< Ezekieli 46 >

1 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
Voici ce que dit le Seigneur Dieu: La porte du parvis intérieur qui regarde vers l’orient sera fermée les six jours dans lesquels on travaille; mais le jour du sabbat elle sera ouverte; et aussi le jour des calendes elle sera ouverte.
2 Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
Et le prince entrera par la voie du vestibule de la porte de dehors; et il s’arrêtera sur le seuil de la porte; et les prêtres offriront son holocauste, et ses oblations pacifiques; il adorera sur le seuil de la porte, et il sortira; mais la porte ne sera pas fermée jusqu’au soir.
3 Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
Et le peuple du pays adorera aussi devant le Seigneur à l’entrée de cette porte aux sabbats et aux calendes.
4 Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
Or le prince offrira au Seigneur cet holocauste: le jour du sabbat six agneaux sans tache, et un bélier sans tache;
5 Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et le sacrifice d’un éphi de farine par bélier; mais pour les agneaux le sacrifice sera ce que donnera sa main; et un hin d’huile par chaque éphi.
6 Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
Mais au premier jour des calendes, un veau sans tache, pris d’un troupeau; et six agneaux et six béliers sans tache seront ajoutés.
7 Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et il offrira en sacrifice un éphi de farine par veau, un éphi aussi par bélier; mais quant aux agneaux, le sacrifice sera selon que sa main aura trouvé, et un hin d’huile par chaque éphi.
8 Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
Et lorsque le prince doit entrer dans le temple, qu’il entre par la voie du vestibule de la porte orientale; et qu’il sorte par la même voie.
9 “‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
Mais lorsque le peuple du pays entrera en la présence du Seigneur dans les solennités, que celui qui entre par la porte de l’aquilon, pour adorer, sorte par la voie de la porte du midi; et que celui qui entre par la porte du midi, sorte par la voie de la porte de l’aquilon; nul ne retournera par la voie de la porte par laquelle il sera entré; mais il sortira par celle d’en face.
10 Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
Mais le prince au milieu d’eux, entrera avec ceux qui entrent, et sortira avec ceux qui sortent.
11 “‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
Et aux jours de foire et dans les solennités, le sacrifice sera un éphi de farine par veau et un éphi par bélier; mais pour les agneaux, le sacrifice sera selon que la main de chacun aura trouvé, et un hin d’huile par chaque éphi.
12 Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
Or lorsque le prince offrira au Seigneur un holocauste volontaire, ou des victimes pacifiques volontaires, on lui ouvrira la porte qui regarde vers l’orient; et il offrira son holocauste et ses victimes pacifiques, comme cela a coutume de se faire au jour du sabbat; et il sortira, et la porte sera fermée après qu’il sera sorti.
13 “‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
Et il offrira chaque jour en holocauste au Seigneur un agneau de la même année, sans tache; et il l’offrira toujours le matin.
14 Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
Et il offrira tous les matins en sacrifice pour cet agneau la, sixième partie d’un éphi, et la troisième partie d’un hin d’huile, afin qu’elle soit mêlée avec la farine; c’est là le sacrifice qu’il est obligé, selon la loi, d’offrir au Seigneur, sacrifice continuel et perpétuel.
15 Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
Il immolera l’agneau, et offrira le sacrifice et l’huile, tous les matins; holocauste éternel.
16 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Si le prince fait un don à l’un de ses fils, ce sera son héritage à lui et à ses fils; ils le posséderont héréditairement.
17 Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
Mais s’il fait un legs de son héritage à l’un de ses serviteurs, il ne lui appartiendra que jusqu’à l’année de rémission; et alors il retournera au prince, mais son héritage appartiendra à ses fils.
18 Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
Et le prince ne prendra rien par violence de l’héritage du peuple, ni de ses biens; mais de son bien propre il donnera un héritage à ses fils, afin que parmi mon peuple, personne ne soit écarté de ce qu’il possède.
19 Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
Et il m’introduisit par l’entrée qui était à côté de la porte, dans les chambres du sanctuaire, près des prêtres, chambres qui regardaient vers l’aquilon; et là était un lieu tourné vers l’occident.
20 Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
Et il me dit: C’est le lieu où les prêtres cuiront les viandes des victimes immolées pour le péché et pour le délit; où ils cuiront ce qui sert au sacrifice; afin qu’ils ne les portent point dans le parvis extérieur, et que le peuple ne soit pas sanctifié.
21 Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
Et il me fit sortir dans le parvis extérieur, et me mena aux quatre coins du parvis; et voici qu’il y avait une petite cour au coin du parvis; à chaque coin du parvis il y avait une petite cour.
22 Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
Ces petites cours ainsi disposées aux quatre coins du parvis, avaient quarante coudées de long, et trente de large; les quatre étaient d’une même mesure.
23 Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
Et une muraille enfermait tout autour les quatre petites cours; et des cuisines avaient été construites sous les portiques tout autour.
24 Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”
Et il me dit: Voici la maison des cuisines, dans laquelle les ministres de la maison du Seigneur cuiront les victimes du peuple.

< Ezekieli 46 >