< Ezekieli 46 >
1 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
Tak mówi panujący Pan: Brama sieni wnętrznej, która patrzy na wschód słońca, zamkniona będzie przez sześć dni robotnych; ale będzie otworzona w dzień sabatu, także i w dzień nowiu miesiąca będzie otworzona.
2 Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
I przyjdzie książę drogą przysionku bramy zewnątrz, a stanie u podwoi onej bramy, a kapłani sprawować będą całopalenie jego, i spokojne ofiary jego, a pokłoniwszy się na progu bramy, potem wynijdzie, a brama nie będzie zamkniona aż do wieczora,
3 Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
Aby się kłaniał lud onej ziemi u drzwi bramy we dni sabatu i na nowiu miesiąca przed obliczem Pańskiem.
4 Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
Ale całopalenie, które będzie książę sprawował Panu w dzień sabatu, będzie sześć baranków zupełnych i baran zupełny;
5 Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
I ofiara śniedna, efa na barana, i na baranki ofiara śniedna według przemożenia ręki jego, a oliwy hyn na efa.
6 Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
A na dzień nowiu miesiąca niech będzie cielec młody zupełny, i sześć baranków i baran zupełny.
7 Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Także niech ofiaruje efa ofiary suchej przy cielcu, i efa przy baranie, a przy barankach według przemożenia ręki swojej, a oliwy hyn na efa.
8 Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
A książę wchodząc drogą przysionku i bramy pójdzie, i drogą jej odejdzie.
9 “‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
Ale gdy będzie lud onej ziemi wchodził przed obliczność Pańską na święta uroczyste, tedy ten, co wnijdzie drogą bramy od północy, aby się kłaniał, wynijdzie drogą bramy południowej; a kto wnijdzie drogą bramy południowej, wynijdzie drogą bramy pół nocnej; nie wróci się drogą onej bramy, którą wszedł, ale przeciwko niej wynijdzie.
10 Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
A gdy oni wchodzić będą, książę między nimi wchodzić będzie; a gdy odchodzić będą, odejdzie.
11 “‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Także na święta i na uroczyste święta niech będzie ofiara śniedna efa na cielca, i efa na barana, a na baranki, co przemoże ręka jego, a oliwy hyn na efa.
12 Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
A będzieli książę ofiarował ofiarę dobrowolną, całopalenie albo spokojne dobrowolne ofiary Panu, tedy mu niech będzie otworzona brama, która patrzy na wschód słońca, a niech sprawuje całopalenie swoje albo spokojne ofiary swoje, jako ofiarę w dzień sabatu; potem odejdzie, i zamkną bramę, gdy wynijdzie.
13 “‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
Nadto baranka rocznego zupełnego Panu ofiarować będzie co dzień na całopalenie; na każdy poranek baranka ofiarować będzie.
14 Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
Także ofiarę śniedną będzie ofiarował przy nim na każdy poranek szóstą część efy, a oliwy trzecią część hynu na skropienie pszennej mąki, śniedną mówię ofiarę Panu postanowieniem wiecznem ustwicznie.
15 Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
Tak tedy ofiarować będą baranka i ofiarę śniedną i oliwę na każdy poranek, całopalenie ustwiczne.
16 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
Tak mówi panujący Pan: Jeźli komu da książe dar z synów swoich, póki dziedzictwem jego jest, synów jego niech będzie ku osiadłości i ku dziedzicwu ich.
17 Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
Ale jeźli da dar z dziedzictwa swego któremu z sług swoich, tedy będzie jego aż do roku wolności, a potem wróci się na onego księcia; a wszakże dziedzictwo jego mieć będą synowie jego.
18 Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
Nie będzie też nic brał książę z dziedzictwa ludu, gwałtem ich wyrzucając z osiadłości ich; ale z osiadłości swojej da dziedzictwo synom swoim, żeby nie był rozproszony lud mój, nikt z osiadłości swojej.
19 Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
Tedy mię wwiódł przez wejście, które jest przy stronie bramy, do kapłanów, do komórek świętych, które patrzyły na północy, a oto tu było miejsce po obu stronach ku zachodowi;
20 Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
I rzekł do mnie: To jest miejsce, gdzie warzą kapłani ofiarę za występek i za grzech, i smażą ofiarę śniednią, aby nic nie wynosili do sieni zewnętrznej ku poświęcaniu ludu.
21 Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
Potem mię wywiódł do sieni zewnętrznej, i obwiódł mię po czterech kątach sieni, a oto sień była w każdym kącie onej sieni.
22 Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Na czterech węgłach onej sieni były sieni z kominami na czterdzieści łokci wdłuż a na trzydzieści łokci wszerz, jednaż miara onych czterech sieni narożnych.
23 Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
A w onych czterech były kuchnie w około, także ogniska poczynione w onych kuchniach w około.
24 Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”
I rzekł mi: Te miejsca są tych, którzy warzą, gdzie słudzy domu warzą ofiary ludu.