< Ezekieli 47 >

1 Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la Hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha Hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa Hekalu ulielekea mashariki). Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa Hekalu, kusini mwa madhabahu.
And he turnede me to the yate of the hous; and lo! watris yeden out vndur the threisfold of the hous to the eest; for the face of the hous bihelde to the eest; forsothe the watris camen doun in to the riyt side of the temple, to the south part of the auter.
2 Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini.
And he ledde me out bi the weie of the north yate, and he turnede me to the weie with out the outermere yate, to the weie that biholdith to the eest; and lo! watris flowynge fro the riyt side,
3 Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000 kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
whanne the man that hadde a coord in his hond, yede out to the eest. And he mat a thousynde cubitis, and ledde me ouer thorou the water til to the heelis.
4 Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni.
And eft he mat a thousynde, and ledde me ouer thorouy the watir `til to the knees.
5 Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kuvuka.
And eft he mat a thousynde, and ledde me ouer thorouy the watir `til to the reynes. And he mat a thousynde, the stronde which Y myyte not passe; for the depe watris of the stronde hadden wexe greet, that mai not be waad ouer.
6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.
And he seide to me, Certis, sone of man, thou hast seyn. And he seide to me; and he turnede me to the ryuere of the stronde.
7 Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto.
And whanne Y hadde turned me, lo! in the ryuer of the stronde ful many trees on euer either side.
8 Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Araba, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Bahari, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi.
And he seide to me, These watris that goon out to the heepis of soond of the eest, and goen doun to pleyn places of desert, schulen entre in to the see, and schulen go out; and the watris schulen be heelid.
9 Popote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako.
And ech lyuynge beeste that creepith, schal lyue, whidur euere the stronde schal come; and fischis many ynow schulen be, aftir that these watris comen thidur, and schulen be heelid, and schulen lyue; alle thingis to whiche the stronde schal come, schulen lyue.
10 Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuu
And fisshers schulen stonde on tho watris; fro Engaddi `til to Engallym schal be driyng of nettis; ful many kyndis of fischis therof schulen be, as the fischis of the greet see, of ful greet multitude;
11 Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi.
but in brynkis therof and in maraisis watris shulen not be heelid, for tho `schulen be youun in to places of makynge of salt.
12 Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za mto huu. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.”
And ech tree berynge fruit schal growe on the stronde, in the ryueris therof on ech side; a leef therof schal not falle doun, and the fruyt therof schal not faile; bi alle monethis it schal bere firste fruytis, for the watris therof schulen go out of the seyntuarie; and the fruytis therof schulen be in to mete, and the leeuys therof to medicyn.
13 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu.
The Lord God seith these thingis, This is the ende, in which ye schulen welde the lond, in the twelue lynagis of Israel; for Joseph hath double part.
14 Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu.
Forsothe ye schulen welde it, ech man euenli as his brother; on which Y reiside myn hond, that Y schulde yyue to youre fadris; and this lond schal falle to you in to possessioun.
15 “Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo-Hamathi hadi maingilio ya Sedadi.
This is the ende of the lond at the north coost fro the grete see, the weie of Bethalon to men comynge to Sedala,
16 Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi), hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani.
Emath, Beroth, Sabarym, which is in the myddis bitwixe Damask and niy coostis of Emath, the hous of Thichon, which is bisidis the endis of Auran.
17 Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasar-Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini.
And the ende schal be fro the see `til to the porche of Ennon, the ende of Damask, and fro the north til to the north, the ende of Emath; forsothe this is the north coost.
18 Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi bahari ya mashariki na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki.
Certis the eest coost fro the myddis of Auran, and fro the myddis of Damask, and fro the myddis of Galaad, and fro the myddis of the lond of Israel, is Jordan departynge at the eest see, also ye schulen mete the eest coost.
19 Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba-Kadeshi, kisha utaambaa na Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini.
Forsothe the south coost of myddai is fro Thamar til to the watris of ayenseiyng of Cades; and the stronde til to the greet see, and the south coost at myddai.
20 Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo-Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi.
And the coost of the see is the greet see, fro the niy coost bi streiyt, til thou come to Emath; this is the coost of the see.
21 “Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli.
And ye schulen departe this lond to you bi the lynagis of Israel;
22 Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.
and ye schulen sende it in to eritage to you, and to comelyngis that comen to you, that gendriden sones in the myddis of you; and thei schulen be to you as men borun in the lond among the sones of Israel; with you thei schulen departe possessioun, in the myddis of the lynages of Israel.
23 Katika kabila lolote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema Bwana Mwenyezi.
Forsothe in what euer lynage a comelyng is, there ye schulen yyue possessioun to hym, seith the Lord God.

< Ezekieli 47 >