< Ezekieli 47 >

1 Yule mtu akanirudisha mpaka kwenye ingilio la Hekalu, nami nikaona maji yakitoka chini ya kizingiti cha Hekalu yakitiririkia upande wa mashariki (kwa maana upande wa mbele wa Hekalu ulielekea mashariki). Maji yalikuwa yakitoka chini upande wa kusini wa Hekalu, kusini mwa madhabahu.
Then, [in the vision], the man brought me back to the entrance of the temple. There I saw water flowing out from under the entrance, flowing toward the east. The water was flowing from under the south side of the entrance, south of the altar.
2 Ndipo akanitoa nje kupitia lango la kaskazini na kunizungusha mpaka kwenye lango la nje linaloelekea mashariki, nayo maji yalikuwa yakitiririka kutoka upande wa kusini.
Then the man brought me out of the inner courtyard through the north entryway, and then he led me around to the outer entryway on the east side [of the inner courtyard].
3 Mtu yule alipokwenda upande wa mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake, akapima dhiraa 1,000 kisha akanipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
As the man continued walking toward the east, he had a measuring line in his hand. He measured off (1,750 feet/530 meters), and then led me through water that covered my ankles.
4 Akapima dhiraa 1,000 nyingine na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika magotini. Akapima dhiraa nyingine 1,000 na kunipitisha kwenye hayo maji ambayo yalifika kiunoni.
Then he measured off another (1,750 feet/530 meters) and led me through water that was up to my knees. Then he measured off another (1,750 feet/530 meters) and led me through water that was up to my waist.
5 Akapima tena dhiraa 1,000 nyingine, lakini wakati huu yalikuwa mto ambao sikuweza kuvuka, kwa kuwa maji yalikuwa na kina kirefu ambacho ni cha kuogelea, mto ambao hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kuvuka.
Then he measured off another (1,750 feet/530 meters) and led me through water that had become a river that I could not cross, because the water had risen [very high, with the result that] it would be necessary to swim across it. It was a river that no one could cross [by walking across it].
6 Akaniuliza, “Je, mwanadamu, unaona hili?” Kisha akanirudisha mpaka kwenye ukingo wa huo mto.
Then he said to me, “You human, think carefully about what you have seen.”
7 Nilipofika pale, nikaona idadi kubwa ya miti kila upande wa ule mto.
Then he led me to the bank of that river. There I saw many trees growing on each side of the river.
8 Akaniambia, “Haya maji yanatiririka kuelekea nchi ya mashariki na kushuka mpaka Araba, ambapo huingia Baharini. Yanapomwagikia kwenye hiyo Bahari, maji yaliyoko humo huponywa na kuwa safi.
He said to me, “This water flows east and down into the [Dead] Sea. And when it flows into the [Dead] Sea, its salty water becomes fresh.
9 Popote mto huu uendapo kila kiumbe hai kinachoyaparamia hayo maji kitaishi, nako kutakuwa na samaki wengi mno, mara maji haya yafikapo huko. Maji hayo yatakuwa hai na kila kitu kitakachoishi kule mto uendako.
Wherever the river flows, there will be lots of animals and fish. And there will be lots of fish in the [Dead] Sea, because the water that flows into it will cause the salt water to become (fresh water/water that people can drink). Wherever the river flows, everything [alongside it] will flourish.
10 Wavuvi watasimama kando ya bahari, kuanzia En-Gedi hadi En-Eglaimu huko patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki. Samaki watakuwa wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kuu
Fishermen will stand along the bank [of the Dead Sea to catch fish]. From En-Gedi [on the western side] to En-Eglaim [on the eastern side] there will be places [for fishermen] to spread their fishing nets. There will be many kinds of fish, like there are in the Mediterranean Sea.
11 Lakini madimbwi yake na mabwawa yake hayatakuwa na maji yanayofaa kunywa, bali yatabakia kuwa maji ya chumvi.
But the swamps and marshes [along the shore] will not become fresh; they will be left to the people to use make salt.
12 Miti ya matunda ya kila aina itaota kwenye kingo zote mbili za mto huu. Majani yake hayatanyauka wala haitaacha kuwa na matunda katika matawi yake. Kila mwezi kutakuwa na matunda, kwa sababu maji yatokayo patakatifu yanaitiririkia. Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa dawa.”
Many kinds of fruit trees will grow on both sides of the river. Their leaves will not wither, and they will always have fruit. They will bear fruit every month, because [they will continually get water from] the water [that comes] from the temple. Their fruit will be good to eat and their leaves will be [good] for healing.”
13 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Hii ndiyo mipaka ambayo kwayo mtagawanya hiyo nchi kuwa urithi miongoni mwa hayo makabila kumi na mawili ya Israeli, pamoja na mafungu mawili ya Yosefu.
[In the vision], Yahweh [also] said this to me: “Here is a list of the twelve tribes of Israel and the territory that each tribe must receive. [The descendants of] Joseph will receive two portions; [the tribe of Levi will not receive any].
14 Mtagawa kwa usawa miongoni mwao. Kwa sababu niliapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu, nchi hii itakuwa urithi wenu.
I lifted up my arm and solemnly declared to your ancestors that I would give you this land to own permanently. [So divide the land equally among all of the other tribes].
15 “Huu ndio utakuwa mpaka wa hiyo nchi: “Upande wa kaskazini utaanzia Bahari Kuu kwa njia ya Hethloni kupitia Lebo-Hamathi hadi maingilio ya Sedadi.
These will be the boundaries of the land: On the north side, [it will extend] from the Mediterranean Sea east along the road to Hethlon, past Lebo-Hamath to Zedad,
16 Berotha na Sibraimu (ambao uko kwenye mpaka kati ya Dameski na Hamathi), hadi kufikia Haser-Hatikoni, ambao uko katika mpaka wa Haurani.
to [the cities of] Berothah and Sibraim, which are on the border between Damascus and Hamath. [From there the boundary will extend] as far [the city of] Hazer-Hatticon, which is on the border of the Hauran [region].
17 Hivyo mpaka utaendelea kuanzia Baharini hadi Hasar-Enoni, ukiambaa na mpaka wa kaskazini wa Dameski, pamoja na mpaka wa Hamathi upande wa kaskazini. Huu utakuwa ndio mpaka wa kaskazini.
So the boundary will extend from the [Mediterranean] Sea to [the city of] Hazar-Enan on the border between Hamath to the north and Damascus [to the south]. That will be the northern boundary.
18 Upande wa mashariki mpaka utapita kati ya Haurani na Dameski, kuambaa Yordani na kati ya Gileadi na nchi ya Israeli, hadi bahari ya mashariki na kufika Tamari. Huu utakuwa ndio mpaka wa mashariki.
On the east side, the boundary [will extend] between Hauran and Damascus, [south] along the Jordan [River] between the Gilead [region] and the land of Israel, along the Dead Sea as far as [the town of] Tamar. That will be the eastern boundary.
19 Upande wa kusini utaanzia Tamari hadi kufikia maji ya Meriba-Kadeshi, kisha utaambaa na Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu. Huu utakuwa ndio mpaka wa kusini.
On the south side, the boundary will extend from Tamar [southwest] to the springs near [the town of] Meribah-Kadesh. Then [the boundary will extend west] along the dry riverbed [at the border] of Egypt to the Mediterranean Sea. That will be the southern boundary.
20 Upande wa magharibi, Bahari Kuu itakuwa ndio mpaka hadi kwenye sehemu mkabala na Lebo-Hamathi. Huu utakuwa ndio mpaka wa magharibi.
On the west side, the boundary will be the Mediterranean Sea, north to near Lebo-Hamath.
21 “Mtagawanya nchi hii miongoni mwenu kufuatana na makabila ya Israeli.
You must distribute this land among yourselves, among the tribes of Israel.
22 Mtaigawanya kuwa urithi kwa ajili yenu na kwa ajili ya wageni wanaoishi miongoni mwenu na ambao wana watoto. Wao watakuwa kwenu kama wenyeji wazawa wa Israeli, pamoja na ninyi watagawiwa urithi miongoni mwa makabila ya Israeli.
You must allot the land to be a permanent possession for yourselves, and [also] to be a permanent possession of any foreigners who are living among you and raising their children. You must consider those people to be like you who were born Israelis, and they must be allotted land among the tribes of Israel.
23 Katika kabila lolote mgeni atakapoishi hapo ndipo mtakapompatia urithi wake,” asema Bwana Mwenyezi.
Wherever foreigners are living, you must give them some land to belong to them permanently. [That is what I], Yahweh the Lord, declare.”

< Ezekieli 47 >