étaient enflées, c'étaient des eaux qu'il fallait passer à la nage, et un torrent que l'on ne pouvait passer à gué.
6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.
Alors il me dit: fils d'homme, as-tu vu? puis il me fit aller plus outre, et me fit revenir vers le bord du torrent.
7 Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto.
Quand j'y fus revenu, voilà un fort grand nombre d'arbres sur les deux bords du torrent.
8 Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Araba, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Bahari, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi.
Puis il me dit: ces eaux-ci se vont rendre dans la Galilée Orientale, et elles descendront à la campagne, puis elles entreront dans la mer, et quand elles se seront rendues dans la mer, les eaux en deviendront saines.
9 Popote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako.
Et il arrivera que tout animal vivant, qui se traînera partout où entrera chacun des deux torrents, vivra, et il y aura une fort grande quantité de poissons. Lors donc que ces eaux seront entrées là, [les autres en] seront rendues saines, et tout vivra là où ce torrent sera entré.
10 Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuu
Pareillement il arrivera que les pêcheurs se tiendront le long de cette mer, depuis Henguédi jusques à Henhéglajim; [tellement que tout ce circuit] sera plein de filets tous étendus pour prendre du poisson, et le poisson qu'on y pêchera sera en fort grand nombre, chacun selon son espèce, comme le poisson qu'on pêche dans la grande mer.
11 Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi.
Ses marais et ses fosses ont été assignées pour y faire le sel, à cause qu'elles ne seront point rendues saines.
12 Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za mto huu. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.”
Et auprès de ce torrent, [et] sur ses deux bords il croîtra des arbres fruitiers de toutes sortes, dont le feuillage ne flétrira point, et où l'on trouvera toujours du fruit; dans tous leurs mois ils produiront des fruits hâtifs, parce que les eaux de ce torrent sortent du Sanctuaire, et à cause de cela leur fruit sera bon à manger, et leur feuillage servira de remède.
13 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu.
Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel: [ce sont] ici les frontières du pays dont vous vous rendrez possesseurs en titre d'héritage, selon les douze Tribus d'Israël; Joseph [en aura deux] portions.
14 Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu.
Or vous l'hériterez l'un comme l'autre, le pays touchant lequel j'ai levé ma main de le donner à vos pères; et ce pays-là vous écherra en héritage.
15 “Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo-Hamathi hadi maingilio ya Sedadi.
C'est donc ici la frontière du pays, du côté du Septentrion, vers la grande mer, [savoir] ce qui est du chemin d'Héthlon, au quartier par où l'on vient à Tsédad.
16 Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi), hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani.
[Où sont] Hamath, [la contrée tirant] vers Béroth, [et] Sibrajim, qui est entre la frontière de Damas, et entre la frontière de Hamath, [et] les bourgs d'entre-deux, qui sont vers la frontière de Havran.
17 Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasar-Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini.
La frontière donc [prise] de la mer sera Hatsar-henan; la frontière de Damas, et le Septentrion qui regarde [proprement] vers le Septentrion, savoir, la frontière de Hamath, et le canton du Septentrion.
18 Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi bahari ya mashariki na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki.
Mais vous mesurerez le côté de l'Orient depuis ce qui est entre Havran, Damas, Galaad, et le pays d'Israël qui est delà le Jourdain, et depuis la frontière qui est vers la mer Orientale; et [ainsi vous mesurerez] le canton qui regarde [proprement] vers l'Orient.
19 Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba-Kadeshi, kisha utaambaa na Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini.
Puis [vous mesurerez] le côté du Midi [qui regarde proprement] vers le vent d'Autan, depuis Tamar jusques aux eaux des débats de Kadès, le long du torrent jusques à la grande mer; [ainsi vous mesurerez] le canton qui regarde [proprement] vers le vent d'Autan, tirant vers le Midi.
20 Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo-Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi.
Or le côté de l'Occident sera la grande mer, depuis la frontière du [Midi] jusques à l'endroit de l'entrée de Hamath, ce sera là le côté de l'Occident.
21 “Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli.
Après cela vous vous partagerez ce pays-là selon les Tribus d'Israël.
22 Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.
A condition toutefois que vous ferez que ce pays-là écherra en héritage à vous et aux étrangers qui habitent parmi vous, lesquels auront engendré des enfants parmi vous, et ils vous seront comme celui qui est né au pays entre les enfants d'Israël, tellement qu'ils viendront avec vous en partage de l'héritage parmi les Tribus d'Israël.
23 Katika kabila lolote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema Bwana Mwenyezi.
Et il arrivera que vous assignerez à l'étranger son héritage dans la Tribu en laquelle il demeurera, dit le Seigneur l'Eternel.

< Ezekieli 47 >